Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Vitu 5 Vinavyo Sababisha Matatizo Katika Ndoa Na Jinsi Ya Kukumbana Nayo

3 min read
Vitu 5 Vinavyo Sababisha Matatizo Katika Ndoa Na Jinsi Ya Kukumbana NayoVitu 5 Vinavyo Sababisha Matatizo Katika Ndoa Na Jinsi Ya Kukumbana Nayo

Kubatilishwa kwa hisia, kutozungumza matakwa yako na kupuuza hisia za mchumba wako ni baadhi ya vyanzo vya matatizo katika ndoa.

Mazungumzo ni muhimu katika kila kitu. Ili ndoa iwe na ufanisi, ni muhimu kwa wanandoa kujifunza jinsi ya kuzungumza wanavyohisi. Kuzungumzia hisia zako na vile ambavyo ungependa kudhaminiwa sio jambo rahisi. Na hakuna anaye penda kurudia jambo moja kwa muda mrefu. Lakini, sio mambo makubwa yanayo anzisha matatizo, ni vitu vidogo vidogo vinavyo sababisha matatizo haya. Kuna sababu nyingi zinazo ibua matatizo katika ndoa. Lakini wanandoa wanapo zifahamu na kuzitatua, ndoa yao itakuwa sawa.

Kipi kinacho sababisha matatizo katika ndoa na unaweza kutatua kivipi?

matatizo katika ndoa

  1. Hisia kubatilishwa

Baada ya siku ndefu kazini, untarajiwa kuwa unapomwelezea mchumba wako kilichofanyika, atakusikiliza kisha kukuegemeza kihisia. Lakini unapomweleza kisha anyamaze ama akose kuhisi ulivyo tarajia, hisia zako zitaumizwa.

Hata kama sio jambo kubwa, hautahisi vyema mchumba wako anapopuuza hisia zako. Atahisi kana kwamba hapendwi. Huenda akafanya kitu sawa wakati ujao ili kuhakikisha kuwa mchumba wake anahisi alivyo hisi wakati ambapo hisia zake zilipuuzwa.

Kutatua: Msikilize mchumba wako, kisha umwambie kuwa unaelewa alichokipitia. Hata kama huenda ukakosa kukubaliana naye. Cha muhimu zaidi ni kuwasikiliza.

2. Kutosema unachotaka

Kutosema unachotaka kutakufanya uumie katika ndoa. Ni vigumu kwa mchumba wako kutojua hasa unachokitaka.

Kutatua: Unapo taka kitu, mweleze, anapofanya jambo lisilo kufurahisha, kuwa na mazungumzo ya kina naye. Mazungumzo haya wakati wote hayatakuwa ya kufurahisha, mbali huenda kukawa na hisia za chuki katika mazungumzo haya. Lakini mchumba wako ataelewa unachotaka na mwishowe mtakuwa na maisha bora.

3. Kuto tenga muda wa kuwa pamoja

Familia huwa na mambo mengi yanayochukua muda mwingi. Kulea watoto, kufanya majukumu ya kinyumbani baada ya siku ndefu kazini, na kudumisha uhusiano na mchumba wako. Katika wakati mmoja, wanandoa hufahamu kuwa hawana muda tosha wa kuwa pamoja.

Kutatua: Ni muhimu kwa wanandoa kutenga muda angalau mara moja kwa wiki, kuwa pamoja na kuzungumza kuhusu maisha yao mbali na watoto. Kufanya hivi kunasaidia kudumisha uhusiano uliokuwa kabla ya watoto.

matatizo katika ndoa

4. Sio mashindano

Wanandoa wanaoshindana katika kila kitu huwa vigumu kufurahishana kwani mmoja wakati wote anajaribu kuwa bora kuliko mwingine. Hakuna mshindi katika ndoa, na kufanya hivi husababisha kuvunjika kwa ndoa.

Kutatua: Ndoa yenye afya ni kufikiria kama timu moja na kufanya mambo yenu kama timu. Kumaanisha kuwa, unafanya juhudi kumhusisha mchumba wako katika uamuzi wako.

5. Mapenzi ya kifizikia kufifia

Mambo yanayo sababisha mazungumzo kufeli katika ndoa pia husababisha kuharibika kwa maisha ya kimapenzi ya wanandoa. Kukosa kufanya mapenzi huenda kukawafanya wanandoa wengine kutengana.

Kutatua: Msikilize mchumba wako na utimize mahitaji yake ya kifizikia, kiakili na kihisia. Tenga muda wa kuwa pamoja.

Chanzo: Healthline

Soma Pia: Dalili Za Mimba Ya Mwezi Mmoja Baada Ya Kufanya Tendo La Ndoa!

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Relationship & Sex
  • /
  • Vitu 5 Vinavyo Sababisha Matatizo Katika Ndoa Na Jinsi Ya Kukumbana Nayo
Share:
  • Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

    Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

  • Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

    Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

  • Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

    Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

  • Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

    Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

  • Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

    Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

  • Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

    Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it