Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Sigara Katika Mimba Zina Madhara Gani Kwa Fetusi: Maswali Maarufu Katika Mimba

2 min read
Sigara Katika Mimba Zina Madhara Gani Kwa Fetusi: Maswali Maarufu Katika MimbaSigara Katika Mimba Zina Madhara Gani Kwa Fetusi: Maswali Maarufu Katika Mimba

Punde tu mama anapo gundua kuwa ana mimba, huenda akapata wasiwasi kuhusu vitu anavyo paswa kuchukua na madhara yake kwa mimba. Tazama baadhi ya maswali maarufu zaidi katika mimba!

Punde tu mama anapo gundua kuwa ana mimba, huenda akapata wasiwasi kuhusu vitu anavyo paswa kuchukua na madhara yake kwa mimba. Tazama baadhi ya maswali maarufu zaidi katika mimba!

Maswali Maarufu Katika Mimba

  • Kaffeini

maswali maarufu katika mimba

Kaffeini nyingi ina athari hasi kwa ujauzito. Mwanamke mwenye mimba anapaswa kupunguza kiwango cha kaffeini anacho chukua kwa siku. Sio zaidi ya vikombe viwili kwa siku.

Hatari kwa fetusi. Kuchukua kaffeini nyingi kunamweka mama katika hatari ya kupoteza mimba.

Kudhibiti kiwango cha kaffeini

Si rahisi kukoma kutumia kaffeini kwa kasi ikiwa ulikuwa umezoea hapo awali. Punguza kiwango unacho chukua kila siku. Kisha baadaye uanze kutumia kinywaji kingine badala ya kaffeini.

  • Vileo

maswali maarufu katika mimba

Mama mjamzito anapaswa kujitenga na vileo kabisa anapo kuwa na mimba. Hakuna kiwango kilicho salama katika mimba, hata kuonja kidogo. Kuna magonjwa kama vile fetal alcohol syndrome inayo husishwa na kunywa pombe katika mimba.

Hatari kwa fetusi. Vileo na pombe katika mimba vina husishwa na ulemavu wa kifizikia, kiakili na kitabia katika mtoto.

Mama anapo kunywa vileo, vinamfikia mtoto kupitia kwa placenta. Na kubaki kwenye mfumo wa mtoto kwa muda mrefu. Mfumo wake wa neva una athiriwa.

Ushauri kwa mama

Hakuna shaka unapo kunywa pombe kabla ya kufahamu hali yako ya mimba. Ila unapo jua, kuwa unatarajia, koma kunywa pombe. Ikiwa unatatizika kuwacha pombe, zungumza na mtaalum wa afya akushauri.

  • Uvutaji wa sigara

 

maswali maarufu katika mimba

Kuvuta sigara katika mimba huwa na hatari nyingi kwa mtoto mchanga. Moshi ya sigara hufikia fetusi kupitia kwa placenta.

Athari kwa fetusi. Kemikali zilizoko kwenye sigara zina hatari ya kumfanya mama ajifungue kabla ya wakati, kujifungua mtoto aliye fariki ama mtoto aliye na uzani wa chini.

  • Dawa zilizo nunuliwa kwa kemia

Mjamzito anapaswa kujitenga na dawa zilizo nunuliwa kwa kemia bila kushauriwa na daktari.

Hatari kwa fetusi. Kuna baadhi ya dawa ambazo huwa na athari hasi kwa fetusi. Mama asipo soma kijikaratasi kinacho andamana na dawa hizo, huenda akahatarisha maisha ya fetusi.

Mama anastahili kutumia dawa alizo shauriwa na mtaalum wa afya. Hakikisha kuwa daktari anaye kutibu anafahamu hali yako ya mimba. Ili aweze kujua dawa zitakazo kufaa na zilizo hatari kwako. Hata unapo umwa na kichwa, jizuie kununua dawa kwa duka la dawa bila kudhibitisha ikiwa ni salama kwa hali yako.

Soma Pia:Hatua 3 Za Uchungu Wa Mama Katika Mimba Na Jinsi Zinavyo Tendeka

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Uncategorized
  • /
  • Sigara Katika Mimba Zina Madhara Gani Kwa Fetusi: Maswali Maarufu Katika Mimba
Share:
  • Vyakula 7 Bora Vya Kichefuchefu na Ugonjwa wa Asubuhi

    Vyakula 7 Bora Vya Kichefuchefu na Ugonjwa wa Asubuhi

  • Jinsi ya Kukabiliana na Ugonjwa wa Asubuhi Katika Mimba

    Jinsi ya Kukabiliana na Ugonjwa wa Asubuhi Katika Mimba

  • Ishara 7 za Mapema za Ujauzito za Kuangazia

    Ishara 7 za Mapema za Ujauzito za Kuangazia

  • Vyakula 7 Bora Vya Kichefuchefu na Ugonjwa wa Asubuhi

    Vyakula 7 Bora Vya Kichefuchefu na Ugonjwa wa Asubuhi

  • Jinsi ya Kukabiliana na Ugonjwa wa Asubuhi Katika Mimba

    Jinsi ya Kukabiliana na Ugonjwa wa Asubuhi Katika Mimba

  • Ishara 7 za Mapema za Ujauzito za Kuangazia

    Ishara 7 za Mapema za Ujauzito za Kuangazia

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2022 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it