Kutoa mimba ni hali ya kusimamisha ama kuondoa mimba kwa hiari. Kuna njia mbalimbali ambazo hutumika kukomesha ujauzito aidha nyumbani ama kwenye hospitali. Mojawapo wa hizo njia ni sindano inayotumika kutoa mimba.
Sindano Inayotumika Kutoa Mimba

- Sindano ya Oxytocin
Sindano ya oxytocin ni homoni ya asili. Hii hufanya kazi kwenye uterasi. Matumizi yake huoana na jinsi inavyofanya kazi kwa kuongeza nguvu ya mikazo ya uterasi.
Kwa hivyo inaweza kutumika: wakati wa kujifungua kuimarisha mikazo ya leba, kushawishi leba, baada ya kujifungua kudhibiti kutokwa na damu, baada ya utoaji mimba usio kamili ili kutoa chochote kilichobaki ndani ya uterasi. Hutumika baada ya kuharibika kwa mimba. Pia hii sindano hutumika kutoa mimba.
Madhara ya kutumia sindano ya Oxytocin
Kuna madhara ambayo imehusishwa na hio sindano : Uwekundu ama kuwashwa kwenye tovuti ya sindano, kupoteza hamu ya chakula, kichefuchefu, kutapika, kubana kwa tumbo la chini, maumivu ya tumbo, mikazo mikali zaidi ya mara kwa mara na matatizo ya kumbukumbu.
- Sindano ya Misuli ya Sulprostone
Sindano za ndani ya misuli ya analog mpya PGE2(sulprostone) ilipewa wagonjwa hamsini na saba kwa utoaji wa mimba wa miezi mitatu ya kwanza. Utafiti ulifanywa kutathmini ufanisi na kiwango cha athari katika utoaji mimba uliosababishwa na sulprostone .
Wanawake wa afya 57 kati ya ujauzito wa wiki 10 hadi 16 walichaguliwa bila mpangilio wowote. Utaratibu huu uliitwa kutofaulu iwapo mwanamke hatakuwa ametoa mimba baada ya masaa 24 baada ya sindano ya kwanza. Wanawake 19 walitoa mimba ndani ya masaa 12 wengine 52 ndani ya masaa 24.
Madhara ya kutumia sindano ya misuli ya Sulprostone
Athari ya upele wa ngozi na kuwashwa, uvimbe wa uso, ulimi au midomo, shida za kupumua, kutokwa na damu nyingi ukeni, mipigo ya moyo yasiyo ya kawada, shinikizo la damu na kuhisi kuzimia.
Njia Nyingine za Kutoa Mimba

Njia hii inahusisha kutumia dawa ambazo husababisha tumbo la uzazi kubana na kutoa nje ujauzito.
Huhusisha kuchukua kidonge cha kwanza cha mifepristone. Hii hufanya kazi kwa kuzuia hatua ya homoni(progesterone) inayounga mkono ujauzito. Kisha unachukua kidonge cha pili cha misoprotol baada ya masaa 24 hadi 48. Hii husababisha tumbo la uzazi kutoa mimba.
- Utoaji mimba kwa njia ya kunyonya au kufyonza
Mimba hutolewa kwa kutumia mirija maalum. Hii huiingizwa kwenye tumbo la uzazi kupitia uke na mlango wa tumbo la uzazi. Sio lazima mama atumie dawa za usingizi ila wakati mwingine huchomwa kwenye mlango wa kizazi kusaidia kupunguza maumivu. Ni rahisi na ni salama kwa mwanamke. Huchukua dakika 5 hadi 10.
- Kutumia vifaa vya ukwanguaji (upanuaji na ukwanguaji)
Hii hufanyika kwa kutumia kifaa kiitwacho curette. Hufanana na kijiko kidogo na kimetengenezwa maalum ili kiingizwe kwenye tumbo la uzazi. Kifaa hiki huwa kikubwa na kikali hivyo basi lazima mlango wa kizazi kutanuliwa. Huu utanuaji huweza kusababisha maumivu. Huhusisha muda mwingi na maumivu hivyo mwanamke hupewa dawa za usingizi.
Kuna njia kadha wa kadha ambazo mwanamke anaweza kutumia kumaliza ujauzito. Ila wengi hawafahamu kuwa kuna sindano inayotumika kutoa mimba.
Soma Pia: Je, Dawa Ya Amplicox Inatumika Kuzuia Mimba?