Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Matatizo Mbalimbali Yanayo Kumba Ulezi

2 min read
Matatizo Mbalimbali Yanayo Kumba UleziMatatizo Mbalimbali Yanayo Kumba Ulezi

Kuwa mzazi kunahitaji nishati nyingi na pia kuna matatizo ya ulezi kama vile mzazi kutopata wakati tosha wa kupumzika.

Kila uchao watoto wanazidi kuzaliwa. Huonekana jambo la urahisi na kweli si ngumu ikizingatiwa huchukua muda wa masaa machache kujaliwa mtoto. Ila safari nyingine na iliyo ndefu huwa imeng’oa nanga. Nayo ni safari ya ulezi. Kuna matatizo ya ulezi ama safari huwa laini?

Matatizo Ya Ulezi

matatizo ya ulezi

Wazazi wanapopata habari kuwa ni wajawazito hujawa na furaha nyingi. Na mara tu wanaanza kujiami kwa maarifa kuhusu watoto. Jinsi ya kuwaosha, kuwatunza, chakula na pia mavazi. Maarifa juu ya chanjo na habari nyingine tofauti. Hili ni kwa kuwa kila mzazi hutaka kumpa mtoto wake maisha mazuri ila huwa kuna matatizo ya ulezi ata baada ya kujiami kwa  maarifa.

Haya matatizo ni kama vile:

  • Magonjwa

Wazazi wengi wanapotarajia mtoto huwa hawana fursa au mwanya wa kuzungumzia magonjwa. Hii ni ikibainika wazi kuwa kila mtoto anapoanza safari yake duniani atakubana na magonjwa. Hili huwa kwa vile bado mwili wake hauna kinga dhabiti. Lakini pindi wanavyokua huweza kukabiliana na magonjwa itakikanavyo.

matatizo ya ulezi

  • Changamoto Za Kifedha

Mtoto huja na mahitaji mengi ya kifedha. Wakati mwingine kama wazazi hupuuzilia wakidhani bado mtoto ni mdogo mpaka anapowasili na kuelewa ata kabla waanze shule bado mahitaji ni mengi. Kutokuwa na fedha za kutosha inafanya hii safari kuwa ngumu. Kutoka mavazi, mahitaji ya hospitali na mahitaji mengine kama tundua.

  • Muda Mfupi Wa Mapumziko

Wazazi wengi huwa wamezoea maisha yao kuwa na utaratibu fulani wakiwa na masaa ya kutosha ya kulala. Ila mtoto anapofika wengi bado huwa hawajajitayarisha kwa mabadiliko. Mtoto huhitaji masaa mengi na mzazi ambalo huchosha. Pia wakati watu wanafaa kulala mtoto anaweza kuwa ameeamka ambalo linamaanisha mzazi hawana wakati tosha wa kupumzika.

  • Ulemavu

Kuna watoto ambao huzaliwa wakiwa na ulemavu wa aina fulani. Wazazi wengi katu hawatapanga kuwa na huu uwezekano ilihali hutokea kila mara. Huku kutokuwa na nafasi ya hili kutokea huwapa wazazi changamoto. Hii ni kwa kuwa huyu mtoto atahitaji mambo ya kitofauti ikilinganishwa na mtoto aliye mzima. Hili litakuwa changamoto kwa wazazi wowote wale.

Kila ujio wa mtoto unamaanisha mabadiliko kwa maisha ya mama ama mzazi yote. Kila kitu katika maisha ya familia hubadilika kwa kuwasili kwa mtoto. Kazi na majukumu mengine hufiki kikomo kwanza kumpa nafasi yule mdogo. Kujiandaa vilivyo kwa kumpokea mtoto kutaweza kukusaidia kukabiliana na matatizo ya ulezi ambayo yanaweza kuchipuka wakati wowote.

Chanzo: Healthline 

Soma Pia:Wazazi Kuchoka Katika Ulezi, Ishara Na Vyanzo Vyake

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Parenting
  • /
  • Matatizo Mbalimbali Yanayo Kumba Ulezi
Share:
  • Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

    Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

  • Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

    Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

  • Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

    Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

  • Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

    Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

  • Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

    Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

  • Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

    Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it