Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Vyanzo 4 Vya Mjamzito Kuwa Na Tumbo Dogo

3 min read
Vyanzo 4 Vya Mjamzito Kuwa Na Tumbo DogoVyanzo 4 Vya Mjamzito Kuwa Na Tumbo Dogo

Sawa na watoto, mimba huja na shepu na saizi tofauti. Ikiwa mtoto anakua vyema katika kila hatua, sio chanzo cha wasiwasi. Lakini je, mjamzito kuwa na tumbo dogo husababishwa na nini?

Ni kawaida kwa mjamzito kuwa na tumbo dogo. Hakuna wakati haswa ambapo tumbo huanza kuonekana katika ujauzito. Kuwa na tumbo ndogo huenda kukamfanya mama ahisi kana kwamba hana mimba. Baadhi ya wanawake huingia kwenye muhula wa pili wa mimba na bado mimba haionekani. Jambo ambalo linaweza kumfanya mama apate wasiwasi. Kila mwili wenye mimba huwa tofauti, ni muhimu kwa mama kutokuwa na hofu. Iwapo anazingatia ushauri wa daktari wake na daktari kuhakikisha kuwa mtoto anakua ipasavyo, sio chanzo cha shaka.

Baadhi ya wanawake hutarajia mimba yao kuanza kuonekana kati ya mwezi wa tatu na wa nne. Kuna sababu ambazo huenda zikamfanya kuwa na mimba isiyo onekana sana.

Sababu za mjamzito kuwa na tumbo dogo

mjamzito kuwa na tumbo dogo

Mimba ya kwanza. Wanawake walio na mimba ya mara ya kwanza huenda wakachukua muda kabla ya ujauzito wao kuanza kuonekana. Kwa wanawake walio kuwa na mimba tena, itaanza kuonekana mapema kwani misuli yao imenyooshwa na mimba ya hapo awali.

Mama kuwa mrefu. Wanawake warefu huwa na mimba ndogo ikilinganishwa na wanawake wafupi, wajawazito warefu wana nafasi zaidi ya mtoto.

Mjamzito kuwa na misuli yenye nguvu. Mimba kwa wanawake walio na misuli yenye nguvu zaidi huchukua muda kabla ya kuanza kuonekana.

Uzito wa kupindukia. Kwa wanawake walio na uzito wa kupindukia, tumbo ya mimba huchukua muda zaidi kabla ya kuanza kuonekana.

Sawa na watoto, mimba huja na shepu na saizi tofauti. Ikiwa mama anakula, kunywa, kufanya mazoezi na kwenda kliniki inavyotakikana, na tumbo ingali dogo. Asiwe na shaka, ikiwa mtoto wake anakua vyema kulingana na kila hatua, sio chanzo cha shaka. Wanawake waliokuwa wamezoea kufanya mazoezi makali hapo awali pia huenda wakawa na tumbo dogo. Kwani misuli yao ina nguvu na kukaza mimba kuonekana mapema.

Wanawake wanaokuwa wamebeba watoto wadogo wana nafasi kubwa ya kuwa na mimba dogo. Sababu za kuwa na mtoto mdogo ni kama vile:

mjamzito kuwa na tumbo dogo

Mama kutumia vileo na sigara. Utumiaji wa vitu hivi una athari hasi kwa ukuaji wa fetusi na kuongeza nafasi za mama kuwa na mimba ya mtoto mdogo.

Matatizo ya placenta. Placenta huwa na jukumu kubwa kwa maisha ya mtoto. Placenta inapofeli kutimiza majukumu yake, mtoto hupoteza chakula na hewa kwenye uterasi na kuifanya iwe vigumu kwake kukua ipasavyo.

Matatizo ya fetusi. Ikiwa fetusi haina usawa wa geni ama ina maambukizi, haitakua ipasavyo na mama atakuwa na mimba dogo.

Ikiwa mjamzito kuwa na tumbo dogo kunamtia wasiwasi, ni vyema kufanyiwa ultrasound kuhakikisha kuwa mtoto anakua ipasavyo.

Chanzo: WebMD

Soma pia: Ukuaji Na Maendeleo Ya Fetusi: Mama, Tarajia Haya Katika Mimba Ya Miezi 6

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Pregnancy
  • /
  • Vyanzo 4 Vya Mjamzito Kuwa Na Tumbo Dogo
Share:
  • Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

    Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

  • Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

    Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

  • Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

    Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

  • Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

    Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

  • Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

    Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

  • Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

    Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it