Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Tumbo Kuuma Ni Dalili Ya Mimba: Vyanzo 5 Vya Kuumwa Na Tumbo

2 min read
Tumbo Kuuma Ni Dalili Ya Mimba: Vyanzo 5 Vya Kuumwa Na TumboTumbo Kuuma Ni Dalili Ya Mimba: Vyanzo 5 Vya Kuumwa Na Tumbo

Wakati ambapo tumbo kuuma ni mojawapo ya dalili ya mimba, kuwa na mzio wa chakula ama virusi vya tumbo husababisha maumivu ya tumbo.

Kila mtu hupata matatizo ya tumbo mara kwa mara. Lakini kulingana na kiwango cha uchungu, huenda ukahitajika kutembelea kituo cha afya ili kufanyiwa vipimo kubaini chanzo cha tatizo lile. Je, tumbo kuuma ni dalili ya mimba? Maumivu ya tumbo husababishwa na mambo tofauti. Tuna angazia vyanzo vya maumivu ya tumbo.

Vyanzo vya kuumwa na tumbo

  1. Ugonjwa wa tumbo (gastritis)

Ili chakula kichakatwe tumboni, asidi nyingi inatumika. Baadhi ya wakati, huenda asidi hii ikapita kwenye tumbo na kuathiri kuta za tumbo, hali inayofahamika kama ugonjwa wa tumbo ama gastritis kwa kimombo. Hali hii pia husababishwa na bakteria, kusombwa kimawazo, watu walio na uraibu wa kunywa pombe sana wako katika hatari ya kupata ugonjwa huu. Hali hii isiporekebishwa mapema, huenda ikasababisha vidonda vya tumbo ama ulcers.

2. Vidonda vya tumbo vya peptic

Hivi ni vidonda wazi vilivyo kwenye ukuta wa tumbo. Husababishwa sana na bakteria ama utumiaji mwingi wa dawa za ibuprofen ama aspirin. Watu wanaotumia sigara na pombe sana huwa katika hatari ya kupata ugonjwa huu.

3. Virusi vya tumbo

Virusi kwenye matumboa. Mtu aliye na virusi hivi hushuhudia ishara kama kuendesha, kuumwa na tumbo, kichefuchefu na kutapika. Virusi hivi hupitishwa kupitia kwa ulaji wa chakula kilicho na virusi ama mtu aliye na virusi hivi. Sawa na virusi vingine, havina tiba, ila huisha bila matibabu.

4. Sumu kupitia chakula (Food poisoning)

Ugonjwa huu husababishwa na virusi, bakteria na viini vilivyo kwenye chakula. Mtu aliye na ugonjwa huu huwa na ishara kama kichefuchefu, kutapika na kuharisha. Hupungua baada ya muda. Lakini unapoanza kutapika damu, ni muhimu kwenda kwenye kituo cha afya kufanyiwa vipimo.

 5. Mzio wa chakula

Hufanyika mwili unapochukulia chakula ulichokila kama kitu hatari na kujaribu kuulinda mwili wako. Ishara zake huwa kuumwa na tumbo, kufura mdomo ama koo na kuhisi kujikuna ngozi. Katika hali sugu, huenda ukasababisha kifo, ni vyema kuchukua dawa ya epinephrine punde tu chakula ulichochukua kinaanza kuwa na athari hasi kwa mwili wako. Baadhi ya vyakula vilivyo na mzio ni kama njugu, mayai, siagi, maziwa na vyakula vya baharini.

Tumbo kuuma ni dalili ya mimba? La hasha, kuumwa na tumbo sio ishara ya kuwa na mimba wakati wote. Unapoumwa na tumbo na kukosa hedhi, nafasi kubwa ni kuwa una mimba. Lakini unapoumwa na tumbo peke yake, sio ishara ya tumbo, ni vyema kufanyiwa vipimo kubaini chanzo chake.

Chanzo: WebMD

Soma Pia: Vyanzo Vya Maumivu Makali Kwa Matiti Katika Wanawake

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Health
  • /
  • Tumbo Kuuma Ni Dalili Ya Mimba: Vyanzo 5 Vya Kuumwa Na Tumbo
Share:
  • Je, Kiamsha Kinywa Kina Manufaa Mwilini?

    Je, Kiamsha Kinywa Kina Manufaa Mwilini?

  • Vyanzo 5 vya Kuhisi Uvimbe na Maumivu ya Tumbo

    Vyanzo 5 vya Kuhisi Uvimbe na Maumivu ya Tumbo

  • Dalili za Ugumba Kwa Wanaume na Jinsi ya Kujikinga Dhidi ya Hali Hii

    Dalili za Ugumba Kwa Wanaume na Jinsi ya Kujikinga Dhidi ya Hali Hii

  • Je, Kiamsha Kinywa Kina Manufaa Mwilini?

    Je, Kiamsha Kinywa Kina Manufaa Mwilini?

  • Vyanzo 5 vya Kuhisi Uvimbe na Maumivu ya Tumbo

    Vyanzo 5 vya Kuhisi Uvimbe na Maumivu ya Tumbo

  • Dalili za Ugumba Kwa Wanaume na Jinsi ya Kujikinga Dhidi ya Hali Hii

    Dalili za Ugumba Kwa Wanaume na Jinsi ya Kujikinga Dhidi ya Hali Hii

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it