Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Vyakula 7 Hatari Kwa Afya ya Mjamzito

2 min read
Vyakula 7 Hatari Kwa Afya ya MjamzitoVyakula 7 Hatari Kwa Afya ya Mjamzito

Orodha ya vyakula hatari kwa mjamzito inamwelemisha mama kuhusu madhara ya kuchukua vyakula fulani kwa afya yake na ya mtoto.

Katika ujauzito, chakula cha mama hupita kwa mtoto pia. Vyakula ambavyo huenda vikakosa kuwa na athari hasi kwa mama huenda vikamwathiri mtoto. Orodha hii ya vyakula hatari kwa mjamzito inamwelemisha mama kuhusu madhara ya kuchukua vyakula fulani kwa afya yake na ya mtoto.

Vyakula Hatari Kwa Mjamzito

1.Chakula cha baharini chenye zebaki ya juu

seafood, vyakula hatari kwa mjamzito

Chakula cha baharini ni chanzo bora cha protini na omega-3 ambazo huhimiza ukuaji wa ubongo na macho ya mtoto. Hata hivyo, vyakula vya baharini vyenye viwango vya juu vya zebaki huwa hatari kwa mfumo wa neva wa mtoto unaokua. Kama shark, swordfish, marlin, king mackerel na tilefish.

2. Chakula ambacho hakijapikika

Katika mimba, mjamzito huwa katika hatari kubwa ya kupata sumu kupitia chakula. Ili kujitenga dhidi ya magonjwa haya, ni muhimu kuhakikisha kuwa nyama imepikika vyakula, kuepuka chakula kilichoweka kwenye jokofu kwa muda mrefu. Kupika mayai mpaka yaive vizuri.

3. Safisha matunda na mboga vizuri

Ili kutoa bakteria mbaya, safisha matunda na mboga vyema. Epuka kula sprouts mbichi na papai mbichi kwani zina bakteria zinazosababisha maradhi.

4. Kaffeini nyingi

vyakula hatari kwa mjamzito

Kaffeini hupita kwenye placenta na kumfikia mtoto. Ili kuwa salama, mjamzito anashauriwa kupunguza kiwango cha kaffeini na bidhaa za kaffeini anazochukua. Kisha kuwachana na unywaji wake kwa pamoja.

5. Mayai mbichi

Mayai mbichi pamoja na bidhaa zenye mayai mbichi. Kama vile mayonnaise na custards kwani zinamweka mama mjamzito katika hatari ya kupata salmonella.

6. Epuka pombe

Hakuna kiwango cha pombe kilicho salama katika mimba. Njia salama ni kuepuka unywaji wowote wa pombe. Wajawazito wanaochukua pombe huwa katika hatari ya kupoteza mimba ama kujifungua watoto wenye matatizo ya kimaumbile.

7. Chai ya mitishamba

Hata ingawa hakuna utafiti dhabiti unaoonyesha athari za chai ya mitishamba kwenye mtoto anayekua. Chai za mitishamba zinapaswa kuchukuliwa daktari anapompa mama kibali.

Chochote mama anachotia mdomoni katika mimba kinamfikia mtoto. Ni muhimu kuwa makini na lishe na kuhakikisha kuwa ni ya afya na salama kwa mama na mtoto.

Chanzo: Healthline

Soma Pia: Vidokezo 7 Vya Kuwa na Mimba Salama na Yenye Afya

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Pregnancy
  • /
  • Vyakula 7 Hatari Kwa Afya ya Mjamzito
Share:
  • Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

    Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

  • Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

    Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

  • Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

    Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

  • Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

    Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

  • Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

    Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

  • Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

    Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it