Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Tendo La Ndoa Katika Ujauzito: Wakati Wa Kuacha Kufanya Mapenzi Katika Mimba

2 min read
Tendo La Ndoa Katika Ujauzito: Wakati Wa Kuacha Kufanya Mapenzi Katika MimbaTendo La Ndoa Katika Ujauzito: Wakati Wa Kuacha Kufanya Mapenzi Katika Mimba

Daktari humshauri mjamzito wakati wa kuacha kufanya mapenzi katika mimba, anapoanza kuvuja damu na kupata maumivu baada ya tendo la mapenzi

Ikiwa una mimba ama unapanga kupata mimba, huenda ukashangaa wakati wa kuacha kufanya mapenzi katika mimba. Umetafuta habari zote uwezavyo kuhusu kufanya tendo la ndoa katika mimba, na iwapo kuna athari hasi kwa mama na mtoto.

Ngono katika ujauzito ni mada isiyozungumziwa kwa sana. Watu wengi hudhania kuwa sio salama kwa mama mjamzito kujihusisha katika tendo la ndoa. Kutakuwa na mabadiliko katika maisha ya kingono ya mama mjamzito, hata hivyo, ni salama kufanya mapenzi.

Je, ni salama kufanya mapenzi katika ngono?

wakati wa kuacha kufanya mapenzi katika mimba

Tendo la ndoa ni salama katika hatua zote za ujauzito ulio salama. Ujauzito salama ni ule usio kuwa na changamoto kama kupoteza mimba ama kujifungua kabla ya wakati. Mabadiliko ya homoni mwilini mama anapokuwa na mimba huathiri hamu yake ya kufanya mapenzi. Hamu yake hupanda na kushuka ama akakosa starehe kufanya tendo la ndoa.

Mazungumzo ni muhimu kati ya wanandoa katika kipindi hiki, kwa njia hii, mama ataweza kumweleza mchumba wake anachotaka. Mitindo anayofurahia na inayomshinikiza na vitendo vingine vitakavyo mchechemua mbali na ngono.

Wakati wa kuacha kufanya mapenzi katika mimba

  • Sio salama kwa mama mwenye historia ya kupoteza mimba
  • Mama aliye na historia ya kujifungua mapema kabla ya wakati
  • Mwanamke anapoanza kuvuja damu katika mimba
  • Kuwa na ujauzito wa fetusi zaidi ya moja
  • Mama anapotatizika kutokana na placenta previa

Je, tendo la ndoa katika mimba huathiri mtoto

kudumisha ndoa yenye furaha

La. Mtoto huwa amezingirwa na amniotic sac inayomlinda kutokana na hatari zozote.

Baadhi ya wanawake hushangaa iwapo tendo la ndoa linaweza kusababisha kuharibika kwa mimba. La. Ikiwa mimba ya mama ni salama, kufanya mapenzi katika ujauzito hakutaathiri safari yake ya mimba kwa vyovyote vile. Hata hivyo, wataalum wa afya hushauri wanawake kukoma kufanya mapenzi katika wiki za mwisho za ujauzito. Hii ni kwa sababu shahawa huwa na kemikali zinazoweza kuanzisha kubana katika wanawake.

Ikiwa una maswali zaidi kuhusu wakati wa kuacha kufanya mapenzi katika mimba, wasiliana na mtaalum wa afya. Unapokuwa na shaka kuhusu chochote katika safari yako ya ujauzito, ni muhimu kumweleza daktari kuhusu shaka zako. Ishara kama kuvuja damu, kutoa uchafu ukeni, maumivu wakati wa tendo la ndoa huwa hasi na wakati wote zinapaswa kuripotiwa kwa daktari kuhakikisha fetusi haijaathiriwa.

Chanzo: WebMD

Soma Pia: Vyanzo Na Jinsi Ya Kukomesha Kuvuja Damu Katika Mimba

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Pregnancy
  • /
  • Tendo La Ndoa Katika Ujauzito: Wakati Wa Kuacha Kufanya Mapenzi Katika Mimba
Share:
  • Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

    Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

  • Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

    Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

  • Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

    Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

  • Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

    Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

  • Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

    Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

  • Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

    Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it