Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Jinsi ya Kuboresha Uzalishaji Katika Wanaume na Kupunguza Utasa wa Kiume

2 min read
Jinsi ya Kuboresha Uzalishaji Katika Wanaume na Kupunguza Utasa wa KiumeJinsi ya Kuboresha Uzalishaji Katika Wanaume na Kupunguza Utasa wa Kiume

Utasa wa kiume ni pale ambapo mwanamme hana uwezo wa kumpa mwanamke ujauzito. Mara nyingi huathiriwa na ubora wa seli zake za manii.

Ikiwa wanandoa wanapatana na changamoto za uzalishaji, ni vyema kukumbuka kuwa hawako peke yao, mbali kuna wanandoa wengine wengi wanaokumbana na changamoto sawa. Utasa ni kawaida zaidi kuliko unavyodhania.

Moja kati ya wanandoa sita hutatizika na changamoto hii na utafiti unadhihirisha kuwa moja kati ya visa vitatu huwa kufuatia matatizo ya utasa katika wachumba wa kiume. Wakati ambapo utasa hauna tiba wakati mwingi, kuna baadhi ya vitu ambavyo unaweza fanya kuboresha nafasi zako za kutunga mimba. Uzalishaji unaweza kuboreshwa kutumia lishe bora na kuimarisha mitindo ya maisha.

Utasa wa kiume

utasa wa kiume

Uzalishaji ni uwezo wa mwanamme kumpa mwanamke mimba.

Utasa wa kiume ni pale ambapo mwanamme hana uwezo wa kumpa mwanamke ujauzito. Mara nyingi huathiriwa na ubora wa seli zake za manii. Utasa unahusishwa na utendaji wa kingono ama ubora wa manii.

  • Hamu ya kufanya ngono. Matamanio ya mtu kufanya mapenzi
  • Idadi ya manii. Nambari ya maii bora ama kukolea kwa seli za manii
  • Mwendo wa manii. Uwezo wa manii kuogelea
  • Viwango vya testosterone. Kichocheo cha kiume cha ngongo kinauwezo wa kuathiri utasa

Mara nyingi, utasa huwa na vyanzo vingi na huweza kuathiriwa na geni, afya kwa ujumla, magonjwa, na lishe. Mtindo wa maisha wenye afya ni muhimu. Baadhi ya vyakula huwa na manufaa ya uzalishaji vikilinganishwa na vingine.

Baadhi ya njia za kuboresha kiwango cha manii na kuimarisha uzalishaji katika wanaume.

Fanya mazoezi mara kwa mara

Mazoezi yana manufaa mengi, na mbali na kuboresha afya yako, yanasaidia kuimarisha viwango vya vichocheo vya ngono( testosterone) na kuboresha uwezo wa uzalishaji. Kulingana na utafiti, wanaume wanaofanya mazoezi mara kwa mara huwa na viwango vya juu zaidi vya kichocheo cha ngono ikilinganishwa na wasio fanya mazoezi.

Pata vitamin C tosha

Vitamin C ina uwezo wa kuboresha kinga mwilini. Inasaidia pia katika kuimarisha uzalishaji katika wanaume. Vitamin C pia huimarisha kiwango cha manii na mwendo wake huku ikipunguza seli za manii zilizo haribika.

utasa wa kiume

Pumzika na upunguze mawazo mengi

Mawazo mengi huathiri uwezo wa mwanamme kufanya mapenzi na kutosheleka. Na hivi kuathiri uzalishaji wa mwanamke. Mwanamme anapokuwa na mawazo mengi, anaweza kufanya mazoezi, kutembea ama kuzungumza na watu.

Pata vitamini D tosha

Vitamini D ni muhimu kwa uzalishaji wa kiume na kike. Ina boresha viwango vya kichocheo cha testosterone. Kulingana na utafiti, wanaume wasiokuwa na viwango tosha vya vitamini huwa na viwango vya chini vya testosterone.

Chanzo: WebMD

Soma Pia: Vyakula 8 Vinavyo Ua Manii Ambavyo Wanaume Wanapaswa Kujitenga Navyo!

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Health
  • /
  • Jinsi ya Kuboresha Uzalishaji Katika Wanaume na Kupunguza Utasa wa Kiume
Share:
  • Je, Kiamsha Kinywa Kina Manufaa Mwilini?

    Je, Kiamsha Kinywa Kina Manufaa Mwilini?

  • Vyanzo 5 vya Kuhisi Uvimbe na Maumivu ya Tumbo

    Vyanzo 5 vya Kuhisi Uvimbe na Maumivu ya Tumbo

  • Dalili za Ugumba Kwa Wanaume na Jinsi ya Kujikinga Dhidi ya Hali Hii

    Dalili za Ugumba Kwa Wanaume na Jinsi ya Kujikinga Dhidi ya Hali Hii

  • Je, Kiamsha Kinywa Kina Manufaa Mwilini?

    Je, Kiamsha Kinywa Kina Manufaa Mwilini?

  • Vyanzo 5 vya Kuhisi Uvimbe na Maumivu ya Tumbo

    Vyanzo 5 vya Kuhisi Uvimbe na Maumivu ya Tumbo

  • Dalili za Ugumba Kwa Wanaume na Jinsi ya Kujikinga Dhidi ya Hali Hii

    Dalili za Ugumba Kwa Wanaume na Jinsi ya Kujikinga Dhidi ya Hali Hii

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it