Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Sabrina Elba, Mkewe Idris Elba Ako Kenya Kutembelea Miradi ya Kilimo Ambayo UN Inawekeza

2 min read
Sabrina Elba, Mkewe Idris Elba Ako Kenya Kutembelea Miradi ya Kilimo Ambayo UN InawekezaSabrina Elba, Mkewe Idris Elba Ako Kenya Kutembelea Miradi ya Kilimo Ambayo UN Inawekeza

Sabrina Elba ako Kenya ambapo anapatana na wakulima wa nchi na pia kuweza kuona jinsi michakato ya UN kwa IFAD inawasaidia wanawake vijijini.

Sabrina Elba ako Kenya!

Sabrina ambaye ni mke wake Idris Elba mwigizaji mashuhuri anayejulikana kwa sinema kama The Wire, Luther na Nelson Mandela.

sabrina elba

Picha: Sabrina Elba Instagram

Kwenye kurasa yake ya mtandao wa kijamii wa Instagram, Bi. Elba aliandika kuwa ana furaha kuwa Kenya. Kama balozi wa UN wa IFAD, anatembelea miradi ambayo shirika hili limewekeza. Alipatana na wanaume na wanawake wanaojitahidi kila siku kukuza chakula kinachowalisha wananchi. Hata hivyo, wakaazi wa eneo la Embu ni baadhi ya watu walioathiriwa zaidi na athari za mabadiliko ya hali ya hewa. Alisikiliza hadithi kuhusu changamoto zao, matumaini na kujitahidi walizomwelezea.

Sabrina Elba, Mkewe Idris Elba Ako Kenya Kutembelea Miradi ya Kilimo Ambayo UN Inawekeza

Picha: Sabrina Elba Instagram

Familia ya Sabrina Elba

Sabrina Dhowre Elba ni mtoto wake Marya Megal ambaye ni mzaliwa wa Somalia. Mnamo Aprili tarehe 25 mwaka wa 2020, Sabrina Elba aliteuliwa kuwa balozi wa UN wa IFAD. Lengo likiwa kuwawezesha wanawake na wasichana vitongojini.

Marya alipokuwa miaka 16, alitoka nchini Somalia na kuenda Canada kuanza maisha upya. Dhidi ya kuenda nchi geni, Marya alifanya juu chini kuhakikisha kuwa watoto wake wanafahamu lugha yao ya mama, kisomali, wanazifahamu tamaduni zao na njia ya maisha ya watu wa Somalia.

Kila alipoweza, alihakikisha kuwa amewapeleka kuzuru Somalia. Jambo ambalo Sabrina alisema ni muhimu wa utambulisho wake. Kuzuru Somalia kulimfanya akaipenda nchi ile, ngamia za huko, joto ya jua na watu wa Somalia.

Kulingana na Sabrina, mamake alimfunza umuhimu wa maendeleo ya kilimo, hasa unapotegemea shamba kuishi. Anafahamu jinsi kisima na umwagiliaji maji unaweza kubadilisha maisha. Na kuwa pia alifahamu jinsi wanawake kutoka bara la Afrika wanahangaika. Sabrina aliandika kwenye kurasa yake ya mtandao wa kijamii wa Instagram.

Kujumuika na IFAD

Sabrina Elba, Mkewe Idris Elba Ako Kenya Kutembelea Miradi ya Kilimo Ambayo UN Inawekeza

Picha: Sabrina Elba Instagram

Marya ndiye aliyekuwa mtu wa kwanza kuwajuza Sabrina na Idris Elba kuhusu shirika kubwa linalo wasaidia watu masikini vijijini na kuwa ingekuwa bora kwao kuhusika.

Sabrina alitaja kuwa kuna bilioni 1.7 ya wanawake na wasichana vijijini waliohitaji matumaini. Aliapa kuwatumikia heshima, bidii, na kwa kujitolea. Kisha kumshukuru mamake kwa kumtia msukumo wakati wote na kutumaini kuwa angemfanya aone fahari.

Sabrina Elba, Mkewe Idris Elba Ako Kenya Kutembelea Miradi ya Kilimo Ambayo UN Inawekeza

Picha: Sabrina Elba Instagram

Sabrina Elba ako Kenya ambapo anapatana na wakulima wa nchi na pia kuweza kuona jinsi michakato ya UN kwa IFAD inavyowasaidia wanawake na wasichana masikini huko vijijini.

Chanzo: Africaparent

Soma Pia:Rihanna Atangaza Kuwasilisha Bidhaa za Fentybeauty na Fentyskin Africa

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Lifestyle
  • /
  • Sabrina Elba, Mkewe Idris Elba Ako Kenya Kutembelea Miradi ya Kilimo Ambayo UN Inawekeza
Share:
  • Vidokezo Vya Ndoa Kwa Kila Mwanamke

    Vidokezo Vya Ndoa Kwa Kila Mwanamke

  • Jinsi ya Kudumisha Ulaji wa Vitafunio Vyenye Afya Kazini

    Jinsi ya Kudumisha Ulaji wa Vitafunio Vyenye Afya Kazini

  • Lishe Bora Kwa Wanawake Waliofikisha Umri wa Kukoma Hedhi

    Lishe Bora Kwa Wanawake Waliofikisha Umri wa Kukoma Hedhi

  • Vidokezo Vya Ndoa Kwa Kila Mwanamke

    Vidokezo Vya Ndoa Kwa Kila Mwanamke

  • Jinsi ya Kudumisha Ulaji wa Vitafunio Vyenye Afya Kazini

    Jinsi ya Kudumisha Ulaji wa Vitafunio Vyenye Afya Kazini

  • Lishe Bora Kwa Wanawake Waliofikisha Umri wa Kukoma Hedhi

    Lishe Bora Kwa Wanawake Waliofikisha Umri wa Kukoma Hedhi

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it