Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Vyanzo 5 Vya Wanandoa Kukorofishana Wakati Wa Likizo

3 min read
Vyanzo 5 Vya Wanandoa Kukorofishana Wakati Wa LikizoVyanzo 5 Vya Wanandoa Kukorofishana Wakati Wa Likizo

Wanandoa kukorofishana wakati wa likizo ni jambo maarufu, kufuatia kuwa na maoni tofauti. Tazama vyanzo vikuu vya kukorofishana huku.

Kufuatia sababu zisizo eleweka, wanandoa hubishana zaidi wakati wa likizo. Likizo ni wakati wa kupumzika na wapendwa wetu na hakuna anayependa kutumia wakati huo akikorofishana na mchumba wake. Tazama baadhi ya sababu zinazopelekea wanandoa kukorofishana wakati wa likizo na jinsi ya kuziepuka.

Wanandoa kukorofishana wakati wa likizo

  1. Zawadi uliyonunua haikuwa bora kwao

Sio kila mtu ana uwezo wa kufahamu zawadi bora, baadhi ya watu huwa na uwezo dhaifu wa kuwapa wengine zawadi. Ni mojawapo ya sababu maarufu kwanini wanandoa hukorofishana. Na ni rahisi kuelewa kwa nini. Kumpa mwenzi wako kadi ya krisimasi haihisi vyema. Hasa kama wewe ni watu wanaochukua muda na kuwatunza watu zawadi nzuri.

Ili kuepuka kukorofishana na mchumba wako, hakikisha kuwa unapanga muda kabla na uchukue muda kufikiria kuhusu wanacho hitaji. Sio lazima ziwe vitu vya bei ghali, mbali zenye maana na spesheli.

2. Kutumia pesa zaidi wakati wa likizo

kwa nini wanandoa hupigana

Sawa na mambo mengi yanayo husiana na pesa, wanandoa hukorofishana sana mmoja wao anapotumia pesa zaidi wakati wa likizo. Haijalishi iwapo alitumia kununua zawadi ama kufanya mambo mengine, ni sababu maaufu inayowafanya wanandoa kukorofishana wakati wa likizo.

Njia moja ya kuepuka haya ni kukaa chini na mchumba wako na kupanga bajeti ya matumizi yenu yote ya kipindi cha likizo na kuhakikisha kuwa mnazingatia bajeti hiyo. Epuka kutumia pesa zaidi ya uwezo wako hata unapotarajia pesa za zaidi kipindi hicho. Inapofika wakati wa zawadi za marafiki na familia, sio lazima ziwe zawadi za bei ghali, lakini kumbuka zinapaswa kuwa spesheli.

3. Sherehe nyingi za likizo

Sherehe wakati wa likizo ni njia ya kusisimua na kupatana na watu ambao hamjaonana kwa muda mrefu. Hata hivyo, kwenda sherehe nyingi kunaweza kufanya uwe na uchovu mwingi. Ukihisi kuwa unachoka sana, unaweza mweleza mchumba wako kuwa ungependa kupumzika. Ni bora kukosa kuhudhuria sherehe zingine na kupumzika badala ya kuhisi uchovu na kushindwa kufanya kazi zako za kawaida.

4. Mawazo mengi wakati wa kusafiri

wanandoa kukorofishana wakati wa likizo

Kuna baadhi ya wanandoa wanaofanya uamuzi wa kwenda nchi zingine wakati wa likizo, na wakati ambapo kuzuru nchi tofauti ni jambo la kusisimua, huenda ikawa chanzo cha wanandoa kupigana.

5. Maoni tofauti ya vitu vya kufanya wakati wa likizo

Kila familia huwa na mila zake za likizo. Baadhi ya familia huwa na sherehe rahisi nyumbani mwao, wakati ambapo familia zingine hupenda kufanya vitu vikubwa. Ili kuepuka kukorofishana kuhusu jinsi ya kutumia wakati wao wa likizo, jambo la maarifa la kufanya ni kuelewana. Ni vyema kwa wanandoa kukaa chini na kujadili mambo ambayo wangependa kufanya katika kipindi hiki.

Chanzo: Huffingtonpost.com

Soma Pia: Vidokezo 3 Muhimu Vya Jinsi Ya Kutumia Mitandao Kwa Wanandoa

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Relationship & Sex
  • /
  • Vyanzo 5 Vya Wanandoa Kukorofishana Wakati Wa Likizo
Share:
  • Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

    Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

  • Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

    Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

  • Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

    Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

  • Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

    Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

  • Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

    Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

  • Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

    Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it