Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Covid-19: Unyama Wa Polisi Washuhudiwa Siku Ya Kwanza Ya Kafyu Nchini Kenya

4masomo ya dakika
Covid-19: Unyama Wa Polisi Washuhudiwa Siku Ya Kwanza Ya Kafyu Nchini KenyaCovid-19: Unyama Wa Polisi Washuhudiwa Siku Ya Kwanza Ya Kafyu Nchini Kenya

Wakenya kutoka pande tofauti waungana mikono kukashifu unyama wa polisi Kenya ulio shuhudiwa leo kufuata amri za rais Uhuru Kenyatta aliye tangaza kafyu siku ya Jumatano. Kafyu hii hairuhusu watu kuwa nje kati ya masaa ya saa moja jioni hadi saa kumi na moja asubuhi. Isipokuwa makundi wa watu walio patiwa kibali cha kuwa nje, ikiwemo polisi, madaktari, wana habari na wanao uza kwenye maduka ya vyakula.

unyama wa polisi kenya

Vurugu huku unyama wa polisi ukishuhudiwa mijini tofauti Kenya

Siku ya kwanza ya kuanzishwa kwa kafyu hii ilikuwa na vurugu na misuko suko mingi. Idadi kubwa ya watu walionekana waki wakimbia polisi walio kuwa kwa idadi kubwa katika miji na mitaa yote nchini.

Mombasa mji wa raha ulikuwa na taharuki nyingi leo huku wananchi wakikimbizana na polisi. Idadi kubwa ya watu ilionekana ikiyakimbilia maisha yao baada ya polisi kuwarushia vitoa machozi na kupiga risasi nyingi hewani. Wazee kwa vijana, wake kwa waume wote walikimbia kuya nusuru maisha yao. Kanda na picha za unyama wa polisi Kenya zimejaa katika mitandao tofauti ya kijamii baada ya polisi hawa kuwaamrisha wananchi kulala chini huku wakiwachapa kwa kutumia fimbo na kuwarushia mateke. Huku wakisukumwa na kuamrishwa wakae chini wakiwa wamekaribiana. Bila kuzingatia umbali unao takikana kuzuia kuenea kwa virusi vya homa ya korona, jambo ambalo halikuzingatiwa katika kisa hiki. Wengi wakikashifu tendo hili kwani ni kuhatarisha maisha ya watu na kufanya iwe rahisi zaidi kueneza virusi vya covid-19.

The disruption in Likoni is a very predicted tactic used by gate-keepers of a police state – there is a dangerous lust to abuse and oppress with no desire to protect #Mombasa #CurfewinKenya pic.twitter.com/kc0UVLfW1V

— Suhayl (@suhayllo) March 27, 2020

Mwanahabari aliye chapwa na polisi

Kilicho wakera wananchi na wanahabari zaidi ni kanda iliyo onekana polisi mmoja akim nyanyasa mwanahabari Peter Wainaina wa chumba cha habari cha NTV. Cha kusikitisha zaidi ni kuwa masaa ya kafyu hayakuwa yameanza. Ilikuwa saa kumi na moja za jioni, lisaa limoja kabla ya kafyuu kuanza. “Nilikuwa katika shughuli za kuifanya kazi yangu na unyama nilio fanyiwa na mwana polisi ulinishika kwa mshangao kwani sikufanya chochote cha kumkasirisha na haikuwa sawa,” Wainaina aliwaambia wana habari wa Daily Nation. Chama cha wanahabari nchini kili kashifu tendo hili la unyama wa polisi Kenya na kutaka hatua kali zichukuliwe kwa polisi aliye mnyanyasa mwana habari huyu. Kumbuka kuwa wana habari ni miongoni mwa watu walio na kibali cha kuwa nje wakati wa kafyu.

Hali ilivyokuwa Nairobi

Katika mji mkuu wa nchi, kulikuwa na hali ya tatanishi huku watu wengi wakipiga foleni ndefu waki ngoja magari ya kwenda katika sehemu tofauti. Kupata magari kuliwa tatiza wengi kwani ma dereva wengi walifunga kazi mapema wakiepuka kupatwa nje masaa yasiyo kubalika. Kwa walio pata magari, nauli zilikuwa zimepanda sana kuwatatiza wengi kufika nyumbani. Kuna kisa ambapo dereva aliwaacha abiria kwenye gari la kwenye sehemu maarufu ya Utawala na kisha kupotea huku akiwaacha bila kujua la kufanya.

 

Covid-19: Unyama Wa Polisi Washuhudiwa Siku Ya Kwanza Ya Kafyu Nchini Kenya

Watu walio jeruhiwa walipelekwa hospitalini

Leo ikiwemo ni siku ya Ijumaa ambapo mji wa Nairobi unajulikana kuwa na uhai. Kwani watu wengi hukusanyika kutoka sehemu tofauti za nchi ili wajivinjari na kuirabisha wikendi, leo mambo yalikuwa tofauti. Ilipofika wakati wa saa moja za usiku, mji ulikuwa umetulia kama maji ya mtungi. Kwa sababu wana biashara wengi walikuwa wamefunga biashara zao na kuelekea manyumbani.

