Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Mimba Ya Miezi Mitatu: Kinachofanyika Mwilini Na Mambo Ya Kutarajia

3 min read
Mimba Ya Miezi Mitatu: Kinachofanyika Mwilini Na Mambo Ya KutarajiaMimba Ya Miezi Mitatu: Kinachofanyika Mwilini Na Mambo Ya Kutarajia

Ishara za mimba ya miezi mitatu huwa tofauti kwa kila mwanamke kwani miili, urefu, uzito na nguvu za misuli huwa tofauti. Mwanamke anashauriwa kuwasiliana na daktari wake anapokuwa na suala lolote katika mimba.

Kwa mama ambaye hii ni mimba ya kwanza, huenda ikawa mimba yake haionyeshi akiwa na miezi mitatu. Wanawake wengi wenye misuli yenye nguvu huanza kuonyesha kuwa wana mimba katika mwezi wa nne ama tano. Kwa wanaoonyesha mapema pia ni sawa, kwani kila mwanamke huwa na mwili tofauti. Baada ya mimba ya kwanza, mwanamke huanza kuonyesha kuwa ana mimba mapema zaidi. Uzito, urefu na nguvu za misuli za mwanamke huathiri wakati ambapo mimba yake itaanza kuonekana.

Mimba Ya Miezi Mitatu

mimba ya miezi mitatu

Ukuaji wa fetusi ya miezi mitatu

Katika mwezi huu, fetusi iko kati ya urefu wa nchi 2 hadi 3 na uzito sawa na limau. Hata kama mama hahisi chochote, kuna mengi yanayofanyika tumboni. Haya yanafanyika mwilini mwa mtoto:

  • Mfumo wake wa misuli, kuchakata chakula, na mifupa unakua
  • Figo zinaanza kufanya kazi
  • Kucha za miguu na mikono zinaanza kumea
  • Sehemu za siri zinaanza kumea
  • Seli nyeupe zinaanza kutengenezwa mwilini

Mambo muhimu kufanya katika mwezi huu

  • Zungumza na daktari wako kuhusu kufanya mazoezi na mazoezi yanayokubalika katika mimba. Kuna baadhi ya mazoezi ambayo sio salama katika mimba na ni vyema kwa mama kujitenga nayo katika kipindi hiki.
  • Hakikisha unachukua vitamini za prenatal inavyofaa.
  • Zingatia ulaji wa vyakula vyenye umuhimu kwa mwili. Hakikisha kuwa kila lishe ina kiwango tosha cha protini, bidhaa za maziwa, wanga, mboga na matunda. Jitenge na ulaji wa vitamu tamu na vyakula vilivyo kaangwa kwa ufuta mwingi.
  • Kunywa maji tosha kwa siku. Maji katika mimba yanasaidia na uchakataji wa chakula na pia kusaidia kutengeneza amniotic fluid inayomlinda mtoto.

Wakati wa kumwona daktari

mimba ya miezi mitatu

Miezi ya hatari katika mimba huwa mwezi wa kwanza na wa pili, katika mwezi wa tatu, umetoka kwenye kipindi cha hatari cha mimba. Hata hivyo, ni vizuri kuwa na ufahamu wa ishara za hatari katika mwezi huu. Wasiliana na daktari wako unapogundua una zaidi ya ishara moja kati ya hizi.

  • Maumivu makali ya tumbo
  • Kuumwa vikali na mgongo
  • Joto jingi isiyopungua wala kuisha kwa kipindi kirefu
  • Ishara za maambukizi ya uke kama vile harufu kali kutoka sehemu ya uke
  • Kuumwa unapopitisha mkojo
  • Kutapika mara kwa mara. Na kufanya iwe vigumu kula bila kutapika

Safari ya ujauzito ya kila mwanamke huwa tofauti. Ishara za mimba ya miezi mitatu zitakuwa tofauti kwa kila mwanamke. Mwanamke hapaswi kulinganisha mimba yake na ya mwanamke mwingine. Kilicho muhimu zaidi ni kuwasiliana na daktari unapokuwa na shaka kuhusu chochote kile katika safari yako ya mimba.

Chanzo: WebMD 

Soma Pia: Kutunga Mimba Baada Ya Kutumia Mbinu Za Kudhibiti Uzalishaji

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Pregnancy
  • /
  • Mimba Ya Miezi Mitatu: Kinachofanyika Mwilini Na Mambo Ya Kutarajia
Share:
  • Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

    Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

  • Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

    Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

  • Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

    Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

  • Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

    Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

  • Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

    Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

  • Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

    Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it