Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Mambo Ambayo Wanandoa Wanapaswa Kufanya Ila Hawafanyi

2 min read
Mambo Ambayo Wanandoa Wanapaswa Kufanya Ila HawafanyiMambo Ambayo Wanandoa Wanapaswa Kufanya Ila Hawafanyi

Ili kuwa na uhusiano wenye utangamano mzuri, ni muhimu kwa wachumba kuheshimu maisha ya kimapenzi ya wachumba wao na kuyaweka siri.

Kuna sababu nyingi ambazo huenda zinafanya uhusi uhusiano wenu unabadilika sio kama  hapo awali. Na hiyo ni ishara kuwa kuna vitu vinavyopaswa kufanyika. Makala haya yanasaidia wanandoa kufahamu vitu ambavyo hawafanyi, wanandoa wanapaswa kufanya mambo haya!

Wanandoa wanapaswa kufanya haya

wanandoa wanapaswa kufanya haya

  1. Mwaminishe mchumba wako unampenda na kumjali

Ikiwa haumwelezi mchumba wako unavyo mjali na kumpenda mara nyingi uwezavyo, ni vyema kuanza mapema uwezavyo. Mwanasaikolojia wa mapenzi alidhibitisha kuwa ishara za mapenzi za mara kwa mara zina matokeo chanya katika mahusiano. Huenda ikawa rahisi kama kumnunulia zawadi, kumpeleka kula hotelini ama kumkumbatia asipotarajia na kumwambia unampenda. Ishara za kimapenzi huchangia pakubwa katika uhusiano.

2. Kuwa wazi usione haya kuonyesha udhaifu wako

Kulingana na mwandishi wa kitabu cha mapenzi Randi Gunther, ni rahisi kunyamaza na kujiwekea matatizo yetu tunapokuwa na jambo linalo tusumbua ama tunapo kasirishwa na mtu mwingine. Walakini, kufanya juhudi za kuwa wazi na kuweka kiburi chini inapofika kwa mawasiliano kuna afya zaidi. Kutapunguza michezo ya kiakili na kutosikizana kusiko faa. Haijalishi kinachofanyika, wanandoa wanapaswa kuzungumza kinachoendelea akilini mwao bila kumfanya mwingine ahisi haya.

3. Weka maisha yake ya kimapenzi siri

Ili kuwa na uhusiano wenye utangamano mzuri, ni muhimu kwa wachumba kuheshimu maisha ya kimapenzi ya wachumba wao na kuyaweka siri. Hasa inapofika kwa marafiki wenu. Huenda ikaonekana kama jambo nzuri kumweleza rafiki yako kinacho endelea katika uhusiano wenu, ni muhimu kukumbuka kuheshimu mipaka ya mchumba wako. Kufanya hivi kutaboresha uhusiano wenu. Ikiwa una tatizo na mchumba wako, ni vyema kumweleza badala ya kumwongelelea. Kunasaidia kutatua matatizo yenu na kuyaepuka katika siku za usoni.

4. Kutazama sinema pamoja

wanandoa wanapaswa kufanya haya

Kulingana na utafiti uliofanyika, wanandoa wanaotazama sinema pamoja angalau mara moja kwa wiki walikuwa na nafasi za chini za kutengana. Hata hivyo, usimlazimishe mchumba wako kutazama sinema asizo zipendelea. Sinema mnazotizama zinapaswa kuwa za kimapenzi mapenzi. Watafiti waligundua kuwa kutizama na kuzungumzia sinema kuhusu mahusiano ni njia bora ya kupunguza nafasi za kutengana. Iwapo ungependa kuboresha uhusiano wenu kwa njia inayo sisimua na bora, unapaswa kutizama sinema na mchumba wako.

5. Jihusishe katika vitendo vya kujikuza pamoja

Wanandoa wazuri waliokatika uhusiano mwema na wenye afya mara nyingi hujaribu kujihusisha katika vitendo vya kujikuza. Huenda vikawa kutembea pamoja, kufanya mambo mapya ya kusisimua kwa pamoja. Ikiwa ungependa kujenga msingi wa uhusiano wenu ama ndoa yenu, mnapaswa kujaribu njia nyingi na mbalimbali za kuboresha uhusiano wenu kupitia kwa vitendo vya kujikuza.

Soma Pia: Tabia Tatu Zinazo Leta Hujuma Katika Uhusiano

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Relationship & Sex
  • /
  • Mambo Ambayo Wanandoa Wanapaswa Kufanya Ila Hawafanyi
Share:
  • Wanaume: Tahadhari, Usimguze Mwanamke Sehemu Hizi Wakati wa Ngono!

    Wanaume: Tahadhari, Usimguze Mwanamke Sehemu Hizi Wakati wa Ngono!

  • Usimfiche Mchumba Wako Vitu Hivi: Siri 5 Zinazoharibu Ndoa:

    Usimfiche Mchumba Wako Vitu Hivi: Siri 5 Zinazoharibu Ndoa:

  • Makosa Yanayoathiri Maisha Yako ya Uchumba

    Makosa Yanayoathiri Maisha Yako ya Uchumba

  • Wanaume: Tahadhari, Usimguze Mwanamke Sehemu Hizi Wakati wa Ngono!

    Wanaume: Tahadhari, Usimguze Mwanamke Sehemu Hizi Wakati wa Ngono!

  • Usimfiche Mchumba Wako Vitu Hivi: Siri 5 Zinazoharibu Ndoa:

    Usimfiche Mchumba Wako Vitu Hivi: Siri 5 Zinazoharibu Ndoa:

  • Makosa Yanayoathiri Maisha Yako ya Uchumba

    Makosa Yanayoathiri Maisha Yako ya Uchumba

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2022 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it