Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Soma Kitu Kimoja Ambacho Wanandoa Wenye Furaha Hufanya Kila Siku

2 min read
Soma Kitu Kimoja Ambacho Wanandoa Wenye Furaha Hufanya Kila SikuSoma Kitu Kimoja Ambacho Wanandoa Wenye Furaha Hufanya Kila Siku

Jambo ambalo wanandoa wenye furaha hufanya kila siku ili kudumisha uhusiano na utangamano wao na kuwa na ndoa bora.

Kabla ya kuanza, ni vyema kusisitiza kuwa: hii sio njia ya kifupi ya kutatua masuala yenu yote kwa kutumia njia hii ili kusuluhisha matatizo ya kindoa yanayo wakumba. Hata hivyo, ni mbinu ya kweli iliyo jaribiwa ambayo kila wanandoa walio katika ndoa zenye furaha hutumia. Katika machapisho ya hivi karibuni na Macy Williams, aliangazia mambo yote ambayo wanandoa wenye furaha hufanya kila siku.

Ili kubaini vyanzo vya ndoa zenye ufanisi, Williams aliwauliza wanandoa wachache maswali kwanini ndoa zao zilifuzu. Kama anavyo ripoti, walikuwa na maswali mbalimbali kwa jibu hilo. Cha kushangaza ni kuwa wote walikuwa na jambo moja sawa: walizungumza na wachumba wao.

Siri ya kuwa katika ndoa yenye furaha sio kuzungumza tu, ni kwa wanandoa kuwasiliana. Ili kudumisha mawasiliano na mazungumzo yenye afya, wanandoa wanapaswa kufanya vitu hivi vitatu. Soma zaidi ili upate kufahamu jinsi ambavyo wanandoa wanavyo dumisha furaha katika ndoa zao.

Pande Tatu Muhimu Za Mazungumzo

wanandoa wenye furaha

Eleza hisia na mahitaji yako

Hakuna jinsi ambavyo mchumba wako anaweza kufahamu mahitaji yako katika uhusiano usipo mweleza. Hakikisha kuwa unaeleza kinaga ubaga hisia zako - iwapo una furaha ama huzuni. Hakikisha kuwa wakati wote mchumba wako anaelewa kinacho kukumba. Hana uwezo wa kusoma akili yako na kujua matarajio yako. Unaweza kusoma kitu kipya kumhusu pia.

Hata kama unamfahamu mchumba wako kumliko mtu mwingine yule, haimaanishi kuwa wana uwezo wa kujua kila kinacho endelea moyoni na akilini mwako. Ikiwa una kitu akilini, jaribu kuwaeleza kwa njia iliyokomaa bila kutumia maneno ya kukera moyo. Usiwe na uwoga wa kumwonyesha udhaifu wako.

Kuwa mwaminifu

Dakika unapo anza kudanganya ndipo mambo yanapo enda mrama. Iwapo huwezi kuwa mwaminifu na mtu unayempenda, utakuwa mwaminifu na nani mwingine? Mbali na kuwa wazi kuhusu uhusiano wenu, mweleze unapokuwa na siku mbaya kazini ama baada ya rafiki kuumiza hisia zako. Jinsi mnavyo zungumza kuhusu mambo tofauti zaidi, ndivyo mnavyo kuwa na utangamano wa karibu zaidi.

Ulipofunga pingu za maisha na mchumba wako, mlikubaliana kuwa mngesema ukweli wakati wote. Mchumba wako sio mama ama baba ya watoto wako tu, mbali ni mpenzi wako wa maisha. Ni muhimu kuwa mkweli nao wakati wote.

wanandoa wenye furaha

Usi zungumze tu, hakikisha una sikiliza pia

Mbali na kuzungumza na mchumba wako na kumweleza yote unayo hisi na unayofikiria, ni muhimu kusikiliza pia. Huenda mchumba wako akawa anakueleza kuhusu vitu unavyopaswa kubadilisha, ni vyema kuwa na mawazo wazi. Pia, hakikisha kuwa unamsikiliza mchumba wako.

Soma Pia: Ndoa Za Kudumu Muda Mrefu: Ishara Kuwa Ndoa Yako Haiwezi Vunjika

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Relationship & Sex
  • /
  • Soma Kitu Kimoja Ambacho Wanandoa Wenye Furaha Hufanya Kila Siku
Share:
  • Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

    Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

  • Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

    Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

  • Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

    Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

  • Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

    Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

  • Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

    Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

  • Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

    Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it