Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Jinsi Ya Kumdhamini Mchumba Baada Ya Kujifungua Mbali Na Kufanya Ngono

2 min read
Jinsi Ya Kumdhamini Mchumba Baada Ya Kujifungua Mbali Na Kufanya NgonoJinsi Ya Kumdhamini Mchumba Baada Ya Kujifungua Mbali Na Kufanya Ngono

Kurejelea mapenzi baada ya kujifungua huchukua muda, ili kumpa mama wakati tosha wa kupona. Hata hivyo, wanandoa wanaweza fanya mambo haya kabla!

Mama anapojifungua, anaanza maisha mapya na kukikaribisha kiumbe kingine maishani na nyumbani mwake. Maisha haya mapya huwa na mabadiliko mengi. Hasa kama ni mama wa mara ya kwanza, angali anajifunza jinsi ya kumtunza mtoto na kurekebisha ratiba yake iandamane na ratiba ya kulala kwa mtoto.  Katika kipindi hiki, mama ana mawazo mengi, kumtunza mtoto, kumlisha, kumnyonyesha, kumbadili nepi, na huenda akawa hana hamu ya mapenzi baada ya kujifungua. Na hata ikiwa anayo, iko chini sana kwani nishati nyingi inatumika kumtunza mtoto. Mbali na hayo, angali anapona kutokana na kujifungua na ni vyema kuchukua muda kupona kabla ya kurejelea tendo la ndoa.

Kuzungumza na mchumba wako kuhusu ngono baada ya kujifungua

virutubisho muhimu kwa mama anaye nyonyesha

Kuwa na mazungumzo wazi na mchumba wako ni muhimu katika kipindi hiki. Huenda wakahisi kana kwamba mtoto amechukua nafasi yao na hawapati muda na bibi zao tena. Mama anaweza fanya mambo haya:

Kuzungumza kwa uwazi. Mweleze mchumba wako unavyo hisi kuhusu ngono baada ya kujifungua. Unacho ogopa, unacho kifurahia na umweleze unapohisi kuwa utakuwa tayari kufanya mapenzi tena.

Mweleze unachotaka. Je, ungependa kufanya mapenzi wakati huu, ama vitendo vingine vya kimapenzi. Kumbuka kuwa mpenzi wako pia ana mahitaji yake, mpe sikio anapokueleza anachotaka pia.

Upe mwili wako muda upone. Miili ya wanawake ni tofauti na huchukua muda tofauti kupona baada ya kujifungua. Usikilize mwili wako. Ukihisi kuwa unahitaji muda zaidi kabla ya kurejelea kufanya mapenzi, ni sawa.

Njia zingine za kuwa karibu na mchumba wako bila ngono

mapenzi baada ya kujifungua

Kuna njia nyingi ambazo wanandoa wanaweza kuwa na utangamano bila ya kufanya mapenzi. Kama vile:

Kuwa na wakati pamoja. Ni vyema kwa wanandoa kuhakikisha kuwa wanazidi kupata chanya cha kuwa peke yao, mbali na kumtunza mtoto. Hata dakika chache kwa siku, kuzungumza kuhusu jinsi siku zao zimekuwa.

Busu. Wakati ambapo kufanya ngono hakuwezekani hasa siku za kwanza baada ya kujifungua, wazazi wanaweza jaribu kuonyeshana mapenzi kwa njia zingine kama kubusiana.

Kumtunza mwenzi wako. Mchumba wa kiume anaweza jaribu kumtunza bibi yake kwa kumfanyia vitu vidogo vinavyo mjaza na furaha kama vile kumkanda miguu, kumsaidia kumbadili mtoto nepi ili mama apate wakati wa kupumzika. Ni vitendo hivi vidogo vinavyo mhakikishia kuwa angali anapendwa na kudhaminiwa. Na hata kama mngali hamjarejelea mapenzi baada ya kujifungua, atahisi mapenzi yako kwake.

Chanzo: Healthline

Soma Pia: Kwa Nini Watu Wasio Na Usawa Hawawezi Kuwa Na Uhusiano Wa Kimapenzi?

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Relationship & Sex
  • /
  • Jinsi Ya Kumdhamini Mchumba Baada Ya Kujifungua Mbali Na Kufanya Ngono
Share:
  • Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

    Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

  • Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

    Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

  • Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

    Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

  • Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

    Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

  • Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

    Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

  • Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

    Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it