Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Vidokezo 7 Vya Kuwa na Mimba Salama na Yenye Afya

3 min read
Vidokezo 7 Vya Kuwa na Mimba Salama na Yenye AfyaVidokezo 7 Vya Kuwa na Mimba Salama na Yenye Afya

Ili kuhakikisha kuwa mama ana mimba salama na yenye afya, zingatia mitindo bora ya maisha, kula lishe bora na kujitenga na unywaji wa vileo.

Mwanamke mwenye mimba ama anayefikiria kupata mimba anafahamu  mambo ya kimsingi anayopaswa kujua kuhusu mimba. Kama kutovuta sigara ama kunywa pombe. Licha ya kutofanya kazi ngumu, tunaangazia vidokezo vya mimba salama na yenye afya.

Vidokezo vya Mimba Salama na Yenye Afya

1. Chukua vitamini za prenatal

mimba salama na yenye afya

Vitamini za prenatal ni muhimu katika kuhakikisha kuwa fetusi inakua kwa njia ipasavyo. Kuilinda dhidi ya kupata matatizo ya neural tube, ya kiakili ama uti wa mgongo. Mjamzito anapaswa kuanza kuchukua vitamini za prenatal miezi michache kabla ya kupata mimba, ama punde tu anapofahamu kuwa ana mimba. Vitamini za prenatal zina virutubisho muhimu kama kalisi, chuma na asidi ya folic.

2. Jifunze kuhusu ujauzito na kuwa mama

Kila ujauzito huwa wa kipekee. Haijalishi iwapo wewe ni mama wa mara ya pili ama ya tano, kuchukua darasa kuhusu kujifungua na kuwa mama ni muhimu. Kunakutayarisha kwa mchakato wa kujifungua na kuondoa hofu inayoandamana na mchakato huu. Kuwa na mkunga wa kujibu maswali ya kiujauzito kunakusaidia kufahamu jambo jipya kila mara.

3. Badilisha majukumu ya kikazi

Baadhi ya majukumu huwa hatari katika mimba. Kusafisha uchafu wa paka kunamweka mama mjamzito katika hatari ya kupata maradhi. Kazi zinazohusisha kugusa kemikali zinahatarisha maisha ya fetusi. Ikiwa kazi inahusisha kusimama kwa muda mrefu, huu ni wakati bora wa kubadilisha majukumu ya kikazi.

4. Fanya mazoezi

mimba salama na yenye afya

Kufanya mazoezi kuna manufaa mengi kwa mjamzito. Kuboresha mzunguko wa damu mwilini, kupunguza mawazo mengi, kupunguza uchungu mwilini, kusaidia kulala vyema zaidi usiku na kuboresha hisia za mama. Mama mjamzito anapaswa kufanya kazi kwa karibu na mtaalum wa mazoezi hasa kama mimba yake ni ya hatari. Kufanya mazoezi mepesi kwa dakika 30-45 kuna manufaa mengi kwa mama na mtoto.

5. Kuwa makini na vitu vyenye sumu

Vileo, pombe, sigara, dawa za kulevya huwa vyanzo vya matatizo ya kiafya katika mimba. Sigara hupunguza kiwango cha hewa kinachomfikia mtoto na kusababisha kujifungua kabla ya muda. Vileo vimehusishwa na kujifungua mtoto aliye na uzani wa chini ama matatizo ya kuchelewa katika ukuaji wake.

6. Kunya maji 

Mjamzito anahitajika kunywa maji zaidi katika kipindi hiki. Ili kuwezesha utendakazi mwilini wa kuzungusha virutubisho na hewa mwilini na kwa mtoto na kutoa uchafu kutoka kwa mtoto kwa mama na kuupitisha nje ya mwili. Maji yanakinga dhidi ya kuvimbiwa, kufura miguu ama maumivu ya mara kwa mara.

7. Kula samaki

mimba salama na yenye afya

Samaki ni chanzo bora cha omega-3, iliyo muhimu katika ukuaji wa ubongo. Kula samaki katika mimba kunasaidia na ukuaji wa ubongo wa mtoto. Hata hivyo, kuna aina ya samaki wenye zebaki nyingi, kama vile swordfish na mackerel. Kwa sababu hii, mama anashauriwa kuwasiliana na mtaalum wa afya kufahamu samaki bora. Wanaoshauriwa ni tuna, shrimps na salmon.

Ili kuhakikisha kuwa mama ana mimba salama na yenye afya, ni muhimu kuzingatia mitindo bora ya maisha. Lishe bora, kujitenga na unywaji wa vileo na kutofanya majukumu yanayohusisha kugusa kemikali.

Chanzo: WebMD

Soma Pia: Aina 3 za Anemia Katika Mimba na Jinsi ya Kuziepuka

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Pregnancy
  • /
  • Vidokezo 7 Vya Kuwa na Mimba Salama na Yenye Afya
Share:
  • Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

    Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

  • Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

    Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

  • Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

    Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

  • Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

    Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

  • Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

    Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

  • Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

    Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it