Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Nifanye Nini Ili Nipate Usingizi? Njia 7 Za Kukusaidia Kupata Usingizi Kwa Kasi

3 min read
Nifanye Nini Ili Nipate Usingizi? Njia 7 Za Kukusaidia Kupata Usingizi Kwa KasiNifanye Nini Ili Nipate Usingizi? Njia 7 Za Kukusaidia Kupata Usingizi Kwa Kasi

Nifanye nini ili nipate usingizi usiku? Hakikisha kuwa chumba chako ni kisafi, zingatia ratiba ya kulala kisha upunguze unywaji wa kaffeini.

Nifanye nini ili nipate usingizi? Swali maarufu kwa watu wanaotatizika na kukosa usingizi. Kukosa usingizi ni jambo linalotia shaka, hata ingawaje, sio kila mtu anayetatizika na hali hii. Kuna baadhi ya watu ambao hulala punde tu wanapoingia kitandani na kufumba macho. Huku wengine wakibaki kuimba nyimbo za kujilaza.

Kutopata usingizi huwa na athari hasi siku ifuatayo. Kama vile kupunguka kwa utendaji kazi wako, kukosa uwezo wa kumakinika na kuzingatia, kulala kazini ama darasani na kuhisi uchovu siku yote. Kabla ya kuchukua tembe za kusaidia kulala kuna njia za kiasili zinazosaidia kulala vyema usiku.

Nifanye nini ili nipate usingizi

nifanye nini ili nipate usingizi

Fanya haya ili upate usingizi:

  1. Tengeneza ratiba ya kulala

Kutokuwa na wakati haswa wa kuingia kitandani huwa chanzo cha kukosa usingizi. Ili kukabiliana na tatizo la kutopata usingizi usiku, ni muhimu kutengeneza ratiba ya kulala. Baini wakati ambao utakuwa ukiingia kitandani kila siku na uuzingatie kwa umakini. Kufanya hivi kutazoesha akili yako kulala wakati fulani unapofika.

2. Fanya mazoezi mchana ama jioni

Kufanya mazoezi kuna manufaa mengi kwa mwili. Mojawapo ya manufaa haya ni kusaidia kulala vyema zaidi usiku. Wakati unapofanya mazoezi, mwili huchoka na unapokoga, inakuwa rahisi kulala ili kuupumzisha mwili. Hata hivyo, kumbuka kutofanya mazoezi magumu jioni, kwani huenda yakawa na athari tofauti na tunazokusudia kutimiza.

3. Usitumie rununu kitandani

nifanye nini ili nipate usingizi

Kutumia simu kitandani kuna ashiria ubongo uendelee kufanya kazi katika wakati unapostahili kuwa ukilala. Watu wanaotumia simu usiku hasa wakiwa kitandani huenda wakatatizika kupata usingizi. Hakikisha hautumii simu ama vifaa vingine vya kiteknolojia kitandani.

4. Usilale mchana

Epuka kulala mchana, hasa kulala zaidi ya masaa mawili. Watu wanaokuwa na mazoea ya kulala kwa zaidi ya masaa mawili kwa siku wameshuhudiwa kutatizika kupata usingizi usiku. Hata unapokosa usingizi usiku, haushauriwi kulala kwa kipindi kirefu mchana. Badala yake, tafuta vitu vya kufanya ili usitatizike kulala tena usiku.

5. Epuka kutumia kaffeini na bidhaa zake usiku

Kaffeini hutumika kuamsha ubongo na kukufanya uwe makini zaidi, unapokunywa kaffeini ama bidhaa zake usiku, una athiri muundo wako wa usingizi. Punguza kiwango cha kaffeini unachochukua mchana. Ikiwa unatatizika kupata usingizi, jitenge na utumiaji wa kaffeini na bidhaa zake kwa muda.

6. Zingatia ratiba ya lishe yenye afya

Watu wanaokula chakula kingi kisha kuenda kulala muda mfupi baada yake, huenda wakatatizika kupata usingizi. Mwili huchukua muda kuchakata chakula, unapolala tu baada ya kumaliza kula, mwili ungali unakifanyia chakula kazi na huenda ukahisi kutapika ama kichefuchefu. Upe mwili wakati tosha kuchakata chakula kabla ya kulala.

7. Sikiliza muziki wa kulala

Kuna baadhi ya muziki unaosaidia kukupumzisha. Kusikiliza aina hii ya muziki unapoenda kulala, huenda kukasaidia kupata usingizi kwa kasi zaidi. Hata hivyo, ni vyema kukumbuka kuwa, siyo kila mtu anayefaidika na jambo hili.

Tuna tumai kuwa swali lako la, nifanye nini ili nipate usingizi limejibiwa. Ikiwa baada ya kutumia mbinu tulizoangazia bado unatatizika kupata usingizi, wasiliana na daktari. Huenda ukawa na matatizo ya kiafya yanayokukosesha usingizi.

Je, kuna mbinu zaidi unazofahamu za kusaidia kupata usingizi usiku? Tujulishe kwa kuwacha ujumbe mfupi hapa chini!

Chanzo: Healthline

Soma Pia: Manufaa Ya Kula Kitunguu Saumu Kwa Afya Yako

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Health
  • /
  • Nifanye Nini Ili Nipate Usingizi? Njia 7 Za Kukusaidia Kupata Usingizi Kwa Kasi
Share:
  • Orodha Ya Faida Ya Asali Mbichi Kwa Mjamzito

    Orodha Ya Faida Ya Asali Mbichi Kwa Mjamzito

  • Jinsi Ya Kupunguza Kuvimbiwa Kwa Tumbo Kwa Njia Rahisi

    Jinsi Ya Kupunguza Kuvimbiwa Kwa Tumbo Kwa Njia Rahisi

  • Kufanya Ngono Baada Ya Kukoma Hedhi: Vidokezo Muhimu Vya Kuzingatia

    Kufanya Ngono Baada Ya Kukoma Hedhi: Vidokezo Muhimu Vya Kuzingatia

  • Orodha Ya Faida Ya Asali Mbichi Kwa Mjamzito

    Orodha Ya Faida Ya Asali Mbichi Kwa Mjamzito

  • Jinsi Ya Kupunguza Kuvimbiwa Kwa Tumbo Kwa Njia Rahisi

    Jinsi Ya Kupunguza Kuvimbiwa Kwa Tumbo Kwa Njia Rahisi

  • Kufanya Ngono Baada Ya Kukoma Hedhi: Vidokezo Muhimu Vya Kuzingatia

    Kufanya Ngono Baada Ya Kukoma Hedhi: Vidokezo Muhimu Vya Kuzingatia

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2022 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it