Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Mtoto Ni Nani Kibibilia? Jinsi Ya Kulea Watoto Wanao Mwamini Mungu

3 min read
Mtoto Ni Nani Kibibilia? Jinsi Ya Kulea Watoto Wanao Mwamini MunguMtoto Ni Nani Kibibilia? Jinsi Ya Kulea Watoto Wanao Mwamini Mungu

Kuelewa mtoto ni nani kibibilia kunawasaidia wazazi kumlea kwa njia inayofaa ya kibibilia kulingana na matakwa ya Mwenyezi Mungu.

Tofauti na dunia ya hapo awali, ambapo walimwogopa Maulana na kujitenga na mambo ambayo hayakubaliki katika jamii, katika dunia ya leo, hali ya kumwogopa Mungu imepungua. Vitu vinavyokubalika katika jamii vimebadilika na hata ingawa hapo awali havikukubalika, leo hii vyaonekana ni vitu vya kawaida. Je, ni tabia zipi ambazo nyanya zetu hawakukubali ila leo zaonekana za kawaida? Wazazi wanao mcha Mungu wangependa kuendeleza imani hii ya kumwamini Mungu katika watoto wao. Ni muhimu kwa wazazi kuelewa mtoto ni nani kibibilia na jinsi ambavyo wanaweza kuwalea watoto wanao mwamini Mungu.

Kuwalea Watoto Wanao Mwamini Mungu

mtoto ni nani kibibilia

  1. Kuwa mfano mwema wa kuigwa

Sawa na nyanja zingine za kimaisha, mtoto huiga anachowaona wazazi wake wakifanya na wala sio wanacho mwambia. Kuwa mtu mwenye utu, kama bibilia inavyohimiza. Kuwa mkarimu na mwenye moyo mkunjufu kwa watu walio karibu nanyi. Kuwa mkristo na kumwamini Mungu sio suala la kwenda kanisani na kusoma bibilia, mbali ni utendaji wa unachosoma katika bibilia na kuwa na vitendo chanya.

Bila shaka mtoto wako atakua akifahamu jinsi ambavyo mtu anaye mcha Mungu anavyopaswa kuwa.

2. Omba pamoja na watoto wako

Fanya mtindo wa kuomba na watoto wako kila mara. Anza siku kwa maombi kabla ya kuanza siku na baada ya kutamatisha siku kabla ya kulala kama familia. Maombi yataongeza imani yao na kuwasaidia kujitenga na mambo yasiyo mpendeza Mungu. Maombi yanasaidia watoto kuwa na imani moyoni na kufahamu kuwa kila kitu kinachotendeka maishani huwa mpango wa Mungu.

3. Wafunze watoto wako

mtoto ni nani kibibilia

Kama bibilia inavyosema kuwa, mfunze mtoto wako kutembea kwa njia zinazo mpendeza Mungu na kamwe hawatatoka katika njia hizo. Wazazi wanaotaka kuwalea watoto wanao mwamini na kumwogopa Mungu wanapaswa kuangazia somo hilo. Wazazi wanapaswa kuwafunza watoto neno la Mungu. Tenga wakati kila wiki kusoma bibilia pamoja na watoto wako, kusikiliza neno la Mungu pamoja kwa televisheni.

Kwa kufanya hivi, watoto hawa watakuwa wakitenga muda wa kusoma bibilia na kuomba hata wanapokuwa watu wazima.

4. Zingatia sinema wanazotazama

Kuna sinema za aina tofauti, na zingine sio sawa kwa watoto, zingine hazikubaliki katika jamii, ila bado zinapatikana. Iwapo ungetaka kulea watoto wanaomcha Mungu, kuwa mwangalifu kwa sinema na nyimbo ambazo watoto wako wanasikiliza. Sinema zinachangia pakubwa katika upotovu ulioko. Wafunze kutizama sinema zisizo na mambo kadri ya matakwa ya Mungu.

5. Washauri kuhusu urafiki

Shinikizo kati ya marafiki ni changio kubwa la kupotoka katika watoto na hata watu wazima. Kwa wazazi wanao fahamu mtoto ni nani kibibilia na anavyopaswa kuwa, watakuwa makini na marafiki wa watoto wao. Ikiwa mwanao ni mzuri ila ana marafiki waliopotoka, atafuata mkondo wao. Kuwa na marafiki wenye tabia chanya na wanaomcha Mungu kutawasaidia kubaki katika njia zinazompendeza Maulana.

Chanzo: Christianbook.com

Soma Pia: Kudumisha Uhusiano wa Kibinadamu na Familia Baada ya Kufunga Ndoa

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Parenting
  • /
  • Mtoto Ni Nani Kibibilia? Jinsi Ya Kulea Watoto Wanao Mwamini Mungu
Share:
  • Sababu 3 Kwa Nini Wanawake Wanachelewa Kupata Watoto

    Sababu 3 Kwa Nini Wanawake Wanachelewa Kupata Watoto

  • Vidokezo 5 vya Ulezi wa Kidijitali Ambavyo Wazazi Wanapaswa Kuangazia

    Vidokezo 5 vya Ulezi wa Kidijitali Ambavyo Wazazi Wanapaswa Kuangazia

  • Ishara 5 Kuwa Hauko Tayari Kufunga Ndoa

    Ishara 5 Kuwa Hauko Tayari Kufunga Ndoa

  • Sababu 3 Kwa Nini Wanawake Wanachelewa Kupata Watoto

    Sababu 3 Kwa Nini Wanawake Wanachelewa Kupata Watoto

  • Vidokezo 5 vya Ulezi wa Kidijitali Ambavyo Wazazi Wanapaswa Kuangazia

    Vidokezo 5 vya Ulezi wa Kidijitali Ambavyo Wazazi Wanapaswa Kuangazia

  • Ishara 5 Kuwa Hauko Tayari Kufunga Ndoa

    Ishara 5 Kuwa Hauko Tayari Kufunga Ndoa

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2022 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it