Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Umuhimu Wa Kuwafunza Watoto Wa Kiume Kuhusu Hedhi

3 min read
Umuhimu Wa Kuwafunza Watoto Wa Kiume Kuhusu HedhiUmuhimu Wa Kuwafunza Watoto Wa Kiume Kuhusu Hedhi

Mazungumzo kuhusu hedhi na vijana ni muhimu, ili wawe na maarifa kuhusu kinachofanyika katika mwili wa mwanamke na wawe watu wenye huruma na utu.

Siku moja niliingia kwenye nyumba kisha nikawapata vijana wangu wakikimbizana. Mwanangu wa miaka saba alikuwa yu-wamkimbiza ndugu yake mdogo na pedi yangu huku akimwambia, "Nitakuweka pedi hii ya mama kwenye kichwa chako!"

Ndugu yake mdogo alikimbia kwa kasi kwa hofu kuwa pedi hii kamwe haingetoka milele.

Yametosha! Nikadhani, sio kukimbizana kwao, kwani hilo kamwe halitawahi koma nyumbani mwangu na katika familia zote zenye watoto wa kiume. Nilichotaka ni kukomesha, na kuwa na mazungumzo kuhusu hedhi na vijana wangu.

Huenda ikawa watoto wangu walikuwa wakiwaambia kuwa mama yao anavalia diapers. Hawakuwa na maarifa yoyote kuhusu jinsi mwili wa mwanamke ulivyofanya kazi. Nikafanya uamuzi wa kuanza na kifungua mimba changu.

Mazungumzo kuhusu hedhi na vijana

mazungumzo kuhusu hedhi na vijana

Hatua ya kwanza: Hakuna drama

Katika miaka saba, kijana wangu ako katika umri ambapo nikisema kitu kwa njia isiyo faa, atafanya hivyo pia. Kwa hivyo niliamua kuzungumza kuhusu hedhi kwa njia iliyo na ukweli. Tulipo enda kufanya ununuzi wa vitu vya kinyumbani, nilimwuliza anichukulie pedi. Tulipofika nyumbani na kuanza kuvitoanisha vitu, nikaanza mada:

Mimi: Unafahamu kuwa hizi sio diaper, kweli?

Yeye: Ni nini?

Hatua ya pili: Kuwa mkweli

Mtoto wangu anapenda wanyama, kwa hivyo nilifanya uamuzi wa kuelezea kuhusu hedhi kwa kutumia kitu anachokifahamu. Anapenda chui kwa sasa hivi. Kwa hivyo nikamweleza kuwa chui wa kike anapotaka kuwa na mtoto, nafasi kwenye tumbo yake ambapo mtoto hukua, hujitayarisha na kukua ukuta laini ndani, ili mtoto wa chui awe na starehe.

Baadhi ya wakati, hakuna mtoto chui, na wakati mwingine, yupo... na ni sawa na binadamu.

mazungumzo kuhusu hedhi na vijana

Hatua ya tatu: Usianze hadithi zingine

Sikutaka kuingia katika mazungumzo ya tendo la wanandoa kwa sababu mtoto yangu bado hakuwa ameniuliza maswali. Kwa hivyo sikuhusisha mazungumzo ya hedhi na tendo la ndoa.

Nilipogeuza mazungumzo kuwa kuhusu binadamu, nilimwambia kuwa iwapo mtoto hakui kwenye tumbo la mama, ukuta wenye starehe unadondoka. Kisha nikamweleza kuwa ukuta huu, hukua kila mwezi iwapo hakuna mtoto, kisha kutoka mwilini mwa mama kama damu. Na hii ndiyo sababu kwanini nilihitaji pedi.

Na kumweleza kuwa jambo hili hunifanyikia poa.

Hatua ya nne: Kipindi cha ukweli

Kwa sababu kijana wangu huhusisha damu sana na uchungu, kitu cha kwanza alichoniuliza ni iwapo hedhi huwa na uchungu. Nikamweleza kuwa la.

Kwa bahati nzuri, hakuniuliza jinsi mtoto anavyotengenezwa, lakini nashuku kuwa swahili hilo litafuata hivi karibuni.

Ni vyema wazazi kutotengeneza mlima kuhusu vitu ambavyo ni vya kawaida. Kuwa mkweli kwa mtoto wako na ujibu maswali yake bila fiche, kwa kutumia lugha anayo elewa kulingana na umri wake.

Soma Pia: Utafiti Unasema Kuwa Familia Zenye Watoto Wawili Huwa Na Furaha Zaidi

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Parenting
  • /
  • Umuhimu Wa Kuwafunza Watoto Wa Kiume Kuhusu Hedhi
Share:
  • Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

    Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

  • Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

    Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

  • Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

    Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

  • Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

    Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

  • Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

    Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

  • Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

    Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it