Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Unatarajia Nini Kwenye Mimba Ya Miezi Mitano?

3 min read
Unatarajia Nini Kwenye Mimba Ya Miezi Mitano?Unatarajia Nini Kwenye Mimba Ya Miezi Mitano?

Hii trimester ya pili haswa mimba ya miezi mitano hufahamika kama kipindi cha honeymoon katika mimba kwani ni wakati wako wa kujiburudisha.

Huu ndio utakuwa mwezi wako wa kutabasamu. Kichefuchefu na mabadiliko mengine ya mwili inayotokana na homoni za ujauzito yako nyuma yako. Unaweza kutulia na kufurahia ujauzito na mtoto unayetarajia. Ni mambo gani itanukuu  mimba ya miezi mitano?

Mimba Ya Miezi Mitano

mimba ya miezi mitano

Hivi sasa tumbo lako limeanza kuwa kubwa lakini si kubwa kukuzuia kufanya kazi zako. Katika hii trimester ya pili, unaweza tarajia kuongeza uzani. Watu wengi huwa hawaongezi uzani kwenye trimestrer ya kwanza sababu ya kichefuchefu.

Katika miezi mitano si tumbo lako tu ambalo linakua mbali pia hamu yako ya chakula. Pia nywele na kucha zako zimekua kwa haraka sana. Utaweza kutarajia:

  • kiungulia
  • maumivu ya miguu
  • kuvimba kwa miguu
  • kuvimbiwa
  • kizunguzungu
  • Kuumwa na kichwa
  • Maumivu ya mgongo
  • Mabadiliko ya ngovi kama vile chuchu kuwa nyeusi
  • Msongamano wa pua
  • Kubadilika kwa kitovu chako

Katika miezi mitano mtoto wako ana urefu wa inchi sita ama saba. Hii kumaanisha wanatoshana na ndizi. Wanakua ngozi ambayo hukinga mtoto kutokana na amniotic fluid inayomzingira mtoto. Pia wanajifunza kunyonya vidole, kugeuka, kupepesa macho na kuitikai sauti kutoka nje.

Pia unafaa kuwa unaanza kuskia mtoto akisonga ndani ya tumbo lako. Iwapo hujaskia chochote ni sawa kabisa. Mara nyingi kwenye ujauzito utaweza kuhisi huku kusonga kwa mtoto  kunakofahamika kama quickening kati ya wiki 16 hadi 20. Ila kila mtoto ni tofauti.

Saizi na vile mtoto alivyokaa kwenye plasenta inaweza kuwa sababu kuu kama utamskia mtoto wako akisonga au la. Ila kwa huu mwezi unafaa kuwa unahisi kusonga ata kwa umbali.

Mazoezi Na Lishe Katika Miezi Mitano

mimba ya miezi mitano

Iwapo mimba yako haina hatari ni vyema kudumisha ratiba ya mazoezi. Vile unavyofanya mazoezi kwa sasa ndivyo mwili wako utakuwa tayari kwa uchungu wa uzazi na pia kupona baada ya kujifungua. Lakini hili hubadilika kama mimba yako iko hatari. Hivyo ni vyema kupata ushauri wa daktari.

Mazoezi  yaliyo sawa na salama kuendelea nayo ni kama vile:

  • Kutembea ama kukimbia
  • Mazoezi ya yoga
  • Kuogelea
  • Kufanya hiking
  • Kujihusisha na darasa za densi
  • Mazoezi ya kujinyoosha na kuinua miguu

Kuzingatia lishe,  inashauriwa kula kalori 300 zaidi kwa kila siku katika trimester ya pili. Hii ni kuwa mtoto anahitaji chakula. Haishauriwa kupata hizi kalori kutoka kwa chakula kisicho na lishe bora. Lakini wakati mchache unaeza kula unachotaka ila hakikisha kuwa chakula chako kina:

  • Vyanzo vya protini kama vile kuku,samaki
  • Maziwa na bidhaa zake kama maziwa ya mgando
  • Nafaka zisizokobolewa
  • Matunda na mboga
  • Mafuta kama inayopatikana kwenye mbegu, karanga na parachichi

Unafaa Kumwona Daktari Lini?

Hivi sasa unafahamu vyema ni mambo gani hatarishi kwa ujauzito wako ama yanayohitaji uangalizi kwa makini.  Ila hii orodha itakukumbusha:

  • Kuvunja damu kutoka kwa uke
  • Uchungu mwingi na maumivu kwenye mgongo
  • Kuongezeka kwa joto la mwili
  • Uchungu unapoenda haja ndogo, inaweza kuwa ishara ya maambukizi.
  • Kutapika ambako ni zaidi ya kichefuchefu
  • Harufu kutoka kwenye mkojo ama ukeni.

Hii trimester ya pili haswa mimba ya miezi mitano hufahamika kama honeymoon kwani ni wakati wako wa kujiburudisha.  Fanya mazoezi, tarajia kusonga kwa mtoto wako na pia furahia picha ya kwanza ya ultrasound.

Chanzo: WebMD

Soma Pia: Jinsi Ya Kutumia Baking Soda Kudhibitisha Hali Ya Mimba

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Pregnancy
  • /
  • Unatarajia Nini Kwenye Mimba Ya Miezi Mitano?
Share:
  • Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

    Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

  • Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

    Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

  • Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

    Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

  • Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

    Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

  • Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

    Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

  • Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

    Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it