Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Maswali 7 Maarufu Kuhusu Ngono Katika Mimba

3 min read
Maswali 7 Maarufu Kuhusu Ngono Katika MimbaMaswali 7 Maarufu Kuhusu Ngono Katika Mimba

Baadhi ya maswali maarufu kuhusu ngono katika mimba ni iwapo mtoto na mama wataumia na kuhusu mitindo bora ya kufanya ngono katika mimba.

Mwanamke anapopata mimba kwa mara ya kwanza huwa na maswali mengi kuhusu mimba. Tuna angazia maswali maarufu kuhusu ngono katika mimba.

Maswali maarufu kuhusu ngono katika mimba

maswali maarufu kuhusu ngono katika mimba

  1. Je, kufanya mapenzi katika ujauzito ni salama?

Ikiwa mama ana mimba ya salama isiyokuwa na matatizo yoyote ya kiafya. Kufanya mapenzi ni salama na hakumuweki katika hatari zozote katika kipindi hiki. Ikiwa mwanamke atahisi uchungu usiopungua ama kuvuja damu baada ya kufanya tendo la ndoa, ni muhimu kuwasiliana na daktari wa afya ya kike anayemshughulikia.

2. Kufanya mapenzi kutamwumiza mtoto?

Kufanya ngono katika mimba hakuna athari hasi kwa mtoto. Kumbuka kuwa fetusi huwa imezingirwa na maji ya amniotic yanayomlinda kutokana na hatari zozote. Mtoto kwenye uterasi ako salama.

3. Ujauzito huathiri hamu ya tendo la ndoa katika mimba

Hamu ya kufanya tendo la ndoa katika mimba hubadilika katika kila muhula na huwa tofauti kwa wanawake wote. Huku wengine wakipata hamu iliyoongezeka ya kufanya tendo la ndoa, wengine hukosa hamu. Katika muhula wa kwanza, mama husumbuliwa sana na kichefuchefu na huenda akakosa hamu ya kufanya mapenzi. Kisha ikrejelea katika trimesta ya pili na kupungua katika trimesta ya tatu kufuatia kukosa starehe kunako fuatia ongezeko la tumbo na uzito wa mwili.

4. Mitindo bora ya kufanya ngono katika ujauzito ni ipi?

Katika ujauzito, mama hushauriwa kutumia mitindo inayompa starehe, bila kujishinikiza. Katika trimesta ya kwanza, mitindo kama missionary na cowgirl. Mtindo wa cowgirl ambapo mwanamke huwa juu humsaidia kudhibiti uzito wake na kiwango cha kupenya katika tendo la ndoa. Ni muhimu kwa wanandoa kujaribu mitindo tofauti hadi watakapopata inayowafaa zaidi.

maswali maarufu kuhusu ngono katika mimba

5. Ni wakati upi ngono sio salama katika ujauzito?

Kulingana na mimba ya mama, kuna wakati ambapo daktari anaweza kuwashauri wanandoa kutofanya mapenzi. Hizi ni baadhi ya sababu zinazoweza kuwafanya wanandoa kushauriwa wajitenge na tendo la ndoa katika mimba.

Ikiwa mama ana historia ya kujifungua kabla ya wakati, ana tatizo la placenta previa, kuvuja damu, ana mimba ya watoto mapacha ama zaidi ama ikiwa maji ya amniotic yana vuja.

6. Ngono inaweza kusababisha uchungu wa uzazi usikomaa

Kufanya ngono katika mimba hakuwezi sababisha uchungu wa uzazi usiokomaa. Isipokuwa pale ambapo daktari anatangaza mimba kuwa katika hatari ya uchungu wa uzazi usiokomaa.

7. Ni lazima kufanya ngono katika mimba?

Sio jambo la lazima, huenda mama akakosa hamu ama kuwa na ujauzito usio salama na kushauriwa na daktari kujitenga na tendo la wanandoa.

Kufanya tendo la ndoa hudumisha utangamano kati ya wanandoa. Kwa wanandoa wasioweza kufanya tendo hili katika mimba kufuatia matatizo tofauti, wanaweza kudumisha uhusiano wao kwa njia zingine za mapenzi kama kukumbatiana, kuwa pamoja kwa muda, kufanya kazi za kinyumbani pamoja ama kwa kumpa mchumba masi.

Chanzo: Healthline

Soma Pia: Dalili 11 Za Mimba Ya Mtoto Msichana Za Kuangazia

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Pregnancy
  • /
  • Maswali 7 Maarufu Kuhusu Ngono Katika Mimba
Share:
  • Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

    Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

  • Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

    Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

  • Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

    Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

  • Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

    Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

  • Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

    Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

  • Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

    Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it