Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Matatizo Katika Trimesta ya Tatu Utakayoshuhudia

2 min read
Matatizo Katika Trimesta ya Tatu UtakayoshuhudiaMatatizo Katika Trimesta ya Tatu Utakayoshuhudia

Matatizo katika trimesta ya tatu ambayo mama mjamzito hupitia ni kama kuhisi haja ya kuenda msalani kila mara na uvimbe kwenye miguu.

Safari ya ujauzito inakaribia kufika tamati. Lakini kabla ya kupatana na mtoto wako, kuna changamoto chache zinazokuwa katika muhula huu wa mwisho. Matatizo katika trimesta ya tatu utakayoshuhudia ni kama vile kukosa usingizi, kuenda msalani mara kwa mara na kuvimba.

Matatizo Maarufu Katika Trimesta ya Tatu

matatizo katika trimesta ya tatu

  1. Kuvimba

Katika wiki ya 30 ya ujauzito, miguu huanza kufura, hasa kufuatia uzito wa zaidi wa mtoto. Miguu na vifundo vya miguu huvimba kufuatia uzito mwingi unaoshinikiza upande wa chini wa mwili.

Njia za kukabiliana na tatizo hili ni:

  • Kuto simama kwa muda mrefu
  • Kufanya mazoezi
  • Kuwekelea miguu kwenye kiti unapokaa chini
  • Kuvalia viatu ambavyo havikufinyi

2. Kukosa usingizi

Tatizo la kukosa usingizi huwa maarufu katika trimesta ya tatu. Mabadiliko ya homoni mwilini hasa ongezeko la progesterone mwilini huchangia pakubwa katika suala hili. Kuhisi haja ya kwenda msalani mara kwa mara hata usiku huathiri mfumo wa kulala.

Jinsi ya kukabiliana na tatizo hili:

  • Lala kwa upande mmoja, wa kulia ama kushoto
  • Tumia mto kukuwezesha kupata starehe kidogo unapolala
  • Koga kabla ya kulala, tazama vidokezo zaidi hapa

matatizo katika trimesta ya tatu

3. Maumivu ya mgongo

Ongezeko la homoni ya progesterone katika mimba hutuliza misuli na viungo ili kustahimili mimba inayokua na kuboresha uwezo wa mwendo wa pelviki ili mtoto aweze kupita kwenye kanali ya kujifungua kwa urahisi zaidi.

Suluhu:

  • Koga kwa maji moto
  • Tumia pedi yenye joto kwenye mgongo kutuliza uchungu
  • Kufanyiwa masi mara kwa mara kutuliza uchungu na kusaidia kupumzika

4. Kushiba mbio

Katika trimesta ya tatu, huwa vigumu kula chakula kingi kama ilivyokuwa hapo awali. Kadri uterasi inavyozidi kukua, ndivyo inavyosukuma tumbo, na kufanya nafasi ya chakula kupunguka.

Kukabiliana na suala hili:

  • Kula chakula kidogo mara tano kwa siku
  • Kula chakula kisicho na kalori nyingi
  • Epuka kula chakula chenye pilipili nyingi
  • Ongeza maziwa ya bururu kwenye lishe yako

5. Kuhisi kizunguzungu

Kusimama kwa muda mrefu kutaleta hisia ya kizunguzungu.

Suluhu:

  • Simama kwa upole
  • Kuto simama kwa muda mrefu
  • Tembea mara kwa mara
  • Uchungu kwenye maziwa

matatizo katika trimesta ya tatu

6. Maumivu kwenye maziwa

Maumivu kwenye maziwa katika mimba husababishwa na homoni mwilini.

Suluhu:

  • Nunua sindiria zinazotosha kwani saizi imeongezeka

7. Kwenda haja ndogo mara kwa mara

Kuhisi haja ya kwenda msalani mara kwa mara ndiyo sehemu inayosumbua zaidi katika muhula wa tatu wa mimba. Kibofu kimefinywa na kwa hivyo kuibua haja ya kwenda msalani kila mara.

Hakuna mengi unayoweza kufanya kuhusu jambo hili.

Chanzo: Healthline

Soma Pia: Orodha ya Watu Mashuhuri Nchini Kenya Walio na Mimba

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Pregnancy
  • /
  • Matatizo Katika Trimesta ya Tatu Utakayoshuhudia
Share:
  • Je, Kulala Kwa Mgongo Katika Mimba Kuna Athari Hasi Kwa Mama na Mtoto?

    Je, Kulala Kwa Mgongo Katika Mimba Kuna Athari Hasi Kwa Mama na Mtoto?

  • Je, Anita Nderu Ana Mimba?

    Je, Anita Nderu Ana Mimba?

  • Vyakula 7 Bora Vya Kichefuchefu na Ugonjwa wa Asubuhi

    Vyakula 7 Bora Vya Kichefuchefu na Ugonjwa wa Asubuhi

  • Je, Kulala Kwa Mgongo Katika Mimba Kuna Athari Hasi Kwa Mama na Mtoto?

    Je, Kulala Kwa Mgongo Katika Mimba Kuna Athari Hasi Kwa Mama na Mtoto?

  • Je, Anita Nderu Ana Mimba?

    Je, Anita Nderu Ana Mimba?

  • Vyakula 7 Bora Vya Kichefuchefu na Ugonjwa wa Asubuhi

    Vyakula 7 Bora Vya Kichefuchefu na Ugonjwa wa Asubuhi

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2022 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it