Katika mitaa kama Nyeri na Nakuru, watu walifuata kanuni zilizo wekwa na serikali na hakuna watu walio onekana waki randa randa katika wakati huu. Kwa madereva wa masafa marefu kama vile kutoka mji wa Nairobi kuwasafirisha watu hadi mji wa Mombasa, wali pumzika mahali ambapo walikuwa saa moja ikifika na kuahirisha safari yao hadi kesho asubuhi kutoka saa kumi na moja za asubuhi.

What Kenyans are going through is worst than Corona Virus 😭#PoliceBrutality#CurfewinKenya #COVID19KE pic.twitter.com/vGoEqOrEjO

— Mjengo Specialist (@ItsJoeKE) March 27, 2020

Maneno ya busara

Hii haikuwa siku ya kwanza iliyo tarajiwa na watu wengi. Ila tungependa kuwahimiza wananchi wa Kenya kujaribu juu chini na kuhakikisha kuwa wanazingatia amri za kafyu zilizo wekwa na serikali. Kupigana na janga la covid-19 ni mwito na juhudi za kila mmoja wetu. Tukizingatia maagizo haya, tutayarudia maisha yetu hivi karibuni. Hakikisha kuwa una jikarantini na kujitenga na watu iwapo una shuku una dalili za covid-19. Enda kwa hospitali iliyo karibu nawe na uripoti shaka zako ili vipimo vifaavyo vifanyike kuhakikisha iwapo una virusi hivi ama la.

Covid-19: Unyama Wa Polisi Washuhudiwa Siku Ya Kwanza Ya Kafyu Nchini Kenya

Kutoka Africaparent, tuna wahimiza wananchi wote kuzingatia usafi kwa kunawa mikono kila mara kwa kutumia vitakasio vyenye viwango vya kileo kinacho hitaji, ama kwa kutumia sabuni na maji safi. Hakikisha unapo kohoa ama kuchemua, unatumia sehemu ya ndani ya kiwiko chako, na kuepuka kuwa miongoni mwa watu wengi na kuzingatia umbali wa mita moja unusu.

Wasiliana na wizara ya afya nchini kuhusu virusi vya covid-19 kwa kupiga nambari hizi za dharura 0800721316 (bila malipo), 0729 471 414, 0732 353 535.

Chanzo: Standard media

img
Yaliandikwa na

Risper Nyakio

  • Nyumbani
  • /
  • News
  • /
  • Covid-19: Unyama Wa Polisi Washuhudiwa Siku Ya Kwanza Ya Kafyu Nchini Kenya
Gawa:
  • Covid-19: Watu Wawili Wauliwa Rwanda Baada Ya Kukiuka Maagizo Ya Kukaa Nyumbani

    Covid-19: Watu Wawili Wauliwa Rwanda Baada Ya Kukiuka Maagizo Ya Kukaa Nyumbani

  • Kafyu Nchini Kenya Kutekelezwa Kufuatia Visa Vyingi Vya Homa Ya Korona

    Kafyu Nchini Kenya Kutekelezwa Kufuatia Visa Vyingi Vya Homa Ya Korona

  • Covid 19: Orodha Ya Watu Wanao Kubalika Kuwa Nje Wakati Wa Kafyu

    Covid 19: Orodha Ya Watu Wanao Kubalika Kuwa Nje Wakati Wa Kafyu

  • Kisa Cha Kwanza Cha Kupona Kwa Mgonjwa wa Covid-19 Nchini Kenya

    Kisa Cha Kwanza Cha Kupona Kwa Mgonjwa wa Covid-19 Nchini Kenya

  • Covid-19: Watu Wawili Wauliwa Rwanda Baada Ya Kukiuka Maagizo Ya Kukaa Nyumbani

    Covid-19: Watu Wawili Wauliwa Rwanda Baada Ya Kukiuka Maagizo Ya Kukaa Nyumbani

  • Kafyu Nchini Kenya Kutekelezwa Kufuatia Visa Vyingi Vya Homa Ya Korona

    Kafyu Nchini Kenya Kutekelezwa Kufuatia Visa Vyingi Vya Homa Ya Korona

  • Covid 19: Orodha Ya Watu Wanao Kubalika Kuwa Nje Wakati Wa Kafyu

    Covid 19: Orodha Ya Watu Wanao Kubalika Kuwa Nje Wakati Wa Kafyu

  • Kisa Cha Kwanza Cha Kupona Kwa Mgonjwa wa Covid-19 Nchini Kenya

    Kisa Cha Kwanza Cha Kupona Kwa Mgonjwa wa Covid-19 Nchini Kenya

Pata ushauri wa mara kwa mara kuhusu ujauzito wako na mtoto wako anayekua!
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • Zaidi
    • TAP Jamii
    • Tangaza Nasi
    • Wasiliana Nasi
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
Kutuhusu|Timu|Sera ya Faragha|Masharti ya kutumia |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it