Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Vitu Ambavyo Wanaume Hufanya Vinavyoharibu Uhusiano kwa Urahisi

2 min read
Vitu Ambavyo Wanaume Hufanya Vinavyoharibu Uhusiano kwa UrahisiVitu Ambavyo Wanaume Hufanya Vinavyoharibu Uhusiano kwa Urahisi

Baadhi ya vitu vinavyoharibu uhusiano ambavyo wanaume hufanya ni kama vile kudanganya, kuvunja imani na kutomuelewa mpenzi wake.

Kuelewa vitu ambavyo wanaume hufanya vinavyoharibu uhusiano kutawasaidia kujitenga navyo na kuwa na mahusiano bora zaidi. Tazama baadhi ya vitu maarufu wanavyovifanya visivyofaa na kuathiri mahusiano yao.

1.Kudanganya

vitu vinavyoharibu uhusiano

Jambo moja ambalo wanaume wengi hufanya kwa ustadi ni kudanganya. Hata kama kutasaidia kutoka kwa tatizo kwa dakika chache, kudanganya huharibu imani kati ya wachumba. Tabia huchangia pakubwa katika kutengana kwa wachumba wengi. Wanaume wanaodanganya wanaongeza nafasi za kuharibu uhusiano wao kwa kasi.

2. Kuvunja imani

Imani ni muhimu katika uhusiano wowote ule. Mwanamke unayempenda atakuamini katika mambo mengi, ila, unapovunja imani yake, ni vigumu kwake kukuamini tena katika lolote lile. Imani inapoisha katika uhusiano, uhusiano huisha.

3. Kutomuelewa mpenzi wako

vitu vinavyoharibu uhusiano

Kutochukua muda kumuelewa mchumba ni ishara dhahiri kuwa hujali kuhusu hisia ama maisha yake. Ikiwa unampenda mpenzi wako, chukua muda kuelewa vitu anavyopenda na asivyopenda. Sio vigumu kumuelewa mtu. Unapotatizika kuelewa kitu chochote anachofanya, mkalishe chini umwulize kinachoendelea.

4. Kutomzawadi mpenzi wako

Kosa kubwa kuliko kumpa mpenzi wako zawadi ni kumpa zawadi asiyotaka. Machoni mwa mwanamke, mwanamme anapaswa kufahamu zawadi bora ya kumpa. Zungumza na mpenzi wako ufahamu anachotaka. Kwa njia hii, utakuwa na maoni ya zawadi ambazo anaweza furahia katika siku zake spesheli.

5. Kutozungumza vya kutosha naye

Kuzungumza kunaweza kuwa vigumu kwa wanaume na rahisi sana kwa wanawake. Lakini mazungumzo ni muhimu katika kudumisha uhusiano hasa wa kimapenzi. Usipozungumza na mpenzi wako, ataona kana kwamba una watu wengine unaozungumza nao ama hutaki kujua kinachoendelea maishani mwake. Chukua muda kila siku kumpigia mpenzi wako simu kujua kinachoendelea.

6. Kumfanya akose kuhisi salama

vitu vinavyoharibu uhusiano

Mwanamke kuhisi kuwa ako salama na mpenzi wake ni muhimu ili uhusiano kustawi. Mwanamke anapohisi ako salama, itakuwa rahisi kwake kumwamini mchumba wake na kumweleza kinachomsumbua. Mazungumzo hupungua na mwishowe mapenzi kudidimia. Mwanamme asipompatia mwanamke nafasi ya kuhisi salama ni chanzo cha uhusiano kuisha.

7. Kutotimiza ahadi zako

Mwanamme anayetimizia ahadi yake huaminika na mpenzi wake. Kutotimiza ahadi zako kwake huwa ishara kuwa hujali kuhusu hisia zake. Kuwa neno lako haliwezi kuaminika na kumfanya mara nyingi kushuku unachomwambia.

Vitu vinavyoharibu uhusiano ambavyo wanaume hufanya ni kama kudanganya, kuvunja imani, kutomuelewa mpenzi wake, tukozungumza vya kutosha na mpenzi wake, kukosa kumfanya kuhisi salama na kutotimiza ahadi.

Soma Pia: Je, Nitaweza kubaini vipi kati ya Mapenzi Bandia na ya Kweli

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Relationship & Sex
  • /
  • Vitu Ambavyo Wanaume Hufanya Vinavyoharibu Uhusiano kwa Urahisi
Share:
  • Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

    Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

  • Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

    Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

  • Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

    Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

  • Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

    Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

  • Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

    Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

  • Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

    Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it