Ikiwa mara kwa mara wewe hujipata ukiwa mhasiriwa wa kuwachwa na wanaume, huenda ukawa unashangaa kinacho endelea, mambo yanayo wafukuza wanaume na kwa nini huwezi pata mapenzi.
Mambo Yanayo Wafukuza Wanaume

Kuna nyakati ambapo unaweza hisi kuwa wanaume wanajitenga nawe na kuwa wangependa kuwa peke yao. Lakini huenda ikawa unafanya kitu kinacho watia kiwewe, na kumaanisha kuwa una haribu nafasi zako za kuwa katika uhusiano wenye afya.
Baadhi ya wakati, wanawake huenda bila ufahamu wao waka onyesha mhemko usio wa kawaida na kufanya jinsia tofauti kuwa ona kama wasio na usalama ama imani na katika visa vingi, wanaume hupata ikiwa vigumu kuwa na mtu kama huyo. Lakini ikiwa unafanya hivi, bado una shaka kuwa hauna mchumba?
Kosa lingine ambalo mabinti wengi hufanya ni kutarajia kuwa wanaume wata wacha maisha yao ya hapo awali na kuwa na maisha mapya yanayo mzunguka mwanamke. Hilo halita tendeka! Na sio kuhusu wakati tu, ila kuhusu mapenzi na kuangazia unayo taka. Mpende kwa utu wake na sio kwa sababu anakupatia sifa zisizo koma.
Uhusiano sio maisha yako yote, unapaswa kuwa na maisha yako sio kukwamilia kwa mchumba wako wakati wote. Ni muhimu kuwa na wakati kando, na kunapaswa kuwa na mambo mengine yanayo endelea maishani mwako sio katika uhusiano wako tu. Kwa hivyo jumuika na marafiki wako wa kike, fanya mambo unayo yapendelea, na usikubalishe uhusiano wako uathiri kazi yako.
- Kuchukua jukumu la kuwa mamake

Mwanamme hahitaji mwanamke mwingine kuchukua jukumu la kuwa mamake na kumchukulia kama mtoto wake. Hauhitaji kumwambia anacho stahili kufanya ama jinsi ya kufanya mambo yake. Nyinyi ni washirika ila hakuna aliye mtoto wa mwingine.
- Kupeleka mambo kwa kasi sana
Usipate starehe kasi sana, punguza mwendo. Uhusiano huchukua muda. Kuweni marafiki kwa muda na unapokuwa tayari, mnaweza kuwa na uhusiano. Usiwe na shaka kuhusu kufikia hatua ifuatayo. Furahikia kila sehemu ya uhusiano wenu.
Kuwa na wivu sio jambo linalo pendeza. Wanaume wanataka wanawake wanao jiamini na wasio hitaji mwanamme kuwakumbusha kuwa wanapendeza. Jifunze jinsi ya kum-amini mchumba wako ama kuwa na wivu kwani huenda ukafanya akose hamu ya kuwa katika uhusiano nawe.
Soma Pia: Mambo ya kuvutia ambayo wanandoa wanaweza jaribu kitandani