Mwanamke yeyote aliyepoteza mimba anafahamu kuwa kuharibika kwa mimba ni jambo linalo wafilisisha haijalishi umri wa mimba kabla ya kuharibika kwake. Hasa kama alikuwa amepanga ujauzito na alikuwa anatarajia kuitwa mama kwa sana. Kupona baada ya kupoteza mimba sio jambo rahisi. Mama, usiyafanye haya baada ya kupoteza mimba.
Usifanye mambo haya baada ya kupoteza mimba

Baada ya kupoteza mimba, utahisi kana kwamba wewe pekee ndiye uliyepoteza mimba na hakuna mtu anayeelewa unachokipitia. Usihisi hivi.
Ukweli ni kuwa, kupoteza mimba hufanyika kwa sana. Kupoteza mimba kabla ya kujifungua pia hufanyika na ni maarufu kuliko watu wanavyojua. Hatari ni kuwa, watu hawazungumzii vya kutosha jambo hili. Ikiwa ungependa watu wajue unachokipitia ama ungependa kupona kwa usiri wako, usihisi kana kwamba uko peke yako.
Ni vigumu kutohisi kana kwamba haukufanya jambo lililosababisha tokeo la kupoteza mimba. Kuhisi hatia jambo mbaya linapofanyikia mtu aliye muhimu kwetu, na hakuna mtu muhimu kwa mama kuliko mwanawe. Kuna njia za kukusaidia kutohisi hatia baada ya kupoteza mimba.
Safari ya kila mtu ya majonzi huwa tofauti. Wengine wanataka kuwajulisha watu wanachokipitia na kusaidiwa kuegemezwa kihisia na marafiki zao, wakati ambapo wengine wanapenda kunyamaza na kuwajuza watu wachache wanao waamini.
Kupoteza ujauzito ni jambo ambalo kama jamii, hatuzungumzii vya kutosha. Kwa hivyo, mama anaposema kuwa amepoteza mimba, watu wengi hawajui jinsi ya kumpa faraja. Na hivyo basi, huenda wakajipata wakisema maneno yanayo mwumiza mama.

Hata kama hutaki kumwambia kila mtu kilicho tendeka na unachokipitia, kuzungumza na watu wachache kutasaidia kupunguza mzigo wa unayopitia. Pia, unapowajulisha marafiki wa karibu na familia kilichokutendekea, watajua jinsi ya kuwa wanapokuwa karibu nawe.
- Kupuuza mahitaji yako ya kihisia
Kuziba hisia na kuendelea na maisha yako kana kwamba hakuna kitu kilichofanyika kutakuwa na athari hasi zaidi. Ni muhimu kwa mama kujipa wakati wa kuomboleza na kukubali kilichofanyika. Kubeba kila kitu moyoni kana kwamba hakuna kitu kisichokuwa sawa kutakuathiri baadaye. Ikiwezekana, chukua wiki chache ubadili mazingira yako ili uweze kupona.
- Kuepuka msaada wa kitaalum
Umejipatia wakati mwingi na subira. Umekuwa na siku nzuri baada ya kupoteza mimba na siku sawa ama zaidi ambazo hazikuwa sawa. Katika siku mbaya, ni vigumu kutoka kitandani. Hauna nishati ya kufanya kitu chochote, hata vitu ambavyo ulivipendelea hapo mbeleni. Hauna hamu ya kula ama kunywa ama kuwasiliana na watu. Ikiwa unahisi hivi, ni wakati wa kupata usaidizi wa kitaalum.
Usiyafanye haya baada ya kupoteza mimba huku ukiendelea kupona. Mpigie daktari wako mzungumze naye.
Chanzo: WebMD
Soma Pia: Maambukizi 10 Yanayo Sababisha Mama Mjamzito Kupoteza Mimba