Katika mwanzo wa muhula wa pili wa ujauzito, mwanamke huenda akaanza kuhisi mtoto akicheza tumboni, kubingirika, na kurusha mateke. Lakini je, mtoto hulia tumboni? Hata kama wanawake wengi wajawazito hawahisi mwendo huu, utafiti una pendekeza kuwa mtoto huanza kulia tumboni muda kabla ya kuzaliwa. Kana kwamba anajitayarisha kwa hatua kubwa ya kuzaliwa.
Mtoto hulia tumbo? Sayansi ina haya ya kusema

Uzinduzi na ukuaji wa teknolojia za kisasa katika nyanja ya afya unatuwezesha kuweza kuangalia kinachoendelea kwenye uterasi na jinsi ambavyo fetusi inakua. Katika baadhi ya video na picha za uterasi, uso wa mtoto anayelia umeonekana. Baada ya watafiti kutumia sauti ya juu kuona jinsi ambavyo fetusi itakavyofanya. Mama anapokuwa kwenye mazingira yenye kelele nyingi, fetusi hutoa sauti kubwa inayodhihirisha kukosa starehe.
Utafiti zaidi uliofanyika na timu ya Reissland, iliyoangalia kwa umakini mwendo wa fetusi katika muhula wa pili na wa tatu kupitia kwa vipimo vya ultrasound kuona usemi wa usoni. Wa kulia na kucheka kudhihirisha kuwa usemi wa usoni unaonekana baada ya mtoto kuzaliwa huanzia mtoto angali tumboni.

Mama hawezi kusikia mtoto anapolia kwani amezingirwa na amniotic fluid. Hakuna ushahidi bayana kuwa kulia kwa fetusi kuna sababishwa na uchungu na kukosa starehe. Kulingana na watafiti, usemi wa uso wa fetusi unawasaidia kufahamu matatizo ya kiafya ambayo mtoto anaweza kuwa nayo akiwa tumbo. Usemi wa uso ni muhimu kwani unasaidia katika utangamano wa mtoto na mazingira yake baada ya kuzaliwa. Mtoto anapolia baada ya kuzaliwa, mama anafahamu kuwa kuna kasoro mahali.
Hata hivyo, usemi wa usoni katika watoto hukomaa baada ya kuzaliwa na kuanza kuingiliana na watu. Watoto huanza kutabasamu na watu wanapofikisha umri wa miezi 8. Na kicheko cha kitoto katika miezi mitano, lakini nyuso hizi huanza kukua wangali tumboni mwa mama. Hata ingawa mtoto hulia tumboni, huwa hatoi machozi anapolia hadi anapofikisha wiki nne baada ya kuzaliwa.
Soma Pia: Vidokezo 5 Vya Kupata Mimba: Kuongeza Nafasi Za Kupata Mtoto Kirahisi