Zawadi bora zaidi ambayo unaweza mpa mtoto wako kama mzazi wake, ni zawadi ya kumlea vyema. Ila ulezi bora huenda ukawa na matatizo na changamoto nyingi kwani kuna hadithi na imani nyingi za ulezi mwema wa kuchagua kutoka. Uislamu ni njia ya maisha ambayo ina mtazamo wa kijumla wa kuisha maisha mema. Kwa hivyo, kuna maana Mwislamu kutaka ukumbatie mbinu ya ulezi wa kiislamu. Tume orodhesha kanuni 5 za ulezi wa kiislamu.
Watoto ni amanah, ni jukumu kadri tu walivyo zawadi kwa wazazi wao. Jukumu lako ni kuhakikisha kuwa watakuwa na bidii ya kufanya kazi, kumwogopa Mungu na ambao ni umiliki kwenye Ummah. Ulezi wa Kiislamu umegawanyika kulingana na sehemu tatu muhimu ambazo wazazi wanawadai watoto wao. Hizi ni: kifizikia, kiakili na usalama wa kihisia.
Kanuni Za Ulezi Wa Kiislamu, Kutoka Kwa Hadith
Kanuni ya 1: Watoto wanazaliwa wakiwa wasafi
Kulingana na nabii Muhammad, “Hakuna mtoto anaye zaliwa mbali kwa al-fitra (Kiislamu ama primordial human nature) kisha wazazi wake kumfanya myehudi, mkristo ama Magian, kwani mnyama hutoa mnyama mwingine msafi: unaona sehemu yoyote ya mwili wake ikiwa imefanyiwa upasuaji?" [Sahih Muslim]
Allah ameumba watoto na mapenzi ya kiasili ya mazuri na kuamini Mwenyezi Mungu. Haiko katika mtoto kufanya mbaya ama maovu. Kwa hivyo usimlaumu mtoto anapo fanya kitu kibaya, hadi anapo kuwa na umri wa miaka 10. Sio uamuzi wake kufanya mabaya, anaiga anacho ona, kusikia, kuhisia na kusoma kutoka kwa mazingara yake.
Kitendo: Kumbuka kuwa mtoto wako ni msafi bila doa. Iwapo anafanya matendo mabaya, kagua mazingara yake kudhibitisha chanzo na kisha utafute suluhu.
Kanuni ya 2: Mzazi ni mwongozo na mtu wa kuigwa
"Kila mmoja wenu ni mlezi na anapaswa kuwajibika na mashtaka yake. Anaye ongoza ana mamlaka juu ya watu, ni mlezi na ana jukumu kwao; mwanamme ni mlezi wa familia yake na ana jukumu kwao; mwanamke ni mlinzi wa nyumba ya bwana yake na ana jukumu kwa watoto; mtumwa ni mlinzi wa mali ya bosi wake na ana jukumu; kwa hivyo nyote mna jukumu kwa malipo ama mashtaka yenu.” [Sahih al-Bukhari]
Wazazi ndiyo walio patiwa jukumu na Mungu la kuongoza, na kuchunga watoto wao. Fanya vyema kuchukua jukumu hili kwa makini na kuhakikisha kuwa wana kuwa kwenye al-fitr na kufuata Allah na Mtumwa wake. Kisha ataendelea kufanya kilicho kizuri na kinachofaa.
Kitendo: Watoto huiga wazazi wao kuliko mtu yeyote mwingine. Iwapo unagundua tabia zozote mbaya kwa mtoto wako, angalia iwapo mchumba wako ama wewe mmefanya hivyo mbele ya mtoto wako. Ulezi wa Kiislamu huegemeza ulezi kwa kuwa mfano. Fanya unacho kisema.
