Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Mambo Muhimu Ya Kufanya Kwa Wanandoa Wanao Taka Kutunga Mimba!

2 min read
Mambo Muhimu Ya Kufanya Kwa Wanandoa Wanao Taka Kutunga Mimba!Mambo Muhimu Ya Kufanya Kwa Wanandoa Wanao Taka Kutunga Mimba!

Kwa wanandoa wanao tia juhudi kuwa wazazi, wakati bora wa kutunga mimba ni mwanamke anapokuwa katika siku zake za rutuba.

Wakati bora wa kutunga mimba ni mwanamke anapokuwa katika kipindi chenye rutuba, kwa kimombo fertile window. Kupevuka hutendeka yai linapo achiliwa kutoka kwa ovari na kusafiri kwenye mirija ya ovari. Yai halina uwezo wa kudumu kwa muda mrefu, lina uhai wa kati ya masaa 12 hadi 24. Mwanamke anapofanya ngono bila kujikinga, manii yana achiliwa kwenye uke wake. Kisha kusafiri hadi kwenye mirija ya ovari. Manii yakipatana na yai, yana lirutubisha. Manii yana uwezo wa kubaki hai kwa muda wa hadi siku tano.

Mwanamke huwa na nafasi zaidi za kutunga mimba anapo fanya mapenzi siku ya kupevuka kwa yai ama siku tano kabla ya siku hii.

  • Kufahamu siku ya kupevuka kwa yai

wakati bora wa kutunga mimba

Njia rahisi zaidi ya kufahamu siku ya kupevuka kwa yai la mwanamke ni kuhesabu siku 14 kutoka siku ya kwanza ya kipindi chako cha hedhi. Ila, kulingana na daktari wa afya ya uke ya wanawake, vipindi vya hedhi hutofautiana na siku ya kupevuka kubadilika.

Kuna baadhi ya wanawake wanao amini kuwa wanaweza kufahamu siku ya kupevuka kwa yai  inapokaribia. Kwa kuona mabadiliko yanayo fanyika mwilini. Dalili iliyo kawaida zaidi ni uchafu wa ukeni kuongezeka, siku chache kabla ya siku ya kupevuka kwa yai. Kwa wanawake wasio makini kuona tofauti hii, wanaweza kutumia kit ya kupima temprecha ya mwili na kufahamu siku hii inapofika. Temprecha ya mwili huongezeka.

  • Mara na wakati bora wa kufanya ngono ili kupata mimba

wakati bora wa kutunga mimba

Wanandoa wanapo jaribu kutunga mimba, ni vyema kufanya tendo hili mara kwa mara ili kuongeza nafasi zao za kutunga mimba. Hakuna wakati hasa ulio bora kuliko mwingine wa kufanya ngono ili kupata mimba. Lakini kuna mbinu zinazo ongeza uwezo wa mwanamke kutunga mimba kwa urahisi.

Kufanya mapenzi kila mara kwa siku huenda kukafanya wanandoa wachoke. Ni vyema kutafuta kinacho fanya kazi kwenu. Kupumzika mara kwa mara ama kuchagua mara mtakazo kuwa mkifanya mapenzi kwa siku.

  • Muda unaochukua kupata mimba baada ya kufanya ngono

Kutunga mimba hufanyika baada ya manii kurutubisha yai kwenye mfumo wa uzalishaji. Hufanyika siku sita baada ya kufanya tendo la ndoa. Kisha yai lililo rutubishwa lita safiri hadi kwenye mji wa mtoto na kujipandikiza kwenye kuta zake. Na ujauzito kuanza.

Kwa wanandoa wanao tia juhudi kuwa wazazi, wakati bora wa kutunga mimba ni mwanamke anapokuwa katika siku zake za rutuba. Fuata vidokezo tulivyo angazia ili kuongeza nafasi zenu za kupata ujauzito.

Chanzo: healthline

Soma Pia: Mama Anaweza Tunga Mimba Anapo Fanya Mapenzi Anapo Nyonyesha?

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Pregnancy
  • /
  • Mambo Muhimu Ya Kufanya Kwa Wanandoa Wanao Taka Kutunga Mimba!
Share:
  • Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

    Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

  • Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

    Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

  • Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

    Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

  • Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

    Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

  • Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

    Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

  • Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

    Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it