Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Kukosa Usingizi Usiku: Vyanzo Na Matibabu Ya Suala Hili

3 min read
Kukosa Usingizi Usiku: Vyanzo Na Matibabu Ya Suala HiliKukosa Usingizi Usiku: Vyanzo Na Matibabu Ya Suala Hili

Kushindwa kulala kwa muda mfupi hudumu kwa kipindi cha usiku mmoja ama wiki chache. Huku kutatizika kulala kwa muda mrefu kukiwa kwa zaidi ya wiki tatu.

Insomnia ni nini? Kukosa usingizi usiku ni hali ambapo mtu hutatizika kulala anavyopaswa usiku, kulala kwa masaa machache ama kugutuka akiwa usingizini kisha kushindwa kulala tena.

Hali hii inaweza kuwa tatizo la muda mfupi (acute) ama muda mrefu (chronic). Kushindwa kulala kwa muda mfupi hudumu kwa kipindi cha usiku mmoja ama wiki chache. Huku kutatizika kulala kwa muda mrefu kukiwa kwa zaidi ya wiki tatu.

Aina za insomnia ama kukosa usingizi

kukosa usingizi

Kukosa usingizi kwa kimsingi. Matatizo ya kulala hayahusishwi na matatizo mengine ya kiafya.

Kukosa usingizi kwa sekondari. Matatizo ya kiafya husababisha kukosa usingizi. Matatizo kama kusombwa na mawazo, saratani, kiungulia, uchungu, dawa, dawa za kulevya na vileo.

Vyanzo vya kutopata usingizi

Vyanzo vya kimsingi:

Mawazo mengi ya kimaisha. Kama vile kuwa na tukio kubwa siku chache zijazo, kufiwa na mwanafamilia ama rafiki, kusafiri ama kuwachwa na mchumba

Mazingara. Kuwa katika mazingira yenye kelele nyingi, temprecha ya juu ama mwangaza mwingi usiku

Kubadilisha ratiba ya kulala. Kuanza kufanya kazi usiku ama kutazama runinga usiku kunaweza athiri usingizi na kusababisha kukosa kulala usiku

Vyanzo vya kisekondari

  • Dawa za hali za kiafya kama homa, mzio, shinikizo la damu
  • Uchungu mwingi usiku
  • Kutumia vitu kama kaffeini, pombe na dawa za kulevya
  • Ujauzito husababisha kutopata usingizi usiku
  • Uchungu na mabadiliko ya mwili kabla ya kipindi cha hedhi
  • Kufika umri wa kutojifungua

Hatari za kukosa usingizi

kukosa usingizi

Wanawake wengi hutatizika na hali ya kutopata usingizi ikilinganishwa na wanaume. Pia, watu wenye umri zaidi hutatizika na hali hii ikilinganishwa na watu wachanga. Kutopata usingizi usiku kwa muda mrefu kunaweza sababisha matatizo ya kiakili, kwani hupati wakati tosha wa kupumzika.

Ishara za kukosa usingizi usiku

  • Kuhisi kulala mchanga
  • Uchovu wa kupindukia
  • Kukasirika ovyo ama kuwa na mhemko wa kihisia
  • Kutatizika kuzingatia kazi unayofanya

Matibabu ya kutopata usingizi usiku

Hali ya kukosa kulala usiku kwa muda mfupi huenda isihitaji matibabu kwani huisha baada ya muda. Ikiwa ni vigumu kwako kufanya kazi zako za kila siku, daktari anaweza kushauri utumie tembe za kulala. Kumbuka kutotumia zaidi ya kiwango kilichoshauriwa.

Kwa kutopata usingizi kwa kipindi kirefu, matibabu yanahitajika kusuluhisha masuala ya kiafya yanayokusumbua. Baada ya kufanyiwa vipimo, daktari ataweza kufahamu chanzo cha kutopata usingizi na dawa bora kwako.

Kuepuka hali ya kutopata usingizi usiku

  • Lala wakati sawa kila siku
  • Epuka kutumia simu kitandani
  • Epuka kula dakika chache kabla ya kulala
  • Usitumie pombe na kaffeini dakika chache kabla ya kulala
  • Fanya mazoezi kila siku ama mara kwa mara
  • Unapokosa usingizi, usitumie simu, jaribu kusikiliza nyimbo za kupumzisha ama kusoma kitabu kigumu

Chanzo : Healthline

Soma Pia: Kipi Kinachomfanya Mtoto Wangu Kulia Usingizini?

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Lifestyle
  • /
  • Kukosa Usingizi Usiku: Vyanzo Na Matibabu Ya Suala Hili
Share:
  • Vidokezo Vya Ndoa Kwa Kila Mwanamke

    Vidokezo Vya Ndoa Kwa Kila Mwanamke

  • Jinsi ya Kudumisha Ulaji wa Vitafunio Vyenye Afya Kazini

    Jinsi ya Kudumisha Ulaji wa Vitafunio Vyenye Afya Kazini

  • Lishe Bora Kwa Wanawake Waliofikisha Umri wa Kukoma Hedhi

    Lishe Bora Kwa Wanawake Waliofikisha Umri wa Kukoma Hedhi

  • Vidokezo Vya Ndoa Kwa Kila Mwanamke

    Vidokezo Vya Ndoa Kwa Kila Mwanamke

  • Jinsi ya Kudumisha Ulaji wa Vitafunio Vyenye Afya Kazini

    Jinsi ya Kudumisha Ulaji wa Vitafunio Vyenye Afya Kazini

  • Lishe Bora Kwa Wanawake Waliofikisha Umri wa Kukoma Hedhi

    Lishe Bora Kwa Wanawake Waliofikisha Umri wa Kukoma Hedhi

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it