Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Je. Kuna Uwezekano Wa Mayai Kupevuka Mapema Katika Mimba?

3 min read
Je. Kuna Uwezekano Wa Mayai Kupevuka Mapema Katika Mimba?Je. Kuna Uwezekano Wa Mayai Kupevuka Mapema Katika Mimba?

Kupevuka kwa mayai ni jambo ambalo hutokea bila usaidizi wa kibinadamu. Ila ni wazi kuwa, iwapo mayai yanaweza pevuka mapema katika mimba ni la.

Kupevuka  ni pale yai moja ama zaidi huachiliwa kutoka kwa ovari ya mwanamke. Kila mwezi kati ya mayai 15 hadi 20 huwa yanakua kwenye mfuko wa mayai wa mwanamke.Hili yai linaporutubishwa mama hushika mimba. Lakini je, mayai yanaweza pevuka mapema katika mimba?

Mayai Yanaweza Pevuka Mapema Katika Mimba?

mayai yanaweza pevuka mapema katika mimba

Wakati wa kupevuka, yai lililokomaa zaidi hutolewa na kusukumwa kwenye mirija ya fallopia. Hii mirija huunganisha mfuko wa mayai na uterasi. Mifuko ya mayai haipokezani kutoa yai lililokomaa kila mwezi. Hali hii hutokea bila mpangilio wowote.  Yai lillilorutubishwa husafiri kwenye mirija ya uzazi kisha kwenye uterasi.

Kama yai limerutubishwa na mbegu linapandikizwa ndani ya ukuta wa uterasi. Huu huwa mwanzo wa ujauzito. Kama yai halijarutubishwa, ukuta uliorutubishwa ndani ya uterasi hutolewa nje ya mwili wakati wa hedhi. Iwapo utakuwa mjamzito, mwili hujua hivi. Hivyo maandalizi yote ambayo hutokea ndani ya mwili kabla ya kupevushwa kwa yai husitishwa.

Uterasi, mirija ya fallopia na ovari huwa kwenye muundo mmoja. Vile vile homoni ambazo huchangia kwa maandalizi hayo. Hivyo basi iwapo kuna kiumbe kinacho umbika kwenye uterasi, mambo mengine hufikia kikomo. Hili huwa ili kukipa kiumbe kinachokua msaada unaohitajika. Hivyo ni vigumu mayai yanaweza pevuka mapema katika mimba.

Nini Husababisha Kupevuka

mayai yanaweza pevuka mapema katika mimba

Homoni ya LH (luteinizing hormone) inayotolewa na tezi ya pituitari huongezeka ndani ya mwili wa mwanamke anapokaribia ovulation. Homoni ya FSH (follicle stimulating hormone) inahushika katika  kuhakikisha kuwa yai linakomaa haraka na kutolewa na ovari. Homoni ya LH husaidia kuongezeka kwa estrogeni. Hii pia husaidia kujenga kiwambo laini ndani ya ukuta wa uterasi.

Hiki kiwambo huongezeka kwa unene uliojaa damu na virutubisho kama maandalizi ya upandikaji wa yai.Utaratibu huu hufanyika kila mwezi mpaka pale yai litakapo pandikizwa au hedhi kutokea. Viwango vya estrogeni huendelea kuongezeka mpaka kufikia hatua ya kuhamasisha homoni ya LH  inayosukuma utoaji wa yai kutoka kwa ovari.

Hutokea Wakati Gani

Kwa kawaida hutokea kati ya siku 11 na 21 baada ya siku ya kwanza ya hedhi  yako ya mwisho. Kwa mfano, tuseme una mzunguko wa hedhi wa siku 28, hesabu siku ya kwanza  ya kuona hedhi yako kama siku ya kwanza. Kila mwanamke ni tofauti na vile vile kila mzunguko wa hedhi  unaweza kuwa tofauti. Hata hivyo, makadirio yaliyofikiwa ni kwamba kupevuka hutokea katikati ya mzunguko wako wa hedhi.

Kupevuka  Hudumu Wakati Gani

Fertile window ni kipindi katika mzunguko wa hedhi wa mwanamke. Hiki kipindi mwanamke anaweza kupata ujauzito. Kipindi hiki hudumu siku tano au sita kila mwezi. Yai lako haliwezi kuwa hai baada ya masaa 24 baada ya kupevushwa. Kwa hivyo kukutana kwa yai lazima kufanyike katika hicho kipindi. Mbegu za kiume huweza kukaa hadi siku saba.

Nitajuaje mayai yanapevuka  ndani ya mwili wangu:

  • Mabadiliko ya uteute kwenye mlango wa uzazi
  • Maumivu ya tumbo la chini
  • Mabadiliko ya hisia za mapenzi
  • Matiti kujaa na chuchu kuuma
  • Matone ya damu katika nguo za ndani
  • Mabadaliko ya joto la mwili
  • Mabadilikoya hisia

Kupevuka kwa mayai ni jambo ambalo hutokea bila usaidizi wa kibinadamu. Ila ni wazi kuwa, iwapo mayai yanaweza pevuka mapema katika mimba ni la.

Chanzo: Healthline

Soma Pia: Jinsi Ambavyo Mwanamke Anaweza Kufahamu Mimba Yake Ina Wiki Ngapi!

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Becoming a Mama
  • /
  • Je. Kuna Uwezekano Wa Mayai Kupevuka Mapema Katika Mimba?
Share:
  • Vidokezo 5 vya Kupata Mimba kwa Wanandoa Wanaolenga Kuwa Wazazi

    Vidokezo 5 vya Kupata Mimba kwa Wanandoa Wanaolenga Kuwa Wazazi

  • Njia 5 za Kujitayarisha kwa Uchungu wa Mama

    Njia 5 za Kujitayarisha kwa Uchungu wa Mama

  • Vitu Vya Kufanya Kabla ya Kuenda Hospitali Kujifungua

    Vitu Vya Kufanya Kabla ya Kuenda Hospitali Kujifungua

  • Vidokezo 5 vya Kupata Mimba kwa Wanandoa Wanaolenga Kuwa Wazazi

    Vidokezo 5 vya Kupata Mimba kwa Wanandoa Wanaolenga Kuwa Wazazi

  • Njia 5 za Kujitayarisha kwa Uchungu wa Mama

    Njia 5 za Kujitayarisha kwa Uchungu wa Mama

  • Vitu Vya Kufanya Kabla ya Kuenda Hospitali Kujifungua

    Vitu Vya Kufanya Kabla ya Kuenda Hospitali Kujifungua

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it