Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Kufanya Kazi Hizi Na Watoto Kunawasaidia Kuwajibika!

3 min read
Kufanya Kazi Hizi Na Watoto Kunawasaidia Kuwajibika!Kufanya Kazi Hizi Na Watoto Kunawasaidia Kuwajibika!

Watoto kusaidia na kazi za kinyumbani kama vile kusafisha nguo, nyumba na vyombo kunawasaidia kuwajibika na kuwa wanajamii bora.

Kufanya kazi za kinyumbani na watoto kunawasaidia kuwajibika maishani. Pia wanafahamu kuwa ni jukumu lao kusaidia na wala sio kungoja kufanyiwa kazi zote wakati wote. Kufanya hivi kunawasaidia watoto hata wanapoanza maisha yao ya kikazi, kufanya kazi kama timu moja. Watoto kusaidia na kazi za kinyumbani kunawasaidia kuwa wanajamii bora. Tazama baadhi ya kazi za kinyumbani ambazo unaweza kuwahusisha watoto wako!

Watoto kusaidia na kazi za kinyumbani

watoto kusaidia na kazi za kinyumbani

  • Nyumbani

Wapatie wanao jukumu la kutengeneza vitanda vyao jambo la kwanza baada ya kuamka. Wafunze kusafisha vyombo na nyumba, na uwahimize kupanga vidoli vyao wanapomaliza kucheza navyo.

Kwa njia hii, watoto wanakua wakifahamu kuwa wanapaswa kuwajibika na kusaidia katika kazi za kinyumbani bila kungoja kufanyiwa kazi wakati wote.

  • Jikoni

watoto kusaidia na kazi za kinyumbani

Unapotayarisha chakula, waulize watoto wako wakusaidie na kazi rahisi kama vile kuosha vyombo na mboga ama kupanga sahani mezani kabla ya kupakua chakula. Baada ya kumaliza kula, waulize wakusaidie kubeba vyombo na kuvipeleka jikoni. Kwa sababu wangali wachanga, waulize wakusaidie na vyombo visivyo weza kuvunjika na visivyo hatari kwao kama visu.

  • Kufua

Dunia imebadilika na tofauti na hapo awali ambapo watu walifua nguo zao, siku hizi kuna mashine za kusaidia na kazi hizi. Kutumia mashine wakati wote kutawafanya watoto wakue bila kufahamu jinsi ambavyo nguo zinafuliwa. Hata kama una mashine ya kufua, ni vyema mara kwa mara kuwafunza jinsi ya kutenga nguo chafu kisha kuzisafisha. Unapofua mavazi yako, waulize wakusaidie kusafisha vitu vyepesi kama vile soksi.

  • Kazi za shambani

Watoto wanapaswa kufahamu kazi zote, kunawasaidia kuwa watu wanaowajibika maishani. Wazazi wanapofanya kazi za shambani kama vile kulima, kupalilia mimea na kutoa magugu shambani, ni vyema kuwahusisha watoto. Usikubali wabaki nyumbani unapofanya kazi hizi. Hata kama hawatafanya kazi nyingi, wanavyozidi kukua watakuwa na furaha kusaidia katika kazi za kinyumbani bila ubaguzi.

Ni vyema kwa wazazi kuwafunza watoto wa jinsia zote mbili uwajibikaji. Kuna visa ambavyo wazazi hawakubalishi watoto wa jinsia moja kufanya baadhi ya kazi, huku jinsia nyingine ikitwikwa majukumu yote. Kwa mfano, baadhi ya familia hawaamini kuwa vijana wanapaswa kuingia jikoni. Kazi zote za jikoni zikibaki kufanywa na mabinti. Imani hii imepitwa na wakati, na sote tunataka kuishi kwa dunia ambapo wanaume hawaogopi kuingia jikoni hata wanapofunga ndoa. Imani tunazo walea watoto nazo ndizo wanazozibeba uzimani wao.

Watoto wote, wa kike kwa waume wanapaswa kusaidia na kazi za jikoni na pia shambani kwa usawa. Hivi basi, watoto hawa wanafahamu kuwa hakuna kazi iliyotengewa jinsia moja. Kunawasaidia pia kujituma maishani wanapokuwa wakubwa.

Chanzo: WebMd 

Soma Pia: Jukumu La Baba Katika Familia Na Maisha Ya Watoto Wake

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Parenting
  • /
  • Kufanya Kazi Hizi Na Watoto Kunawasaidia Kuwajibika!
Share:
  • Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

    Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

  • Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

    Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

  • Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

    Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

  • Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

    Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

  • Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

    Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

  • Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

    Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it