Kanuni ya 3: Mambo muhimu kuhusu ulezi wa Kiislamu ni huruma na ukarimu
Katika hadith inayo hadithiwa na `Aisha:
"Bedouin alikuja kwa nabii na kusema, “Nyinyi (watu) wabusu wavulana! Hatuwabusu.” Nabii alisema, “Siwezi weka fadhili kwenye mioyo yenu baada ya Allah kuiondoa.” [Sahih al-Bukhari]
Mapenzi ya kifizikia ni muhimu kwa kuwafanya watoto wahisi salama na wenye furaha. Usiwache mtoto wako anapo kua. Bila shaka, unaweza punguza mtoto wako anapo zeeka, ila usikome kufanya jambo hili.
Kitendo: Mtoto wako anapofanya makosa, badala ya kumkelelesha na kumlaumu, mkumbatie na umpapase kisha useme, 'Nimekusamehea. Tutafute suluhu ya jambo hili! Kisha, mwelezee kosa lake na umhimize arekebishe. Huenda ikawa ni kusema 'astaghfir-Allah' ama kuomba msamaha kwako ama kwa mtu mwingine. Kitu kingine cha muhimu kumfunza mtoto wako ni kuwa kitendo kizuri hufuta kitendo kibaya!
Kanuni ya 4: Mipaka ni muhimu
“Bila shaka Mwenyezi mkuu ameweka fara’id (matakwa ya kidini), kwa hivyo usiya puuze. Ameweka mipaka, kwa hivyo usiyatupilie mbali, na usiya kanyage sana. Amepiga marufuku baadhi ya mambo, kwa hivyo usiende kinyume yake; kuhusu baadhi ya mambo Alikuwa amenyamaza, kwa mapenzi, sio kusahau, kwa hivyo usiyafuate." [Hadith Nawawi]
Iwapo mtoto wako anafunzwa mapema tabia nzuri na mbaya, atafanya mambo iliyo kwenye mipaka na hatabaki akishangaa ama kushuku.
Kitendo: Weka masharti na kanuni kwa kila mwanafamilia hata wewe mwenyewe! Mwelezee mtoto wako kwanini wanapaswa kufuata kanuni hizo. Watoto wanapenda kujua maana ya kufanya vitu, ila, hakikisha kuwa unafanya hivi kwa njia rahisi kuelewa. Zawadi tabia nzuri ipasavyo na mara kwa mara.
Kanuni ya 5: Small responsibilities for the small shoulder to make it big!
"Nay na kwa mwezi, na kwa usiku inapo jitoa, na kwa kutwa kunapo angaa, bila shaka, ni mojawapo ya janga kubwa zaidi. Onyo kwa watu, kwa yeyote kati yenu anaye chagua kuenda mbele (kwa kufanya matendo ya kidini nzuri), ama kubaki nyuma (kwa kufanya dhambi), Kila mtu ana jukumu binafsi kwa matendo yake."[Qur’an: Chapter 74, Verses 32-38]
Kumpa mtoto wako majukumu mapema na katika umri unaofaa kunamsaidia kujua iwapo hafanyi kisicho faa kita muathiri yeye na kuwafanya wengine wahisi hawajafurahia. Pia kuna mtayarisha mtoto wakati ukifika awajibike ili awe amezoea.
Kitendo cha kufanya: Baadhi ya majukumu mepesi kama kumwuliza mtoto wako apeleke sahani yake jikoni ama kukusaidia kuweka chakula. Baadaye anapo endelea kukua, anaweza anza kuosha sahani yake ama kukusaidia kupanga vitu vya jikoni ulivyo nunua. Mwulize kijana wako kukusaidia jikoni na mapishi ama kuosha, kuweka vitu vyema kwenye nyumba na kuhakikisha nyumba ni safi.
Kanuni hizi za ulezi zina fanya utaratibu huu uwe rahisi zaidi. Je, ni kanuni ipi kati ya hizi unazo zingatia nyumbani mwako? Tujulishe kwa kuwacha ujumbe mfupi.
Kumbukumbu: ProductiveMuslim
Soma pia: Platonic parenting: The future trend for mum and dads?