Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Sababu Kwa Nini Mchumba Wako Atatoka Nje Ya Ndoa Yenu

3 min read
Sababu Kwa Nini Mchumba Wako Atatoka Nje Ya Ndoa YenuSababu Kwa Nini Mchumba Wako Atatoka Nje Ya Ndoa Yenu

Huenda kukawa kuna matendo uyafanyayo yanayo mfanya mchumba wako kutoka nje ya ndoa? Epuka kufanya haya katika ndoa ama uhusiano wako!

Kutoka nje ni lawama yako ama kuna baadhi ya vitu unavyo vifanya vinavyo msukuma mchumba wako kuwa na umbali nawe. Kuna baadhi ya vitendo vinavyo mfanya mchumba wako kutoka nje ya ndoa ama uhusiano wenu.

Sababu Za Mchumba Wako Kutoka Nje Ya Ndoa Yenu

kutoka nje katika ndoa

  1. Kuto jitunza

Jambo hili hushuhudiwa sana kwa wanawake walio jifungua ama baada ya kuwa na mchumba wako kwa muda mrefu. Unapata kuwa hauko makini na unavyo kaa, haujitunzi wala kuhakikisha kuwa bado unapendeza. Kuna baadhi ya wanaume ambao pia hufanya hivi. Baada ya kuwa na wachumba wao, wana sahau kutunza miili yao. Jambo linalo wakera wachumba wao. Kwa kufanya hivi, unamfanya mchumba wako apoteze hamu ya kuwa nawe.

2. Kuto mpa mchumba wako wakati

Ikiwa moja wenu hana wakati wa kuwa na mwingine, huenda ikamaanisha kuwa ana kitu ama mtu mwingine anaye chukua muda wake, na hiyo ndiyo sababu kwa nini wakati wake kwako umepungua.

3. Kucheza mchezo wa lawama

wanawake kutoka nje ya ndoa

Jambo linapo enda mrama, unamlaumu mchumba wako badala ya kukubali kosa lako. Inafika wakati ambapo kila kitu kinacho enda vibaya kinakuwa ni lawama ya mchumba wako. Ikiwa una zingatia makosa yake, hakuna wakati ambapo uta ona kitu chochote chanya wanacho fanya. Kufanya hivi kutamfanya mchumba wako aende atafute mtu ambaye anahisi ana furahia na kuona juhudi anazo tia kwenye uhusiano.

4. Hauna wakati wa kufanya ngono

Hii huwa sababu kuu ya baadhi ya watu kutoka nje ya ndoa ama uhusiano wao na kuwa na mchumba wa kando. Kufanya mapenzi ni muhimu sana kwa watu walio katika ndoa. Hakikisha pia unatia juhudi kwa ngono sio kana kwamba ni jukumu, huu ni wakati wenu wa kufurahia na kukaribiana zaidi. Uhusiano huu unapo isha katika ndoa, unapata kuwa mambo mengi yame badilika.

5. Haumpi sikio mwenzi wako

Uhusiano huwa kati ya marafiki, hata baada ya kufunga ndoa, mnapaswa kuzidi kuwa marafiki, tena wa dhati. Kwa njia hii, mpenzi wako anapata imani ya kukueleza kinacho endelea maishani mwake na kinacho msumbua. Usimpo msikiza, huenda akaona haja ya kutafuta mtu mwingine wa kumweleza kinacho mtatiza.

Ili mapenzi yafanikiwe, wanandoa wote wanapaswa kutia juhudi kuhakikisha kuwa wanafanya yote wawezayo ili mapenzi yao yasiishe. Mpe mchumba wako wakati na umsikilize anapo taka rafiki wa kumweleza kinacho endelea. Kwa wakati wowote ule, kamwe kutoka nje katika ndoa ama uhusiano hakukubalishwi. Ikiwa mpenzi wako ana kukosea, chukua muda na umweleze anacho fanya kisicho kufurahisha na mtatue matatizo yenu.

Soma Pia: Njia Tofauti Za Kuboresha Uhusiano Wako Na Watu Unao Penda

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Relationship & Sex
  • /
  • Sababu Kwa Nini Mchumba Wako Atatoka Nje Ya Ndoa Yenu
Share:
  • Sababu 3 Kwa Nini Wanawake Hutoka Nje Ya Ndoa Kulingana Na Wataalum

    Sababu 3 Kwa Nini Wanawake Hutoka Nje Ya Ndoa Kulingana Na Wataalum

  • Uraibu Wa Kutoka Nje ya Ndoa Nchini Kenya

    Uraibu Wa Kutoka Nje ya Ndoa Nchini Kenya

  • Watu 7 Mashuhuri Walio Zifufua Ndoa Zao Baada Ya Visa Vya Kutoka Nje Ya Ndoa

    Watu 7 Mashuhuri Walio Zifufua Ndoa Zao Baada Ya Visa Vya Kutoka Nje Ya Ndoa

  • Njia 3 Ambavyo Uhusiano Unaathiriwa Baada Ya Mchumba Kutoka Nje

    Njia 3 Ambavyo Uhusiano Unaathiriwa Baada Ya Mchumba Kutoka Nje

  • Sababu 3 Kwa Nini Wanawake Hutoka Nje Ya Ndoa Kulingana Na Wataalum

    Sababu 3 Kwa Nini Wanawake Hutoka Nje Ya Ndoa Kulingana Na Wataalum

  • Uraibu Wa Kutoka Nje ya Ndoa Nchini Kenya

    Uraibu Wa Kutoka Nje ya Ndoa Nchini Kenya

  • Watu 7 Mashuhuri Walio Zifufua Ndoa Zao Baada Ya Visa Vya Kutoka Nje Ya Ndoa

    Watu 7 Mashuhuri Walio Zifufua Ndoa Zao Baada Ya Visa Vya Kutoka Nje Ya Ndoa

  • Njia 3 Ambavyo Uhusiano Unaathiriwa Baada Ya Mchumba Kutoka Nje

    Njia 3 Ambavyo Uhusiano Unaathiriwa Baada Ya Mchumba Kutoka Nje

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it