Hivi sasa umemaliza trimesta ya kwanza na mabadiliko yaliyokuwamo kwenye kipindi hicho. Kwa kawaida umekaa vizuri katika nusu ya mwisho wa trimesta ya pili. Una nguvu zaidi na bado unaweza kutembea barabarani bila ya kuteleza. Mimba ya miezi sita hukaa vipi?
Cha Kutarajia Katika Mimba Ya Miezi Sita

Labda huna kichefuchefu tena ila unaweza kuwa mmoja wa wale wataendelea na kutapika kwa miezi tisa. Hilo si kumaanisha kuwa katika miezi sita huna dalili zozote:
- Wakati uterasi yako inayokua inaweka shinikizo kwenye matumbo yako. Hili hupunguza mwendo wa chakula
- Kujikunja hasa kwenye mgongo. Pia kwenye nyonga na kiuno. Hii ni kwa sababu ya uzito wa ziada unaobeba na jinsi unavyosambazwa mwilini
- Hii ni kwa kuwa mzunguko wako unakua ili kutoa mtiririko zaidi wa damu kwenye uterasi yako.
- Kuvimba na kubana kwenye miguu na vifundo vya miguu. Hili hutokana na mishipa yako kufanya kazi ya ziada ili kuhakikisha kila sehemu ya mwili wako inapata damu
- Njaa kubwa. Hii ni wazi kwa kuwa kuna kiumbe anayehitaji kukua
- Kiungulia na mmeng’enyo wa chakula, chuki kwa harufu maalum
Tumbo Lako Katika Mimba Ya Miezi Sita

Baada ya miezi sita ni wazi kuwa wewe ni mjamzito. Unaweza kutarajia mambo haya:
- Matiti yako yanaendelea kukua
- Tumbo lako limekuwa kubwa vya kutosha kuhitaji mabadiliko ya nguo za uzazi
- Kitufe chako cha tumbo kinaanza kugeuka nje
- Umeongeza uzito wa popote kutoka kilo 10 hadi 15 tangu trimester ya kwanza
Kina mama wote wajawazito huendeleza kwa njia na viwango tofauti. Tumbo lako linaweza kuonekana dogo kwa miezi sita ikiwa:
- Ni ujauzito wako wa kwanza
- Ulikuwa na nguvu ya msingi ya tumbo kabla ya ujauzito
- Uko juu ya wastani wa urefu
Hii ni kawaida kabisa, lakini usitie shaka tumbo lako litatokea nakuahidi. Idadi ya ujauzito ambao umekuwa nao pamoja na afya yako yote na uzito hucheza jukumu kubwa katika kuamua saizi ya tumbo lako.
Ukuaji Wa Fetasi Katika Miezi Sita Ya Mimba
Katika hatua hii, mdogo wako si mdogo tena. Wamekuwa pia wakifanya tani za hatua mbalimbali. Katika miezi sita, mtoto wako ameunda mapafu na seti ya kipekee ya alama za vidole, na wanaanza kuzingatia sauti zilizoko nje.
Kama huu ni ujauzito wako wa kwanza unaweza kuwa bado hujakubana au kumsikia mtoto akisonga tumboni lako. Lakini sasa hivi utaanza kukubana na mateke. Hufai kuanza kuhesabu mateke hadi week ya 28 lakini unafaa kuanza kuelewa ni wakati upi mtoto wako husonga.
Ni wakati gani bora wa kuona daktari?
- Iwapo unavunja damu
- Ishara kuwa maji yako imevunja
- Uchungu wa kupita kiasi kwenye mgongo na chini ya tumbo lako
- Kuhisi uchungu wakati wa kupitisha mkojo ama dalili zingine za ujauzito kama mkojo unaonuka
- Joto mwilini linaloendelea kwa siku nyingi
- Kutapika na kuendesha kwa mfululizo
- Kubana ambako hakuachi ama kupunguka ata baada ya mapumziko
- Kupunguka kwa mienendo ya mtoto wako
- Kuvunja damu kiasi ama kubadilika kwa dalili ulizokuwa nazo
Kufikia miezi sita ya mimba ni hatua kubwa kwa kila mama. Hii ni kwa vile umeweza kustahimili mabadiliko yanayoambatana na ujauzito toka mwezi wa kwanza.
Chanzo: WebMD
Soma Pia: Matatizo Ya Kiafya Mwanamke Anayo Kumbana Nayo Katika Mimba