Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Vitu 5 Visivyofaa Kuwa Chumbani cha Kulala

2 min read
Vitu 5 Visivyofaa Kuwa Chumbani cha KulalaVitu 5 Visivyofaa Kuwa Chumbani cha Kulala

Vitu visivyofaa kuwa chumbani cha kulala kama vile dawati ya kazi, simu na runinga huathiri ratiba yako ya kulala.

Chumba cha kulala kinapaswa kuwa mahali pa kupumzika baada ya kuwa na siku ndefu na kupata usingizi wa kuupumzisha mwili. Kuwa na vitu visivyofaa kuwa kwenye chumba hiki hufanya iwe vigumu kupata usingizi wa kutosha ama kuzingatia ratiba ya kulala. Tazama orodha ya vitu visivyofaa kuwa chumbani cha kulala

Vitu visivyofaa kuwa chumbani cha kulala

  1. Runinga/Televisheni

vitu visivyofaa kuwa chumbani cha kulala

Mwangaza wa buluu unaotoka kwenye runinga huharibu mfumo wa kulala. Kutazama runinga dakika chache kabla ya kulala hufanya iwe vigumu kupata usingizi. Pia, kuna jaribio la kuendelea kutazama runinga kwa muda zaidi. Kuweka runinga kwenye chumba cha kulala kuna athiri kwa njia hasi lengo la chumba kile.

2. Simu

vitu visivyofaa kuwa chumbani cha kulala

Wataalum wa afya wanashauri kutotumia simu dakika chache kabla ya kulala. Kuwa na simu chumbani cha kulala huingilia mchakato wa kulala. Simu inapolia inaathiri usingizi wako unapoamka kuipokea ama kuizima. Mbali na hayo, kuna jaribio la kutumia simu kuangalia kinachoendela kwenye mitandao ya kijamii. Kutumia simu usiku kunakuweka katika hatari ya kuitumia kwa muda zaidi badala ya kupata usingizi.

3. Chakula

vitu visivyofaa kuwa chumbani cha kulala

Haupaswi kula ukiwa chumbani cha kulala kisha kutazama runinga ama kutumia simu. Mabaki ya chakula huchafua kitanda na hakuna anayepata usingizi mzuri kwa chumba kichafu. Unapojipata ukikula chakula chumbani cha kulala, hakikisha kuwa unaondoa vyombo vichafu.

4. Vifaa vya mazoezi

Kuweka vifaa vya mazoezi hujaza nafasi kwenye chumba cha kulala. Vyumba vilivyo na nafasi ndogo huonekana kujaa, na kana kwamba hewa tosha haifiki. Pia, chumba kinaonekana hakina usafi. Epuka kufanya mazoezi kwenye chumba cha kulala.

5. Dawati ya kufanya kazi

vitu visivyofaa kuwa chumbani cha kulala

Kutofautisha kati ya wakati wa kupumzika na wa kufanya kazi ni muhimu. Hata kama unafanyia kazi nyumbani, sio jambo la busara kufanyia kazi kwenye chumba cha kulala. Kwani mara nyingi huenda ukapata unafanya kazi zaidi badala ya kulala ama kulala zaidi baada ya kufanya kazi. Badala yake, weka dawati lako sebuleni.

Soma Pia: Mazungumzo 5 Muhimu Kabla ya Kufunga Ndoa Kati ya Wachumba

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Lifestyle
  • /
  • Vitu 5 Visivyofaa Kuwa Chumbani cha Kulala
Share:
  • Sababu 7 Kwa Nini Watu Wanaogopa Ndoa Siku Hizi

    Sababu 7 Kwa Nini Watu Wanaogopa Ndoa Siku Hizi

  • Zari Hassan Amewasili Nchini Kenya Ambapo Anavumbua Nyumba Mpya

    Zari Hassan Amewasili Nchini Kenya Ambapo Anavumbua Nyumba Mpya

  • Lori Harvey na Michael B. Jordan Wametengana Baada ya Kuwa Pamoja Kwa Mwaka Mmoja

    Lori Harvey na Michael B. Jordan Wametengana Baada ya Kuwa Pamoja Kwa Mwaka Mmoja

  • Sababu 7 Kwa Nini Watu Wanaogopa Ndoa Siku Hizi

    Sababu 7 Kwa Nini Watu Wanaogopa Ndoa Siku Hizi

  • Zari Hassan Amewasili Nchini Kenya Ambapo Anavumbua Nyumba Mpya

    Zari Hassan Amewasili Nchini Kenya Ambapo Anavumbua Nyumba Mpya

  • Lori Harvey na Michael B. Jordan Wametengana Baada ya Kuwa Pamoja Kwa Mwaka Mmoja

    Lori Harvey na Michael B. Jordan Wametengana Baada ya Kuwa Pamoja Kwa Mwaka Mmoja

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2022 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it