Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Mimba Huweza Kutambulika Baada Ya Muda Gani?

3 min read
Mimba Huweza Kutambulika Baada Ya Muda Gani?Mimba Huweza Kutambulika Baada Ya Muda Gani?

Ni rahisi sana kujua iwapo mtu ana ujauzito au la kwa kutumia vipimo ama kuzingatia dalili. Lakini wakati huwa ni jambo la msingi. Hivyo ni vyema kuelewa mimba inajulikana baada ya muda upi.

Mimba hutokea pale ambapo yai la mwanamke hutungishwa na mbegu ya mwanamume. Hili hujipandikiza kwenye ukuta wa uterasi na hapa ujauzito hutokea. Mwanzoni ni vigumu kujua iwapo mtu ni mjamzito. Hivyo basi, mimba inajulikana baada ya muda upi?

Mimba Inajulikana Baada Ya Muda Upi?

mimba inajulikana baada ya muda upi

Vipimo vya ujauzito vinaweza kutoa majibu ikiwa una ujauzito au la. Hii huwa baada ya siku ya kwanza ya Kukosa siku zako za hedhi. Hata hivyo, kuna vipimo vinavyoweza kutoa majibu ya kuwepo kwa mimba hata siku nne au tano kabla ya kuanza siku zako.

Kama una mzunguko ambao ni sawa ni rahisi kwako kujua ni lini utaanza kuona siku zako. Kama mzunguko wako haueleweki, inashauriwa usubiri wiki mbili hadi tatu. Mara nyingi ukipima na kupata majibu ya ndiyo hilo huwa jibu sahihi zaidi.

Hii ni ikilinganishwa na kupata majibu ya hauna mimba. Kwa hivyo kuna uwezekano kipimo kusema huna mimba lakini kumbe tayari unayo. Ikiwa unahisi kuwa wewe ni mjamzito lakini kipimo kina sema la, inashauriwa kufanya kipimo kingine baada ya siku saba ama wiki moja.

Lini Haswa Nilipata Ujauzito?

Vipimo vya ujauzito huangalia kuwepo kwa homoni ya mimba ijulikanayo kama Human chorionic gonadotrophin (hcg) kwenye mkojo au damu.  Mwili wako huanza kuizalisha mara tu ukiwa mjamzito. Ikiwa utafanya kipimo siku moja baada ya Kukosa siku zako za hedhi, ukapata  majibu ya kuwa ni mjamzito kuna uwezekano ukawa tayari na ujauzito wa wiki mbili hivi.

Vipimo vikubwa zaidi vya ujauzito vinaweza kutoa majibu ya uhakika  ikiwa ni mjamzito kuanzia siku ya nane tangu mimba ilipotungwa. Baadhi ya vipimo vinaweza kukupa makadirio  juu ya lini haswa unaweza kuwa ndiyo  ulipata ujauzito. Mimba huanza kuhesabiwa tangu siku ya kwanza ilipotungwa.

Dalili Za Mimba Changa

mimba inajulikana baada ya muda upi

Dalili zinazoweza kuashiria ujauzito zinazoripotiwa sana na wanawake mwanzoni mwa ujauzito.

  • Kukosa kipindi cha hedhi

Kwa mara nyingi hii huwa ndiyo dalili ya kwanza wanawake hutambua nayo kuwa ni wajawazito. Ikiwa mwanamke atasema kuwa amekosa kipindi cha hedhi, hii ni ishara nzuri ya ushikaji wa mimba.  Na hii sana sana ni kwa wanawake walio na mzunguko wa hedhi wa kawaida.

  • Mabadiliko ya matiti

Wanawake wajawazito  huhisi matiti kuwa laini, yaliyojaa, yanayonywea, utanukaji na areola kuwa nyeusi. Mwanzoni mwa ujauzito, tezi za areola hutanuka kutokana na uchochelezi wa homoni. Na ukubwa  wa matiti huongezeka polepole kujitayarisha kutengeneza maziwa ya mtoto. Lakini kumbuka kuwa ukubwa wa matiti mara nyingi huongezeka muda tu kabla ya kipindi cha hedhi cha kila mwezi.

  • Kichefuchefu na kutapika

Hii dalili hutokea kwa kina mama wengi sana katika miezi tatu ya kwanza. Huwa kali zaidi asubuhi ndio maana kuitwa maradhi ya asubuhi. Lakini inaweza kutokea wakati wowote na huweza kuchochewa na harufu za upishi na viungo vya upishi.

  • Uchovu

Mwanzoni mwa ujauzito wanawake hujihisi wachovu na wenye usingizi wakati wa mchana. Pia hutaka kupumzika mara kwa mara kuliko kawaida wanapofanya kazi zao.

Ni rahisi sana kujua iwapo mtu ana ujauzito au la kwa kutumia vipimo ama kuzingatia dalili. Lakini wakati huwa ni jambo la msingi. Hivyo ni vyema kuelewa mimba inajulikana baada ya muda upi.

Chanzo: Healthline

Soma Pia: Mambo Muhimu Ya Kufanya Kwa Wanandoa Wanao Taka Kutunga Mimba!

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Pregnancy
  • /
  • Mimba Huweza Kutambulika Baada Ya Muda Gani?
Share:
  • Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

    Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

  • Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

    Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

  • Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

    Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

  • Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

    Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

  • Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

    Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

  • Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

    Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it