Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Mambo 7 Usiyofahamu Kuhusu Watoto Wachanga

2 min read
Mambo 7 Usiyofahamu Kuhusu Watoto WachangaMambo 7 Usiyofahamu Kuhusu Watoto Wachanga

Je, ulifahamu kuwa watoto wachanga wa kiume husimamisha uume wao? Tazama mambo usiyofahamu kuhusu watoto wachanga!

Wazazi wapya hasa wa mara ya kwanza huwa na maswali mengi kuhusu watoto wadogo na safari hii mpya ya ulezi. Tuna angazia mambo usiyofahamu kuhusu watoto wachanga, ili kuwapa maarifa kuhusu mambo ya kutarajia kuona katika watoto wao yaliyo ya kawaida.

Mambo usiyofahamu kuhusu watoto wachanga

mambo usiyofahamu kuhusu watoto wachanga

1.Watoto hulia bila machozi

Baada ya watoto kuzaliwa, wao huanzia kulia kati ya wiki 2-3 lakini bila kutoa machozi. Katika miezi ya kwanza michache, watoto husumbua sana hasa masaa ya jioni. Mtoto husumbua zaidi katika wiki ya 6 na ya 8.

2. Choo cha mtoto hakinuki

Choo cha mtoto mchanga huwa na ute na maji maji kutoka tumboni na chochote ambacho mtoto amekula tangu kuzaliwa na hakina harufu. Harufu kwenye choo cha mtoto husababishwa na bakteria zinazoenea tumboni. Choo cha kwanza cha mtoto huwa cha rangi ya kijani kisha kubadilika na kuwa kinjano kisha hudhurungi.

3. Alama zingine za kuzaliwa hupotea

Watoto wachanga huwa na alama nyingi za kuzaliwa. Nyingi ambazo huendelea kufifia japo wanapoendelea kukua.

4. Tonsils huwa na tezi za kujua ladha ya chakula

Mtoto mdogo huwa na tezi zinazoweza kujua ladha ya chakula na huwa sawa na zile katika vijana wadogo. Tezi kwenye watoto wachanga huwa zimekuchua sehemu kubwa hadi kufika kwenye upande wa nyuma wa koo. Tezi hizi zinamsaidia kubainisha kati ya vitu vitamu, vitu chachu na vichungu.

mambo usiyofahamu kuhusu watoto wachanga

5. Watoto wa kiume husimamisha uume wao

Mara nyingi hufanyika mtoto anapotaka kuenda haja ndogo. Unapombadilisha diaper, utaweza kuona. Mama anapofanyiwa ultrasound akiwa na mimba, jambo hili huonekana pia. Sio jambo la kutia shaka kwani ni kawaida.

6. Hulala mara nyingi kwa upande wa kulia

Asilimia 15 ya watoto wachanga wanapenda kuelekeza uso wao kwenye upande wa kushoto wanapolala kwa mgongo. Kupendelea kulala kwa upande huu huchukua miezi kabla ya kutokomea. Kuchagua kulala kwa upande wa kulia kunaweza kutumika kueleza kwa nini watu zaidi wanatumia mkono wa kulia ikilinganishwa na wa kushoto.

7. Kiwango kikubwa cha seli za ubongo

Ubongo wa mtoto mchanga huwa na seli nyingi na idadi ya seli hizi zitaongezeka kwa mara mbili katika mwaka wa kwanza. Una seli za neva nyingi ikilinganishwa na za mtu mkubwa. Hata hivyo seli hizi hufa, watu wazima wana seli za neva chache ikilinganishwa na walivyokuwa wakiwa wachanga.

Soma Pia:Kwa Nini Watoto Wachanga Hulia? Sababu 5 Kuu Zinazowafanya Watoto Wachanga Kulia

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Baby
  • /
  • Mambo 7 Usiyofahamu Kuhusu Watoto Wachanga
Share:
  • Vyakula Katika Mimba vya Kuboresha Ukuaji wa Ubongo wa Mtoto 

    Vyakula Katika Mimba vya Kuboresha Ukuaji wa Ubongo wa Mtoto 

  • Ishara 5 Kuwa Una Mtoto Mwerevu

    Ishara 5 Kuwa Una Mtoto Mwerevu

  • Ishara Kuwa Mama Atajifungua Mtoto Mwenye IQ ya Juu

    Ishara Kuwa Mama Atajifungua Mtoto Mwenye IQ ya Juu

  • Vyakula Katika Mimba vya Kuboresha Ukuaji wa Ubongo wa Mtoto 

    Vyakula Katika Mimba vya Kuboresha Ukuaji wa Ubongo wa Mtoto 

  • Ishara 5 Kuwa Una Mtoto Mwerevu

    Ishara 5 Kuwa Una Mtoto Mwerevu

  • Ishara Kuwa Mama Atajifungua Mtoto Mwenye IQ ya Juu

    Ishara Kuwa Mama Atajifungua Mtoto Mwenye IQ ya Juu

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it