Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Vitu Muhimu Kwa Wanaume Kufanya Kabla Ya Kujaribu Kupata Mtoto

2 min read
Vitu Muhimu Kwa Wanaume Kufanya Kabla Ya Kujaribu Kupata MtotoVitu Muhimu Kwa Wanaume Kufanya Kabla Ya Kujaribu Kupata Mtoto

Kuna mambo yanayo athiri uzalishaji wa kiume ambayo wanaume wanastahili kuangazia kama kubadili mitindo yao ya maisha ili kuboresha nafasi zao za kutunga mimba.

Rutuba ya kiume haitazamiwi kama jambo kubwa hadi pale ambapo wanandoa wanachukua muda mrefu kutunga mimba. Hata kama ni baada ya mama kufanyiwa kipimo. Kuna mambo yanayo athiri uzalishaji wa kiume ambayo wanaume wanastahili kuangazia kama kubadili mitindo yao ya maisha ili kuboresha nafasi zao za kutunga mimba na kupata ushauri kabla ya kutunga mimba.

Kuna baadhi ya shirika zinazo husika na kuwaelimisha wanaume kuhusu afya yao ya uzalishaji. Ikiwa utajaribu kupata watoto, ni vyema kwako kuwa makini na afya yako kwani afya ya manii ni muhimu kwa mtoto. Ni muhimu kwa wanaume kufanya mtindo wa kutembelea vituo vya afya mara kwa mara hata wasipokuwa na fikira za kupata watoto. Wasipo jitunza, wana hatarisha maisha ya mama na mtoto. Watoto ambao baba zao wana matatizo ya kiafya kama kisukari, uzito wa kupindukia na kuvuta sigara, wako katika hatari ya kupata shinikizo la damu.

Mambo matatu yanayo athiri uzalishaji wa kiume

Uzito

mambo yanayo athiri uzalishaji wa kiume

Wanaume wengi hawana habari kuwa uzito wao unaweza kuathiri uwezo wa wachumba wao kupata mimba. Kuwa na uzani wa kupindukia kunaweza punguza idadi na mwendo wa manii. Na kumaanisha kuwa mchumba atachukua muda zaidi kushika mimba. Wanaume walio na uzani wa mwili wa kupindukia wana kiwango cha chini cha testosterone na kuathiri uwezo wao wa kuwa na mapenzi mara kwa mara.

Mtindo wa maisha

maswali maarufu katika mimba

Mitindo hasi ya maisha kama uvutaji wa sigara, kutumia mihadarati na kula vyakula visivyo na manufaa mwilini. Uvutaji wa sigara unaweza athiri watoto wako. Wanawake wameelimishwa na sio rahisi kupata mjamzito akivuta sigara. Ila, mwanamme anaye vuta sigara anaweza kuathiri mtoto wake ambaye hajazaliwa? Wanaume wanaovuta sigara huwa na nafasi changa za kutunga mimba ikilinganishwa na wanaume wasio vuta sigara. Ni vyema kwa wanaume kupunguza na kisha kuwacha utumiaji wa sigara muda kabla ya kujaribu kupata watoto.

Umri

mambo yanayo athiri uzalishaji wa kiume

Ubora na kiwango cha manii hupunguka wanaume wanapotimiza umri wa miaka 45. Na kumaanisha kuwa inachukua muda mrefu zaidi kwao kupata mtoto na kuwa na nafasi za juu kupoteza mimba. Baadhi ya wakati mwanamke anaposhuhudia matatizo katika mimba yake, huenda ikawa chanzo ni mwanamme hata kama yeye ndiye atakaye athiriwa. Wanaume wanafahamu kuwa wanawake wana muda ambao wanatatizika kupata mimba, ila hawafahamu kuwa wao pia wana saa ya kibiolojia.

Chanzo: Healthline

Soma Pia: Njia 5 Za Kuboresha Mfumo Wa Uzazi Katika Wanawake

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Pregnancy
  • /
  • Vitu Muhimu Kwa Wanaume Kufanya Kabla Ya Kujaribu Kupata Mtoto
Share:
  • Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

    Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

  • Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

    Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

  • Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

    Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

  • Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

    Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

  • Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

    Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

  • Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

    Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it