Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Vyakula 5 Bora Vya Kuleta Usingizi Kwa Wanaotatizika Na Insomnia

3 min read
Vyakula 5 Bora Vya Kuleta Usingizi Kwa Wanaotatizika Na InsomniaVyakula 5 Bora Vya Kuleta Usingizi Kwa Wanaotatizika Na Insomnia

Usingizi ni muhimu katika utendaji kazi wa kawaida wa mwili. Kwa wanaotatizika kulala, vyakula hivi vya kuleta usingizi vitasaidia.

Kulala kwa masaa machache na kufanya kazi kwa masaa zaidi kunasifika na kuonekana kama jambo la kutiliwa maanani. Wanaofanya hivi wanaonekana shupavu na watu wa kuigwa katika jamii. Ila katika masomo ya kliniki, hili ni jambo hasi linalopaswa kukemewa. Kutopata usingizi tosha wa masaa manane kwa siku ni hatari kwa afya na mwili. Kabla ya kuchukua tembe za kuratibisha mfumo wako wa usingizi, kuna mengi unayoweza kufanya nyumbani, kama ulaji wa vyakula vya kuleta usingizi.

Athari hasi za kutopata usingizi tosha

vyakula vya kuleta usingizi

Kutolala vyema usiku na kuupa mwili wakati tosha wa kupona baada ya siku nzima ya kufanya kazi na shughuli tofauti huwa na athari hasi. Mwili huathiriwa kwa njia zifuatazo:

  • Kuathiri ongezeko kubwa la uzani wa mwili
  • Kusababisha kisukari
  • Kulegea kazini
  • Kukosa umakini masomoni na kazini

Vyakula vya kuleta usingizi

  1. Maziwa yenye joto

vyakula vya kuleta usingizi

Kunywa maziwa yenye joto muda kabla ya kulala kumedhihirishwa kuwa na athari chanya katika kusaidia kupata usingizi. Maziwa huwa na misombo inayoboresha kupata usingizi, kama vile: kalisi, tryptophan, melatonin na vitamini D. Kunywa maziwa kabla ya kulala husaidia kupumzisha mwili na kulala vyema zaidi.

2. Almonds

vyakula vya kuleta usingizi

Almonds zimedhihirishwa kuwa na kiwango kikubwa cha kichocheo cha melatonin kinachosaidia kudhibiti mfumo wa kulala. Almonds zina kalisi na magnesiumu zinazosaidia kuboresha kulala vyema zaidi usiku. Almonds zina afya kwani zina wingi wa ufuta mzuri na kiwango cha chini cha sukari.

3. Chai ya chamomile

vyakula vya kuleta usingizi

Hapo zamani, mmea wa chamomile ulitumika kuponya kutopata usingizi usiku. Msimbo wa apigenin unaopatikana kwenye mmea huu unasaidia kuleta usingizi. Kunywa kikombe kimoja cha chai ya chamomile kabla ya kulala kunasaidia kulala vyema zaidi.

4. Samaki 

vyakula vya kuleta usingizi

Samaki ni chanzo kizuri cha vitamini D na pia ina omega-3 fatty acids zote ambazo zinasaidia kuboresha usingizi. Msimbo wa serotonin unaopatikana kwenye samaki unasaidia kutengeneza mfumo bora wa kulala na kuamka. Kula samaki kama vile salmon kwa wiki moja kuna athari chanya kwenye mfumo wa kulala.

5. Viazi vitamu 

vyakula vya kuleta usingizi

Viazi vitamu vya kuoka vina potassium, kalisi na magnesiamu. Zote ambazo zinasaidia kupumzika. Kula kipande cha kiazi kitamu kabla ya kulala kunasaidia kupumzisha mwili na kuwezesha kulala vyema usiku.

Mbali na kula vyakula hivi, ni vyema kufanya haya:

  • Kufanya mazoezi mara kwa mara
  • Kujitenga na ulaji wa chakula chenye sukari nyingi muda mfupi kabla ya kulala
  • Kuepuka ulaji wa chakula kingi hasa chenye wanga dakika chache kabla ya kulala
  • Kunywa maji tosha kwa siku, glasi nane ni bora
  • Kujipa masaa mawili ama matatu kabla ya kulala baada ya kula chajio
  • Kuepuka unywaji wa vileo kabla ya kulala

Soma Pia: Usingizi Wa Mtoto: Mambo Ya Kufanya Na Kuto Fanya

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Health
  • /
  • Vyakula 5 Bora Vya Kuleta Usingizi Kwa Wanaotatizika Na Insomnia
Share:
  • Je, Kiamsha Kinywa Kina Manufaa Mwilini?

    Je, Kiamsha Kinywa Kina Manufaa Mwilini?

  • Vyanzo 5 vya Kuhisi Uvimbe na Maumivu ya Tumbo

    Vyanzo 5 vya Kuhisi Uvimbe na Maumivu ya Tumbo

  • Dalili za Ugumba Kwa Wanaume na Jinsi ya Kujikinga Dhidi ya Hali Hii

    Dalili za Ugumba Kwa Wanaume na Jinsi ya Kujikinga Dhidi ya Hali Hii

  • Je, Kiamsha Kinywa Kina Manufaa Mwilini?

    Je, Kiamsha Kinywa Kina Manufaa Mwilini?

  • Vyanzo 5 vya Kuhisi Uvimbe na Maumivu ya Tumbo

    Vyanzo 5 vya Kuhisi Uvimbe na Maumivu ya Tumbo

  • Dalili za Ugumba Kwa Wanaume na Jinsi ya Kujikinga Dhidi ya Hali Hii

    Dalili za Ugumba Kwa Wanaume na Jinsi ya Kujikinga Dhidi ya Hali Hii

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it