Utafiti uliofanyika kati ya mama mwenye furaha na aliye na hasira wanapowalea watoto wao na hata katika uhusiano wao na watu wengine. Utafiti huu ulidhihirisha baadhi ya vitu tofauti ambavyo wanawake katika vikundi hivi hufanya.
Vitu ambavyo mama mwenye furaha hufanya tofauti na mwenye hasira

Mama wenye furaha hawatarajii kazi bila doa. Na sio kwa watu wengine tu mbali pia kwa wao wenyewe. Mama aliye na furaha ana tarajia mema kutoka kwa watoto wake na yeye mwenyewe bila kuwa na matarajio ya juu zaidi. Hakuna aliye bila doa. Wanawake wenye furaha wanafahamu hii. Wanaelewa kuwa, ni vigumu kutofanya makosa na pia kila kosa huandamana na funzo.
Mama wenye furaha hung'aa. Watu wenye furaha kwa ujumla huwa vyanzo vya furaha. Wanawake wenye furaha huandamanishwa na hisia chanya wanapoingia chumbani na pia ni chanzo cha utunzaji na mapenzi.
Wao huchagua vita vizuri. Haufai kupigana katika vita vyote. Na bila shaka haingilii kati katika vita vyote maishani mwa watoto wake. Wakati mwingine, anawaacha ili wafahamu wanachopaswa kufanya peke yao, huku kunasaidia katika kukuza utu wao. Watoto wanahitaji kupatiwa nafasi yao na mama mwenye furaha huwa na mipaka.
Mama aliye na furaha huwa mwaminifu. Mtu aliye na furaha huwa mwaminifu na sio kwa kina mama peke yake. Mama aliye na furaha ana uwezo wa kutimiza ahadi zake na kuipa familia yake juhudi zake zote.

Mama aliye na furaha hucheza na watoto wao. Kucheza na watoto huwapatia wazazi chanya cha kuwa na utangamano zaidi. Mama mwenye furaha hataona aibu kucheza na watoto wake nyumbani na wanapoenda kwenye buga.
Mwanamke mwenye furaha husikiliza kwa makini. Mama mwenye furaha ana uwezo wa kumsikiliza mtoto wake na kuelewa msaada anaotaka kutoka kwake. Kumsikiliza mtoto kunamsaidia kuhisi ako salama kukueleza anapokuwa na tatizo lolote.
Mama aliye na furaha huwapatia watoto wake maarifa. Mama mwenye furaha huwasaidia watoto wake kukua kwa kuongeza maarifa yao. Hufanya hivi kwa kusoma na watoto wao na kuwafunza.
Wanapenda kuwa na furaha. Wakati wote wanapenda kuwa na furaha na kuwa na mtazamio chanya maishani. Kuwa na furaha kunawasaidia watoto kuwa na furaha pia kwa kuiga mfano wa mama.
Soma Pia: Faida Za Kufanya Mazoezi Katika Mimba Kwa Mama Na Mtoto!