Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Rais Wa Tatu Wa Kenya Emilio Mwai Kibaki Afariki

2 min read
Rais Wa Tatu Wa Kenya Emilio Mwai Kibaki AfarikiRais Wa Tatu Wa Kenya Emilio Mwai Kibaki Afariki

Rais wa tatu wa Kenya Emilio Mwai Kibaki afariki akiwa na miaka 90. Rais wa sasa wa Kenya Uhuru Kenyatta athibitisha.

Rais wa tatu wa nchi ya Kenya, Emilio Mwai Kibaki afariki. Kifo chake kimetangazwa na rais wa Kenya Uhuru Kenyatta katika press briefing siku ya Ijumaa Aprili tarehe 22 mwaka wa 2022.

Rais Wa Tatu Wa Kenya Emilio Mwai Kibaki Afariki

Picha: The Nation

“Ni siku ya huzuni kwetu kama nchi. Tumepoteza kiongozi mkubwa, raisi wa zamani mzee Mwai Kibaki, rais Uhuru Kenyatta alisema.

“Alikuwa mtu wa heshima na hadhi ambaye maisha yake yatazidi kuwahamasisha wananchi wa Kenya muda katika siku zao za usoni. Tunakumbuka maadili aliyofuata maishani, heshima yake, uangalifu wake, kuhusika kwake kuhusu ustawi wa wakenya wote. Kama mmojawapo ya watu walioongoza nchi baada ya kupata uhuru, rais Mwai Kibaki alipata heshima na mapenzi kutoka kwa wananchi na nchi zingine duniani kote. Daima atakumbukwa kama mtu mashuhuri katika siasa za Kenya ambaye weledi, ujasiri na maarifa yake yalishinda kila siku, muda baada ya mwingine,” rais Uhuru alizidi kusema.

Rais Wa Tatu Wa Kenya Emilio Mwai Kibaki Afariki

Picha: The Nation

Kamwe hatasahaulika kwa yote aliyochangia alipokuwa waziri wa fedha, mdogo wa rais na rais wa nchi ya Kenya. Katika uongozi wake kama rais wa nchi, uchumi ulishuhudia ustawi mkubwa, ambao kamwe haujaweza kudhihirika muda baada ya uongozi wake.

Kama rais, aliapa kuondoa utoaji rushwa uliokuwa umeharibu ustawi na uchumi wa nchi, uliokuwa umefanya nchi za nje kutosaidia Kenya. Kibaki aliongoza nchi kutoka mwezi wa Disemba mwaka wa 2007 hadi Aprili mwaka wa 2013.

Marehemu raisi wa zamani Mwai Kibaki atakumbukwa kwa mengi aliyotimiza alipokuwa rais, weledi wake, utulivu wake, ujasiri wake katika uongozi wake na bila shaka ucheshi wake.

Amefariki akiwa na miaka 90. Lala pema peponi rais Mwai Kibaki.

Chanzo: Citizen

Soma Pia:Harusi Ya Kufana Ya Rita Dominic na Fidelis Anosike

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Lifestyle
  • /
  • Rais Wa Tatu Wa Kenya Emilio Mwai Kibaki Afariki
Share:
  • Vidokezo Vya Ndoa Kwa Kila Mwanamke

    Vidokezo Vya Ndoa Kwa Kila Mwanamke

  • Jinsi ya Kudumisha Ulaji wa Vitafunio Vyenye Afya Kazini

    Jinsi ya Kudumisha Ulaji wa Vitafunio Vyenye Afya Kazini

  • Lishe Bora Kwa Wanawake Waliofikisha Umri wa Kukoma Hedhi

    Lishe Bora Kwa Wanawake Waliofikisha Umri wa Kukoma Hedhi

  • Vidokezo Vya Ndoa Kwa Kila Mwanamke

    Vidokezo Vya Ndoa Kwa Kila Mwanamke

  • Jinsi ya Kudumisha Ulaji wa Vitafunio Vyenye Afya Kazini

    Jinsi ya Kudumisha Ulaji wa Vitafunio Vyenye Afya Kazini

  • Lishe Bora Kwa Wanawake Waliofikisha Umri wa Kukoma Hedhi

    Lishe Bora Kwa Wanawake Waliofikisha Umri wa Kukoma Hedhi

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it