Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Vyakula 5 Hatari Zaidi Kwa Mama Mjamzito!

3 min read
Vyakula 5 Hatari Zaidi Kwa Mama Mjamzito!Vyakula 5 Hatari Zaidi Kwa Mama Mjamzito!

Mayai mbichi huwa na viini vya Salmonella. Inayosababisha ishara kama maumivu ya tumbo, kuharisha, kutapika na joto jingi. Mama mjamzito anapaswa kula mayai yaliyoiva vizuri.

Kitu cha kwanza ambacho wanawake wenye mimba hujuzwa wanapotunga mimba ni vyakula hatari kwa mama mjamzito. Sio rahisi kuwacha vyakula ulivyokuwa umezoea hapo awali kama kula sushi ama kunywa vikombe viwili vya kahawa kila siku. Hata hivyo, sio jambo la kutia wasiwasi kwani kuna vyakula vingi ambavyo mama mjamzito anaweza kukula. Tuna orodhesha baadhi ya vyakula ambavyo mama mjamzito hapaswi kula.

Vyakula Hatari Kwa Mama Mjamzito

  1. Samaki mbichi

vyakula hatari kwa mama mjamzito

Wanawake waliozoea kula chakula kilicho na samaki mbichi kama sushi ama samaki ambaye hajapikwa vizuri. Vyakula hivi vinamweka mama katika hatari ya kupata maambukizi ya viini na mengineyo kama Listeria, Vibrio, na Salmonella. Maambukizi haya yanamfanya mama akose maji tosha mwilini na kumfanya akose nishati mwilini. Katika visa hatari, huenda mtoto akapata viini hivi na kusababisha kifo chake. Bakteria hizi zinapatikana kwenye samaki mbichi, na maji na mimea iliyo ambukizwa. Ni muhimu kwa mama kujitenga na vyakula hivi anapokuwa na mimba.

2. Samaki wenye viwango vya juu vya zebaki

Zebaki ni hatari, na viwango vya juu husababisha matatizo kwenye mfumo wa neva, kinga na figo. Inapopita amniotic fluid na kumfikia mtoto, inasababisha matatizo ya ukuaji. Samaki wenye viwango vya juu vya zebaki ni kama vile tuna, shark, marlin na swordfish. Samaki bora katika mimba ni kama salmon, tilapia, haddock, trout na cod.

3. Nyama mbichi

Kula nyama mbichi ama ambayo haijaiva vizuri inahatarisha afya ya mama mjamzito. Inamweka katika hatari ya kupata maambukizi ya viini kama Salmonella na E. coli. Na kumweka mtoto katika hatari ya kupoteza maisha yake, kupoteza uwezo wa kuona, kukosa maarifa na kuwa epileptic. Mama mjamzito anapaswa kula nyama iliyopikwa vizuri na ikiwezekana kula chakula alichokitayarisha mwenyewe ama anachofahamu kilivyo tayarishwa.

4. Mayai mbichi

vyakula hatari kwa mama mjamzito

Mayai mbichi huwa na viini vya Salmonella. Inayosababisha ishara kama maumivu ya tumbo, kuharisha, kutapika na joto jingi. Inapomfikia mtoto, huenda ikasababisha kujifungua mtoto aliyefariki ama kujifungua kabla ya wakati. Mama mwenye mimba anastahili kuhakikisha kuwa chakula chake kina mayai yaliyoiva na kujitenga na vyakula vilivyo na mayai mbichi kama mayonnaise.

5. Pombe

Kunywa vileo katika mimba kunaongeza hatari ya kupoteza mimba ama kujifungua mtoto aliyeaga dunia. Mtoto aliyezaliwa na mama aliyekuwa anatumia pombe katika mimba huenda akawa na matatizo ya kimaumbile, matatizo ya moyo na kutatizika kiakili.

Mbali na vyakula hatari kwa mama mjamzito tulivyoangazia, mama mwenye mimba anapaswa kuepuka utumiaji wa kaffeini nyingi, vitamutamu vya kuchakatwa, na kuhakikisha kuwa anakula mboga na matunda yaliyosafishwa vizuri.

Soma Pia: Chakula Bora Katika Mimba: Vyakula Muhimu Kwa Mama Anapokuwa Mjamzito

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Pregnancy
  • /
  • Vyakula 5 Hatari Zaidi Kwa Mama Mjamzito!
Share:
  • Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

    Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

  • Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

    Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

  • Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

    Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

  • Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

    Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

  • Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

    Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

  • Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

    Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it