Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Sababu Za Kukosa Kupata Hedhi Kwa Wanawake Kwa Muda Mrefu

2 min read
Sababu Za Kukosa Kupata Hedhi Kwa Wanawake Kwa Muda MrefuSababu Za Kukosa Kupata Hedhi Kwa Wanawake Kwa Muda Mrefu

Kutumia mbinu za uzazi wa mpango zilizo na homoni humfanya mwanamke kukosa kupata hedhi. Tazama sababu za kukosa hedhi katika wanawake.

Kipindi cha hedhi cha kila mwezi huwa ishara ya hadhi ya mwanamke. Mwanamke anapokosa kupata hedhi, ni kawaida kuwa na mawazo mengi. Na mara nyingi kushangaa iwapo ana tatizo la kiafya ama ana mimba. Kukosa hedhi na kuwa na vipindi vya hedhi visivyo vya kawaida sio jambo geni kwa wanawake. Hata hivyo, ni vyema kuwasiliana na daktari wako unaposhuhudia jambo hili. Je, sababu za kukosa hedhi ni kama zipi?

Utaratibu wa kushuhudia hedhi

kuvuja damu katika ujauzito

Kila mwezi, mwanamke hutoa ovari kutoka kwa mirija ya ovari. Mzunguko wa kawaida huwa kati ya siku 25 hadi 28. Yai linapokutana na mbegu za kiume, lina rutubishwa na fetusi kuumbwa. Yai la mwanamke lisipo kutana na manii, ukuta wa ndani ya uterasi huporomoka na mwanamke kupata hedhi. Mwanamke anapokosa kupata hedhi, ni ashirio kuwa huenda akawa na mimba ama matatizo mengine ya kiafya. Kukosa kupata hedhi kuna mweka mama katika hatari ya kutatizika kutunga mimba.

Kukosa hedhi mara nyingi husababishwa na kuvurugika kwa vichocheo mwilini. Njia ya kufahamu iwapo vichocheo mwilini vimevurugika ni kwa kuzingatia kuoa dalili hizi. Kuhisi uchungu mwingi unapokuwa na hedhi, kukosa kupata hedhi, kuchelewa kupata hedhi na kuwa na hedhi inayopitiliza wiki moja.

Sababu za kukosa hedhi

Baadhi ya sababu zinazomfanya mwanamke kukosa kupata vipindi vyake vya hedhi ni kama vile:

Kusongwa na mawazo

Unapokuwa na mawazo mengi, utendaji kazi wa kawaida mwilini hudhoofika, na kufanya kupevushwa kwa yai kuwa ngumu. Utoaji mdogo wa kichocheo cha estrogen hufanya iwe vigumu kupata hedhi.

Uzito mdogo wa mwili

Kuwa na uzito mdogo wa mwili huwafanya wanawake wakatatizika kupata vipindi vyao vya hedhi. Kwani uzalishaji wa homoni ya hedhi, estrogen, huwa duni na kufanya iwe vigumu kupata hedhi.

Lishe duni

sababu za kukosa hedhi

Lishe isiyo na chakula kutoka vikundi vyote ikiwemo mboga, matunda na madini hufanya tezi za adrenal kufanya kazi nyingi kuliko inavyo stahili. Kichocheo kinachotolewa mwilini cha cortisol hufanya iwe vigumu kwa mwili kuzalisha homoni ya estrogen inayo husika na kusababisha hedhi kutendeka.

Mbinu za uzazi wa mpango

Kuna baadhi ya mbinu za kupanga uzazi zinazo mfanya mwanamke kutopata hedhi. Kumeza tembe za dharura baada ya kufanya ngono isiyo salama humfanya mwanamke kupata hedhi siku baada ya wakati anapotarajia. Mbinu za kupanga uzazi zinazokuwa na homoni huathiri hedhi ya mwanamke.

Chanzo: Healthline

Soma Pia: Sifa Za Hedhi Baada Ya Mimba Kutoka Ikilinganishwa Na Hedhi Ya Kawaida

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Health
  • /
  • Sababu Za Kukosa Kupata Hedhi Kwa Wanawake Kwa Muda Mrefu
Share:
  • Je, Kiamsha Kinywa Kina Manufaa Mwilini?

    Je, Kiamsha Kinywa Kina Manufaa Mwilini?

  • Vyanzo 5 vya Kuhisi Uvimbe na Maumivu ya Tumbo

    Vyanzo 5 vya Kuhisi Uvimbe na Maumivu ya Tumbo

  • Dalili za Ugumba Kwa Wanaume na Jinsi ya Kujikinga Dhidi ya Hali Hii

    Dalili za Ugumba Kwa Wanaume na Jinsi ya Kujikinga Dhidi ya Hali Hii

  • Je, Kiamsha Kinywa Kina Manufaa Mwilini?

    Je, Kiamsha Kinywa Kina Manufaa Mwilini?

  • Vyanzo 5 vya Kuhisi Uvimbe na Maumivu ya Tumbo

    Vyanzo 5 vya Kuhisi Uvimbe na Maumivu ya Tumbo

  • Dalili za Ugumba Kwa Wanaume na Jinsi ya Kujikinga Dhidi ya Hali Hii

    Dalili za Ugumba Kwa Wanaume na Jinsi ya Kujikinga Dhidi ya Hali Hii

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it