Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Mazungumzo Muhimu Kuhusu Fedha ya Kuangazia na Mwenzio Kabla ya Kufunga Ndoa

3 min read
Mazungumzo Muhimu Kuhusu Fedha ya Kuangazia na Mwenzio Kabla ya Kufunga NdoaMazungumzo Muhimu Kuhusu Fedha ya Kuangazia na Mwenzio Kabla ya Kufunga Ndoa

Kuangazia mazungumzo muhimu kuhusu fedha kabla ya ndoa kunawasaidia wanandoa kufahamu majukumu ya kila mmoja.

Mazungumzo kuhusu fedha sio baadhi ya mazungumzo yenye starehe zaidi. Hasa na mtu unayependa, huenda ukawa na shaka nyingi na kujiuliza iwapo yataadhiri uhusiano wenu. Hata hivyo, ni muhimu kuzungumzia fedha kabla ya kuingia katika ndoa. Tazama baadhi ya mazungumzo muhimu kuhusu fedha unayopaswa kuangazia na mwenzio kabla ya kufunga ndoa.

Mazungumzo Muhimu Kuhusu Fedha Unayopaswa Kuangazia na Mwenzio Kabla ya Kufunga Ndoa

mazungumzo muhimu kuhusu fedha kabla ya ndoa

  1. Je, tuna utangamano wa kifedha

Ndoa huja baada ya kuwa katika uchumba na mpenzi wako kwa muda. Katika kipindi hiki, unaweza kuangalia tabia zake za kifedha na kufahamu uhusiano alio nao na pesa. Huenda kuna vitu anavyofanya na pesa zake na hata baada ya kuangalia mienendo yake, lazima uulize maswali ili kujua zaidi. Swali la utangamano wa kifedha linakusaidia kujua mambo anayoyapatia kipau mbele na iwapo yanaendana na unayoyathamini pesa zinapohusika.

Je, mchumba wako anaamini kuhifadhi kiwango fulani cha pesa kwanza kabla ya kutumia pesa zinazobaki ama anatumia pesa kisha kuhifadhi zinazobaki?

2. Je, una deni?

Baadhi ya watu wengi waliosomea vyuo vikuu nchini Kenya wana madeni ya wanafunzi. Hizi ni fedha ambazo kila mwanafunzi aliyefuzu na kwenda katika chuo kikuu hupatiwa kumsaidia kulipa karo ya shule na kupata kiwango kidogo cha pesa za mfukoni. Baada ya kuhitimu, kila mwanafunzi anatarajiwa kuanza kulipa deni lake. Kufahamu deni za mpenzi wako kabla ya kufunga ndoa kutawawezesha kupanga fedha zenu kwa njia inayowawezesha kukamilisha deni hizi kwanza.

Je, deni zake ni kufuatia deni la wanafunzi, ununuzi wa mali ama kununua vitu vinavyopunguka dhamani.

3. Majukumu ya kifedha

Je, kuna wanafamilia wanaokutegemea kulipa bili zao kila mwezi. Huenda ikawa ni karo ya ndugu, wazazi kutarajia kutumiwa pesa za matumizi ama kulipiwa kodi na kadhalika. Kufahamu majukumu ya kifedha ya mpenzi wako yatawasaidia kujua mtakavyo panga fedha zenu na iwapo baadhi ya majukumu hayo ni muhimu ama yanaweza kupunguzwa.

mazungumzo muhimu kuhusu fedha kabla ya ndoa

4. Kugawanya bili za nyumba

Mazungumzo muhimu kabla ya kufunga ndoa. Yanakuwezesha kujua iwapo mna malengo tofauti. Kuingia katika ndoa na majukumu dhabiti kunasaidia kuepuka matatizo ya siku za usoni kuhusu fedha. Kufahamu mchumba atakaye lipa kodi, karo ya shule, vyakula  na kadhalika kunasaidia kuhakikisha mna utangamano wa kifedha.

5. Je, tutakuwa na akaunti moja ya fedha ama tofauti

Kuwa na uhusiano wa ndani kuna maanisha kuwa na mazungumzo magumu hasa ya kifedha. Je, mtakuwa mnahifadhi pesa zenu kwenye akaunti moja ama kila mtu atakuwa naye. Kufahamu jambo hili kutawasaidia kufahamu mtakavyojipanga mnapokuwa na fikira za kuwekeza katika sekta fulani.

Soma Pia: Ushauri Wa Kindoa Ulio Muhimu Kwa Wanandoa Wote

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Lifestyle
  • /
  • Mazungumzo Muhimu Kuhusu Fedha ya Kuangazia na Mwenzio Kabla ya Kufunga Ndoa
Share:
  • Sababu 7 Kwa Nini Watu Wanaogopa Ndoa Siku Hizi

    Sababu 7 Kwa Nini Watu Wanaogopa Ndoa Siku Hizi

  • Zari Hassan Amewasili Nchini Kenya Ambapo Anavumbua Nyumba Mpya

    Zari Hassan Amewasili Nchini Kenya Ambapo Anavumbua Nyumba Mpya

  • Lori Harvey na Michael B. Jordan Wametengana Baada ya Kuwa Pamoja Kwa Mwaka Mmoja

    Lori Harvey na Michael B. Jordan Wametengana Baada ya Kuwa Pamoja Kwa Mwaka Mmoja

  • Sababu 7 Kwa Nini Watu Wanaogopa Ndoa Siku Hizi

    Sababu 7 Kwa Nini Watu Wanaogopa Ndoa Siku Hizi

  • Zari Hassan Amewasili Nchini Kenya Ambapo Anavumbua Nyumba Mpya

    Zari Hassan Amewasili Nchini Kenya Ambapo Anavumbua Nyumba Mpya

  • Lori Harvey na Michael B. Jordan Wametengana Baada ya Kuwa Pamoja Kwa Mwaka Mmoja

    Lori Harvey na Michael B. Jordan Wametengana Baada ya Kuwa Pamoja Kwa Mwaka Mmoja

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2022 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it