Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Mambo 8 Kila Mwanamke Anapaswa Kufanya Kabla Ya Kufunga Ndoa

3masomo ya dakika
Mambo 8 Kila Mwanamke Anapaswa Kufanya Kabla Ya Kufunga NdoaMambo 8 Kila Mwanamke Anapaswa Kufanya Kabla Ya Kufunga Ndoa

Kufanya mambo haya kutakupatia maarifa na kukufanya uwe na uwezo wa kufanya uamuzi bora zaidi maishani. Ni jukumu lako kama binti asiye katika uhusiano kufanya mambo mazuri zaidi maishani kabla ya kufunga ndoa. Kufanya vitu hivi kutakusaidia kuwa mwerevu zaidi na kujua mambo unayo na usiyo paswa kufanya. Soma makala yetu ya mambo ambayo mwanamke anapaswa kufanya kabla ya kuingia katika ndoa!

Mambo 8 mwanamke anapaswa kufanya kabla ya kufunga ndoa

Mambo 8 Kila Mwanamke Anapaswa Kufanya Kabla Ya Kufunga NdoaMambo 8 Kila Mwanamke Anapaswa Kufanya Kabla Ya Kufunga Ndoa

 

  1. Jifunze jinsi ya kupika

Tofauti na imani za watu kuwa kila mwanamke anapaswa kujua kupika ili ampikie bwana yake, kujifunza kupika kwa mwanamke kuna umuhimu tofauti. Ukiwa peke yako bila mchumba, una wakati mwingi, kwa hivyo katika wakati huu, utaweza kujipikia vyakula vinavyo kufurahisha zaidi. Pia, unapo pata wageni utaweza kuwa burudisha na ustadi wako wa mapishi.

2. Fanya vitu vinavyo kupendeza katika wakati wako wa ziada

Unapokuwa peke yako, una wakati mwingi wa mapumziko, ni vyema kufahamu vitu unavyo vipendelea, katika wakati huu, utaweza kuvifanya badala ya kubaki kwenye nyumba ama kulala wakati wote. Kufahamu mambo yanayo kufurahisha kuta kusaidia kuto mngoja mchumba wako wakati wote ili mfanye mambo pamoja. Ni muhimu sana kuwa na maisha yako kando na maisha yenu pamoja kama wachumba.

3. Kuvunjwa moyo

mchumba mwaminifu

Ni kawaida kuwa na hofu ya kuvunjwa moyo, lakini usipo ingia katika uhusiano na kugundua mambo usiyo paswa kumkubalisha mpenzi wako afanye, huenda ukafanyiwa mambo haya na wakati huo hauna chaguo la kutoka kwa ndoa ni ya muda mrefu.

4. Kufahamu maoni yako kuhusu watoto

Katika siku za hapo awali, ilikuwa lazima kwa mwanamke kupata watoto katika ndoa. Ila siku hizi mambo yame badilika na wanawake wana weza kuchagua ikiwa wangependa kupata watoto ama la na pia idadi ya watoto ambao wangependa. Unapo fanya hivi, utakuwa wazi na mchumba wako na kugundua kama mna maono sawa, ili kuepuka vurugu za kuwa na maoni tofauti kuhusu mada fulani.

5. Zuru

Kuzuru kuna kusaidia kuona pande tofauti za dunia na kupatana na watu mbalimbali. Kufanya ziara peke yako kuna kusaidia kuwa jasiri zaidi. Huenda ikawa vigumu kufanya hivi unapo ingia kwenye uhusiano na baadaye kupata watoto kwani una majukumu zaidi na hauna wakati tosha. Kwa hivyo, hakikisha unafanya hivi ungali peke yako kabla ya kuingia kwenye uhusiano.

6. Soma mambo tofauti

Ni kawaida kuwa na mambo machache ambayo ungependa kufahamu jinsi ya kuyafanya na hata kupata vyeti zaidi. Ungali peke yako, una wakati tosha wa kufanya hivi. Kwa hivyo hakikisha unapata vyeti zaidi katika kipindi hiki.

7. Tengeneza malengo yako ya kifedha

Ni rahisi kuwa na majaribio ya kutumia fedha zako kiholela holela kwani wakati huu hauna majukumu mengi. Fahamu umuhimu wa kuhifadhi pesa hasa katika kipindi ambacho mambo yanaenda mrama. Unaweza anza kuwekeza baadhi ya kiwango cha fedha zako.

8. Anza kufanya mazoezi

Mazoezi haya kusaidii kuwa na mwili unao pendeza tu, mbali kuwa na afya nzuri ya kiakili na kihisia. Kwa hivyo hakikisha kuwa umejiunga na darasa za kufanya mazoezi.

Soma Pia: Jinsi Ya Kufurahia Maisha Yako Ya Ndoa Kama Mwafrika

img
Yaliandikwa na

Risper Nyakio

  • Nyumbani
  • /
  • Lifestyle
  • /
  • Mambo 8 Kila Mwanamke Anapaswa Kufanya Kabla Ya Kufunga Ndoa
Gawa:
  • Mambo Ambayo Mwanamme Anaangalia Kwa Mwanamke Kabla Ya Kumuoa

    Mambo Ambayo Mwanamme Anaangalia Kwa Mwanamke Kabla Ya Kumuoa

  • Mambo 5 Muhimu Unayo Paswa Kufanya Kabla Ya Kufanya Mazoezi

    Mambo 5 Muhimu Unayo Paswa Kufanya Kabla Ya Kufanya Mazoezi

  • Jinsi Ya Kukabiliana Na Hamu Ya Ngono Kabla Ya Ndoa

    Jinsi Ya Kukabiliana Na Hamu Ya Ngono Kabla Ya Ndoa

  • Kwa Nini Una Harakisha Kufunga Ndoa?

    Kwa Nini Una Harakisha Kufunga Ndoa?

  • Mambo Ambayo Mwanamme Anaangalia Kwa Mwanamke Kabla Ya Kumuoa

    Mambo Ambayo Mwanamme Anaangalia Kwa Mwanamke Kabla Ya Kumuoa

  • Mambo 5 Muhimu Unayo Paswa Kufanya Kabla Ya Kufanya Mazoezi

    Mambo 5 Muhimu Unayo Paswa Kufanya Kabla Ya Kufanya Mazoezi

  • Jinsi Ya Kukabiliana Na Hamu Ya Ngono Kabla Ya Ndoa

    Jinsi Ya Kukabiliana Na Hamu Ya Ngono Kabla Ya Ndoa

  • Kwa Nini Una Harakisha Kufunga Ndoa?

    Kwa Nini Una Harakisha Kufunga Ndoa?

Pata ushauri wa mara kwa mara kuhusu ujauzito wako na mtoto wako anayekua!
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • Zaidi
    • TAP Jamii
    • Tangaza Nasi
    • Wasiliana Nasi
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
Kutuhusu|Timu|Sera ya Faragha|Masharti ya kutumia |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it