Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Njia 3 Salama Za Kuavya Mimba: Sindano Ya Kutoa Mimba Inatumika Vipi?

2 min read
Njia 3 Salama Za Kuavya Mimba: Sindano Ya Kutoa Mimba Inatumika Vipi?Njia 3 Salama Za Kuavya Mimba: Sindano Ya Kutoa Mimba Inatumika Vipi?

Utoaji wa mimba nchini Kenya umepigwa marufuku. Hata hivyo, kuna wakati ambapo utaratibu huu unakubalika, fahamu zaidi kuhusu nyakati hizi!

Kuavya ama kutoa mimba ni tendo la hiari la kukomesha ukuaji wa mimba tumboni mwa mwanamke. Sababu tofauti zinamfanya mama kufika kwenye uamuzi huu. Kuna mbinu tofauti zinazotumika kufanya hili, kama kutumia sindano ya kutoa mimba, na kutumia tembe za kutoa mimba.

Sheria za Utoaji Mimba Nchini Kenya

sindano ya kutoa mimba

Utoaji wa mimba nchini Kenya umepigwa marufuku ila katika visa ambapo mama alibakwa, ama mimba inapohatarisha maisha yake. Kuavya mimba kwa njia zisizo salama ni chanzo kikuu cha vifo na matatizo ya kiafya kwa wanawake wengi nchini Kenya. Kutumia njia hatari kutoa mimba kunamweka mama katika hatari ya kuvuja damu kupindukia na kupoteza maisha yake ama kuharibika kwa uterasi yake.

Kulingana na katiba ya Kenya Makala 26(IV), utoaji wa mimba haukubaliki usipofanywa na mtaalum wa afya aliye na maarifa ya kufanya kitendo hicho, hali ya matibabu ya dharura ama maisha ya mama yamo hatarini.

Njia salama za kuavya mimba

  • Kutumia vifaa vya upanuaji na ukwanguaji

Kifaa kinachofahamika kama curette kilicho sawa na kijiko kidogo kimetengenezwa maalum cha kuingizwa kwenye tumbo la uzazi. Kinatumika kukwangua mimba. Kinapanua mlango wa uzazi ili kiweze kufika kwenye tumbo la uzazi. Mbinu hii ya utoaji wa mimba huwa na uchungu mwingi.

  • Kutumia dawa

Dawa za kutoa ujauzito hufanya kazi kwa kubana kisha kutoa mimba nje. Dawa hizi zilizo kwa aina ya tembe humezwa ama kuingizwa kwenye uke. Inapotumika kwa njia sahihi, huwa na ufanisi mkubwa. Ndani ya masaa matatu, mwanamke huwa ameanza kuvuja damu. Hata hivyo, mbinu hii ya kuavya mimba humweka mwanamke katika hatari ya kupata maambukizi na anapaswa kuchukua dawa za antibacterial kumlinda dhidi ya kuugua. Dawa hizi hupatikana kwenye vituo vya hospitali peke yake.

  • Sindano ya kutoa mimba

sindano ya kutoa mimba

Ujauzito hutolewa kwa kunyonywa kutumia sindano maalum inayoingizwa kwenye mlango la uzazi hadi kwenye tumbo la uzazi. Huwa bora mbinu hii inapofanyika kwa ujauzito ndani ya miezi mitatu, baada ya hapo, mama huwa katika hatari. Mwanamke aliyejaribu kutoa mimba kisha utaratibu huo kutomalizika ifaavyo, mbinu hii inatumika kutoa mabaki.

Mbinu yoyote ile ya kutoa mimba inapaswa kufanyika kwenye kituo cha hospitali na mtaalum mwenye mafunzo ya kufanya kitendo hicho. Kutumia dawa za kutoa mimba kama mifepristone na misoprostol bila ushauri wa daktari kuna hatari kubwa.

Chanzo: WebMD

Soma Pia: Jinsi Ya Kutumia Vidonge Kutoa Mimba Na Athari Kwa Mwanamke

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Abortion
  • /
  • Njia 3 Salama Za Kuavya Mimba: Sindano Ya Kutoa Mimba Inatumika Vipi?
Share:
  • Matokeo 7 Mwanamke Anayoshuhudia Baada Ya Kutoa Mimba

    Matokeo 7 Mwanamke Anayoshuhudia Baada Ya Kutoa Mimba

  • Jinsi Ya Kutumia Vidonge Kutoa Mimba Na Athari Kwa Mwanamke

    Jinsi Ya Kutumia Vidonge Kutoa Mimba Na Athari Kwa Mwanamke

  • What Does It Mean To Have An Abortion?

    What Does It Mean To Have An Abortion?

  • Matokeo 7 Mwanamke Anayoshuhudia Baada Ya Kutoa Mimba

    Matokeo 7 Mwanamke Anayoshuhudia Baada Ya Kutoa Mimba

  • Jinsi Ya Kutumia Vidonge Kutoa Mimba Na Athari Kwa Mwanamke

    Jinsi Ya Kutumia Vidonge Kutoa Mimba Na Athari Kwa Mwanamke

  • What Does It Mean To Have An Abortion?

    What Does It Mean To Have An Abortion?

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it