Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Tatizo la Kukosa Usingizi Linasababishwa Na Nini Hasa?

2 min read
Tatizo la Kukosa Usingizi Linasababishwa Na Nini Hasa?Tatizo la Kukosa Usingizi Linasababishwa Na Nini Hasa?

Tatizo la kukosa usingizi pia huathiriwa na tabia hafifu za kulala kama kutumia simu kitandani na mazingira hafifu ya kulala.

Tatizo la kukosa usingizi hushuhudiwa na mamilioni ya watu kutoka sehemu tofauti duniani. Mtu anapokuwa na tatizo hili hushindwa kupata usingizi, kuendelea kulala, kuamka mapema asubuhi tofauti na ilivyo kawaida, kukosa kupata usingizi baada ya kuamka. Kukosa usingizi hakuathiri usingizi tu, mbali nyanja tofauti maishani mwako pia kama kikazi na kiasi cha ubora wako.

Kiasi cha usingizi kinachoshauriwa kuwa bora kwa afya ni kupata masaa manane ya usingizi kila usiku. Huenda mtu akatatizika na kupata usingizi kwa muda mfupi wa siku na wiki chache ama miezi mingi. Kuna sababu nyingi zinazoathiri uwezo wa kulala vyema ama kukosa usingizi usiku.

Tatizo la kukosa usingizi

tatizo la kukosa usingizi

Dalili za tatizo la kukosa usingizi

  • Kuamka katikati ya usiku
  • Kuamka alfajiri na mapema asubuhi
  • Kutatizika kupata usingizi usiku
  • Kuhisi uchovu baada ya kuamka
  • Kulegea kazini mchana

Vyanzo vya tatizo la usingizi

Kukosa usingizi ama kutatizika kufanya usingizi kunaweza sababishwa na tatizo lingine unalopitia ama kuwa hilo ndilo tatizo la kipekee. Baadhi ya sababu maarufu zinazo sababisha kukosa usingizi ni kama vile:

1.Kusafiri: Unapozoea kulala wakati fulani kila siku, mwili wako hupata ratiba ya usingizi unaofuata, wa kulala na kuamka kila siku. Unaposafiri na kubadili mazingira yako, mpango wako wa kulala huvurugika na kuifanya iwe vigumu kwako kupata usingizi kama ilivyo kawaida kwako.

tatizo la kukosa usingizi

2. Kusongwa na mawazo: Msongo wa mawazo unaosababishwa na masuala ya kimaisha kama vile ya kikazi, mapenzi, fedha, familia na masomo yanaweza kufanya iwe vigumu kwako kulala baada ya siku ndefu shuleni ama kazini. Pia, matukio makubwa maishani kama kupoteza mtu unayempenda, ugonjwa, kuwachwa na mchumba ama kupoteza kazi kuna athiri uwezo wako wa kulala.

3. Kulala mchana: Jambo lingine linalofanya iwe vigumu kupata usingizi usiku ni kulala mchana. Unapokuwa na wakati wa ziada mchana, badala ya kulala, fanya jambo lingine la kupitisha wakati, kama kuandika, kuchora, kusoma kitu kipya ama kusoma kitabu. Kulala mchana kutafanya iwe vigumu kulala usiku ama kukufanya ulale usiku zaidi kuliko ilivyo kawaida yako.

Tatizo la kukosa usingizi pia huathiriwa na tabia hafifu za kulala kama kutumia simu kitandani, mazingira hafifu ya kulala, kutazama runinga kitandani, kucheza video simuni na kadhalika.

Chanzo: WebMD

Soma Pia: Faida 7 Za Kufanya Yoga Kwa Afya Yako

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Health
  • /
  • Tatizo la Kukosa Usingizi Linasababishwa Na Nini Hasa?
Share:
  • Je, Kiamsha Kinywa Kina Manufaa Mwilini?

    Je, Kiamsha Kinywa Kina Manufaa Mwilini?

  • Vyanzo 5 vya Kuhisi Uvimbe na Maumivu ya Tumbo

    Vyanzo 5 vya Kuhisi Uvimbe na Maumivu ya Tumbo

  • Dalili za Ugumba Kwa Wanaume na Jinsi ya Kujikinga Dhidi ya Hali Hii

    Dalili za Ugumba Kwa Wanaume na Jinsi ya Kujikinga Dhidi ya Hali Hii

  • Je, Kiamsha Kinywa Kina Manufaa Mwilini?

    Je, Kiamsha Kinywa Kina Manufaa Mwilini?

  • Vyanzo 5 vya Kuhisi Uvimbe na Maumivu ya Tumbo

    Vyanzo 5 vya Kuhisi Uvimbe na Maumivu ya Tumbo

  • Dalili za Ugumba Kwa Wanaume na Jinsi ya Kujikinga Dhidi ya Hali Hii

    Dalili za Ugumba Kwa Wanaume na Jinsi ya Kujikinga Dhidi ya Hali Hii

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it